rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,208
- 20,191
Siyo lazima kila aliye fanya jitihada kukijenga chama chake finally apewe fursa ya kugombea URAIS. Mbona MZEE KAWAWA(MUNGU AMREHEMU) pamoja na kukitumikia cha kwa uadilifu mkubwa hakupata kuomba apendekezwe kugombea urais?na jitihada zote za mbowe kukijenga chama asigombee?
Kwani mtu kuwa kijana ni dhambi au udhaifu?
Mbowe ana mchango mkubwa sana kuliko mtu mwingine yeyote chadema.
Ana haki ya kugombea kama wanachama wengine.
Acha kura za wanachama ndio ziamue.
Mkuu wangu tutobolee hiyo mipango inayofanywa na vibaraka wa ccm walioko CDM.
Zitto atasema chadema ni ya wakristo ili agombee yeye,same way JK alivyopata madaraka,nimeisema kwa njia nyingine na mod unayefuatilia mabandiko yangu,ifute na hii ukitaka.
Dr. Slaa ndio anakubalika sana pia hata kamanda Mbowe naye pia anafaa lakini the so called Zitto hafai koz ni mwanaCCM original na ni disaster kwa chama na Taifa.
Mh. Mbowe,
Kila mtanzania anafahamu kwamba unatamani sana kuwa rais. Kumbuka mwaka 2010 kabla ya CHADEMA kumsimamisha Dr. Slaa kuwa mgombea wa urais, vijana wachache sana walikiunga cchadema mkono. Lakini baada ya kumsimamisha Dr. Salaa, Tanzania ililipuka kwa shangwe na nderemo. Muda unavyokwenda ndivyo CHADEMA inavyozidi kupaa kwani Dr. Slaa anaaminika kwa machungu aliyonayo kwa taifa letu. Dr. Slaa ndiye Nyerere aliyebaki katika hii taifa
Nikiwa mwana CCM anayeiombea mema CHADEMA, na ambaye anajitayarisha kujiunga na ukombozi kabla ya 2015, nakusihi usijaribu kugombea urais 2015. Endeleeni kujenga chama, mwacheni Dr. Slaa agombee. Waambie mamluki kama Zitto na Shibuda wana CCM wenzangu watulie. Wewe bado kijana, tulia mwachie Dr. Slaa alikomboe taifa. Kwani yeye ndio mhimili wa upinzani hapa nchini. Mkifanya kosa kukurupuka na mambo ya urais kama mwana CCM Zitto, utashangaa CHADEMA itakavyo pukutika. Gombea Urais 2020 au 2025
Kuna kundi la vijana mahiri na wataalamu wa hali ya juu Ulaya na marekani ambao wanajipanga kuisaidia CHADEMA ikiwa Dr. Slaa atasimamishwa. Na watu kama Samwel Sitta wanaodahi kwamba CHADEMA haina watu wanaoweza kuongoza serikali, watashangaa mfuriko wa vijana toka Marekani na ulaya pamoja na waliopo nyumbani wakiongozwa na wewe pamoja na Dr. slaa watakavyoibadilisha sura ya Tanzania. Endeleza harakati bila kukiangalia kiti cha urais. waache wakina zitto waendelezo ndoto na tamaa zao za kibinafsi na za madaraka
NB: Kuna siri nzito nitawamwagieni humu siku chache zijazo. Ila kwa sasa, kuweni makini na January Makamba pamoja na Zitto. Kuna mpango maalum wa kuwatumia kukimaliza CHADEMA
Usitufanye watoto wewe,sisi watu wazima na akili zetu usitake kututoa nje ya mada Slaa ndio kila so usitutake kuwafanya watu wachange mawazo yao,najuwa SlaA anawachachafya sana ndio maana hamlali so usituletee pumba zako hapa tuna msimamo na tunajuwa tunachofanya.....kama unampenda Mbowe mchague mwenyewe
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Siyo lazima kila aliye fanya jitihada kukijenga chama chake finally apewe fursa ya kugombea URAIS. Mbona MZEE KAWAWA(MUNGU AMREHEMU) pamoja na kukitumikia cha kwa uadilifu mkubwa hakupata kuomba apendekezwe kugombea urais?
Duuuu. Hakika unataka kutufanya hatuijui Marekani wala UK. Haya, tuambie hawa wataalam wanaojipanga kuja kuisadia Chadema wako kona zipi na wanafanya nini? Hivi umewahi kuhudhuria mikutano ya Chadema Marekani na UK? Kwa ufupi, Tanzania hakuna upinzani, ni njaa tupu. Dr Slaa ni dhaifu kuliko hata huyo Mbowe. Kwa kawaida, Mkatoliki yeyote anaekiuka kiapo cha upadri, huwa kama kichaa tu. mwacheni Mbowe
na jitihada zote za mbowe kukijenga chama asigombee?
Kwani mtu kuwa kijana ni dhambi au udhaifu?
Mbowe ana mchango mkubwa sana kuliko mtu mwingine yeyote chadema.
Ana haki ya kugombea kama wanachama wengine.
Acha kura za wanachama ndio ziamue.
Naona umeminiwa thanks nyingi sana kwa kauli zako hizi za busara.Mbowe hajafaa kuwa rais. Kama anashindwa kuendesha ofisi yake tu ndogo ya gazeti la tanzania daima na ofisi nyingine moshi ambayo imemshinda hadi kaifunga kwa kuwa alikuwa halipi mishahara watu wakaacha. Kwa haya machache tu mbowe hafai hata kidogo kuwa rais. Na mengi sana ya mbowe ambayo yanaonyesha udhaifu wake wa kutoweza kuendesha mambo ila kwa sasa namhifadhi. Abadilike kwani hata ubunge siku sio nyingi viatu vitampwaya na ataweka matambara. Mbowe badilika mwachie slaa walau anaweza japo kuwa na yeye anasfa nyingi sana.