Barua kwa Dr. W. Slaa

Nimevutiwa sana na jinsi watu walivyo na uchungu na jambo la kutafuta haki. Basi kwa majumuisho tuseme CDM ifanye kile ambacho kitaipa uwezekana wa kulibakiza jimbo la Arusha. Kwa hali ilivyo wananchi wako tayari kwa hilo, ninachomaanisha ni mazingira ya kisheria yatakayofanikisha hilo. Ikiwa rufaa ndiyo itakayoipa Chadema legitimacy ya hata tu kuingia kwenye uchaguzi, basi hilo lifanyike bila kigugumizi. Lakini ikiwa inawezekana kuepuka hilo na kuingia kwenye uchaguzi, acha tu waje tuwabutue. Kulipa milioni 50 kwa ajili ya kuokoa maisha ya watanzania si jambo baya, tena hawa huwa wanaiba zaidi ya hizo bila ridhaa yetu. Tunawapa milioni hamsini kama chambo, wakimeza tu, tunawaburuza nje na kuwabanika kama samaki ng'onda. Hawajui tumewachoka sasa na hatuwataki tena hawa hata wafanyaje.
 
Hujaeleweka mkuu unaweza kudadavua chama kitagawikaje hapa.
Mkuu kuna post nimesema viongozi wa juu wa CDM of course na viongozi wa serikali pamoja na wafanyabiashara wakubwa wa Arusha hawako comfortable na Lema. Pia kada ya kati haiko comfortable naye ila ana mtaji mkubwa sana wa vijana wa Arusha na vitongoji vyake. Viongozi wanamuona ni mtu wa vurugu. Wafanyabiashara wanamuona anawaharibia biashara zao kwa kuwaogofya watu kutembelea Arusha. Hivyo basi kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka itakuwa ni nafasi nzuri ya hayo makundi kumweka nje. Hivyo basi CDM haitakata rufaa na itaamua kumsimamisha mtu mwingine na kwa hakika watashinda. Ila sasa nimjuavyo Lema hatakubali kirahisi kuwekwa kando yeye atataka kukata rufaa. Hapo ndipo panapokuja hilo la kukigawa chama. Inaweza ikawa siyo kukigawa mapande bali kukigawa mawazo gongana mengi.
 
Mbona unasema uongo aisee.... Lema mwenyewe amesema hakati rufaa akaenda mbele zaidi akasema hataki kuwa mbunge wa mahakama sasa wewe unaleta hadithi gani tena.
 
Mbona unasema uongo aisee.... Lema mwenyewe amesema hakati rufaa akaenda mbele zaidi akasema hataki kuwa mbunge wa mahakama sasa wewe unaleta hadithi gani tena.
Mkuu alisema hata kama atakuwa amezuiwa kugombea? Kuna vitu viwili hapa: Kuna kukata rufaa kama Lema atakuwa amezuiwa kugombea kwa miaka mitano ili mahakama imtakase na kuweza kugombea. Kuna kutokata rufaa kwa kuwa Lema hajazuiwa kugombea hivyo ana nafasi ya kurudi kugombea ndani y siku 90 na ku retain kiti chake.
 
Luteni umenena safi, but tukiachie chama kitaamua kina wanasheria wazuri waichakachue vizuri hii issue, na amin watakuja na zuri.... mungu bariki CCM.
 

Wellsaid mkuu
 
Ninavyojua mimi kama ni kuzuiwa kwa miaka mitano anaweza kukata rufaa muda wowote hata baada ya uchaguzi kufanyika ili asafishwe kwa ajili ya 2015, kuliko kuzuia uchaguzi na watu kubaki bila mwakilishi (amelisema hili). Kumbuka aliyezuiwa ni Lema si chama na yeye amesema anasubiri maamuzi ya chama ninavyomjua Lema alivyo loyal kwa chama chake sidhani kama anaweza kwenda against na chama chake.
 
Tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu.VIVA CHADEMA.
 
Anaweza akawa loyal ila nyuma yake kuna kundi la vijana ambalo wanaona bila Lema hakuna Arusha!
 
Chadema Mungu awatangulie mfanye maamuzi sahihi kwa umakini mkubwa kwa faida chama na taifa kwa ujumla.
 

Nakuaminia mkuu, ushauri mzuri.
Chondechonde CDM pamoja na kuw na wansheria wengi waliobobea, kuweni makini sana, mtego uliowekwa ni mkali.
 
Kitu kinachotakiwa ni kukata rufaa kwa mahakama ya wananchi ambayo kuhongeka si rahisi, hizi mahakama zingine zote hamuwezi kuni convince.
 
Ndugu Slaa, CCM wameshafanya kosa wanajishauri endapo
waingie kwenye uchaguzi ama la. Ushauri wangu ni kuwa,
whatever the case, nendeni kwenye uchaguzi hata kama Lema
hatogombea najua mtapata mgombea mwingine makini. Kama
chama kitaona Lema asigombee, apewe kazi makao makuu ya
kukiimarisha chama, akusaidie kuzunguka nchi nzima hasa katika
kuimarisha matawi tayari kwa uchaguzi wa ndani na wa serikali za
mitaa.
IMENIKUNA SANA HII!
 

Mkuu jaribu kuelewa jinsi Jaji alivyolikoroga kwa makusudi kabisa na si bahati mbaya, mtego wao CCM na huyo Jaji wao ni huu hapa,

"Lema amehukumiwa kwa kifungu 108 ‘Illegal Campaign' kinachomruhusu kugombea lakini kwenye majumuisho ya hukumu imeandikwa kahukumiwa kwa kifungu 114 "Illegal Practice" kinachomuzuia kugombea kwa miaka 5. Wanataka mkate rufaa au muombe ku review case na hapo itacheleweshwa mwisho mtaambiwa muda ni mfupi wa kuitisha uchaguzi."
 
jaji hajafuata sheria......kapindisha vingele na hata kutengua ubunge...usitegemee haki itendeke mahakamani kwa hii issue kabisa......bora warudie uchaguzi na wananchi watoe hukumu wenyewe....Pia kama wale makada wa ccm walioshinda kesi wakiamua kukata rufaa kwa ajili ya vile vipengele vilivyotupwa nje..then hapa CDM wanaweza ku counter appeal all together......
 
Nimependezwa sana na ushauri wako luteni. Kwa mtazamo wangu ninaomba Dr W Slaa agombee ili arudi bungeni kupambana ili pia watanzania wengine wamfahamu vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…