Wakuu naombeni ushauri, kajua kametoka sasa shemeji yenu ananilazimisha nikaoge eti kisa keshachemsha maji. Me nimemwambia sijisikii kuoga maana sio lazima. Hapa tumekwazana kwa ajili ya hilo.
Eti jamani kuna haja ya kulazimishana kuoga wakati kila mtu na mwili wake halafu siku zenyewe ambazo sijaoga ni tatu yaani siku tatu tu.
Arusha hamna baridi kama ya Njombe, nimeishi kule Oldonyosambu nilikua natoa bangi kule napeleka Moro na Dar hali ya kule ni ya baridi sio baridi yenyewe hasa. Njoo Njombe uone baridi yenyewe.
inachangia mshawasha kwa wanawake na kupelekea "ngono" ya hali ya juu na ndio sababu kuna UKIMWI sana huu mkoa na pia kuna mimba nyingi sana za watoto.
Nipo Njombe kwa shughuli zangu binafsi na hii ndio hali ya hewa ya leo. Baridi kali 9ยฐC asubuhi hii na usiku ndio ilikua kali zaidi.
Nawatakia siku njema waungwana.
Ila pia nimegundua huku watu wanafunga biashara mapema sana na wanachelewa kufungua, nikiwa makambako pale sokoni kwao nikaona mgambo wanapuliza filimbi saa 11 jioni eti watu wafunge biashara. Nilishangaa sana.
Ukiwa umeenda kwa malengo hata hao wanawake hutawaza.Hatupaswi kufikiria ngono kila wakati Njombe ni home na kila wakati narudi hua Sina hata muda wa kutafuta wanawake.the same nikiwa Arusha,mbeya,Moro,Moshi nk..piga kazi iliyokupeleka huko๐๐๐๐๐