BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
SIRI ya muda mrefu ya kinacholifanya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuendesha shughuli zake kwa kiwango cha chini na kutaka kupandisha bei ya umeme kila siku hatimaye imefichuka.
Katika hali iliyowaacha vinywa wazi wajumbe na wadau waliokutana jana katika kikao cha kujadili maombi ya Tanesco ya kutaka kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 155, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo William Mhando alikiri kuwa wanashindwa kufanya kazi kikamilifu kutokana na ukosefu wa fedha, na kwamba wanaidai serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kiasi cha sh bilioni 137 ambazo zingefidia gharama za uendeshaji wa shirika hilo.
Kujulikana kwa madeni hayo, kuliwafanya wajumbe wengi waliokutana katika mkutano ulioitishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) na kuwashirikisha timu ya viongozi wa Tanescco wakiongozwa na mkurugenzi wake pamoja na wajumbe wa bodi ya Tanesco akiwamo Mbunge wa Lupa Victor Mwambalaswa (CCM) kukataa ombi la shirika hilo la kutaka kupandisha bei ya umeme.
Akichangia katika mkutano huo, mwanaharakati na mdau wa maendeleo, Renatus Mkinga, alisema haiwezekani wananchi waumizwe na kubebeshwa mzigo wakati serikali ikikalia fedha za Tanesco.
Mkinga bila kutafuna maneno alisema ni lazima serikali ilipe madeni yanayofikia sh bilioni 87 huku Zanzibar ikidaiwa sh bilioni 50 ambazo zitaliwezesha shirika hilo kuimarisha shughuli zake.
Mdau huyo aliwashambulia viongozi wa serikali kwa kile alichokiita kutokuwa na huruma kwa watu wake kiasi cha kusababisha mgawo wa umeme.
"Hivi sasa suala la umeme linaendeshwa kisiasa zaidi kuliko utaalamu na hili linachangiwa kwa kiasi kikubwa na kukosekana kwa uzalendo na uhuru kwa wananchi. Kama bei ikipandishwa, tutashuhudia wizi ukitamalaki," alisema Mkinga.
Alieleza pia kutofurahishwa kwake na kitendo cha watumishi wa Tanesco kupewa uniti 700 kila mmoja, kwa madai kuwa kinachangia kurudisha nyuma maendeleo kwa kulifanya taifa kuwa na tabaka la watu wenye nacho na wasio nacho kila kukicha.
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza la Ushauri la Serikali, William Buhunire, alisema baraza hilo licha ya kupitia ombi hilo la dharura la Tanesco la kupandisha umeme kwa asilimia 155, wamelitaka shirika hilo kufanya juhudi kukusanya madeni yake kwa wadaiwa sugu.
"Hakuna sababu wala haja ya kuongeza bei ya umeme kwa kiwango kikubwa, lazima mhakikishe mnakusanya kiasi hiki kikubwa cha fedha na muandae mnyumbuliko wa kuwabaini wale wote mnaowaita wadeni sugu ili waweze kulipa fedha hizi," alisema Buhure.
Alisema Tanesco ilipaswa kuonyesha gharama halisi na badala yake wametumia gharama za ziada za kulisha umeme wa dharura kutoka kwa kampuni za Symbion na Aggreko pamoja na mafuta ya mitambo yao.
"Hali kama ikiachwa na Tanesco kuruhusiwa kupandisha umeme, inaweza ikaleta madhara makubwa na hata kuathiri uchumi wa nchi na inaweza kuwafanya wawekezaji wasivutiwe tena kuja nchini kwa kuogopa gharama za uendeshaji," alifafanua Buhure.
Naye Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma zinazodhibitiwa na Ewura, Profesa Jamidu Katima, alisema kutokana na utafiti uliofanyika imebainika kuwa Tanesco imeshindwa kutoa mchanganuo unaosababishwa na gharama za umeme wa dharura.
"Gharama za Tanesco kuzalisha umeme ni sh 139,293 huku mapendekezo ya mwaka 2012 ni 248,536 sawa na asimilia 74.84, hizi ni baadhi tu ya gharama ambazo hazipaswi kuongezeka na hazina uhusiano na dharura iliyopo hivi sasa nchini," alisema Profesa Katima.
Alisema baraza hilo linapinga hatua ya watumiaji wengine kulipia gharama za wafanyakazi wa Tanesco zipatazo sh bilioni 16 huku ikiitaka Ewura kutoyakubali maombi hayo.
Awali akiwasilisha mada katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhando, alisema Tanzania imekuwa ikitoza gharama za chini kwa watumiaji wa umeme ikiwa tofauti na nchi nyingine.
"Kutokana na hali hii, tunaiomba Ewura iidhinishe ongezeko la bei ya dharura, ambapo bei ya wastani ya kuuza umeme hivi sasa ni sh 141 kwa uniti ipande hadi sh 359 kwa uniti kuanzia Januari 2012, na sababu kubwa ni kuiwezesha Tanesco kukabiliana na gharama za uendeshaji kutokana na juhudi za kuondoa mgawo wa umeme," alisema Mhando.
Hatua ya kupingwa ongezeko la umeme, imekuja siku chache tu baada ya mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (CHADEMA) kupinga hatua hiyo, akieleza kuwa itawaumiza wananchi wa kipato cha chini.
Mnyika alisema badala ya kupandisha, serikali kupitia shirika hilo, ingetafuta mbinu nyingine za kupata fedha za kuendeshea shughuli za Tanesco badala ya kuwaongezea wananchi bei ya umeme.
Katika hali iliyowaacha vinywa wazi wajumbe na wadau waliokutana jana katika kikao cha kujadili maombi ya Tanesco ya kutaka kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 155, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo William Mhando alikiri kuwa wanashindwa kufanya kazi kikamilifu kutokana na ukosefu wa fedha, na kwamba wanaidai serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar kiasi cha sh bilioni 137 ambazo zingefidia gharama za uendeshaji wa shirika hilo.
Kujulikana kwa madeni hayo, kuliwafanya wajumbe wengi waliokutana katika mkutano ulioitishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) na kuwashirikisha timu ya viongozi wa Tanescco wakiongozwa na mkurugenzi wake pamoja na wajumbe wa bodi ya Tanesco akiwamo Mbunge wa Lupa Victor Mwambalaswa (CCM) kukataa ombi la shirika hilo la kutaka kupandisha bei ya umeme.
Akichangia katika mkutano huo, mwanaharakati na mdau wa maendeleo, Renatus Mkinga, alisema haiwezekani wananchi waumizwe na kubebeshwa mzigo wakati serikali ikikalia fedha za Tanesco.
Mkinga bila kutafuna maneno alisema ni lazima serikali ilipe madeni yanayofikia sh bilioni 87 huku Zanzibar ikidaiwa sh bilioni 50 ambazo zitaliwezesha shirika hilo kuimarisha shughuli zake.
Mdau huyo aliwashambulia viongozi wa serikali kwa kile alichokiita kutokuwa na huruma kwa watu wake kiasi cha kusababisha mgawo wa umeme.
"Hivi sasa suala la umeme linaendeshwa kisiasa zaidi kuliko utaalamu na hili linachangiwa kwa kiasi kikubwa na kukosekana kwa uzalendo na uhuru kwa wananchi. Kama bei ikipandishwa, tutashuhudia wizi ukitamalaki," alisema Mkinga.
Alieleza pia kutofurahishwa kwake na kitendo cha watumishi wa Tanesco kupewa uniti 700 kila mmoja, kwa madai kuwa kinachangia kurudisha nyuma maendeleo kwa kulifanya taifa kuwa na tabaka la watu wenye nacho na wasio nacho kila kukicha.
Kwa upande wake Mjumbe wa Baraza la Ushauri la Serikali, William Buhunire, alisema baraza hilo licha ya kupitia ombi hilo la dharura la Tanesco la kupandisha umeme kwa asilimia 155, wamelitaka shirika hilo kufanya juhudi kukusanya madeni yake kwa wadaiwa sugu.
"Hakuna sababu wala haja ya kuongeza bei ya umeme kwa kiwango kikubwa, lazima mhakikishe mnakusanya kiasi hiki kikubwa cha fedha na muandae mnyumbuliko wa kuwabaini wale wote mnaowaita wadeni sugu ili waweze kulipa fedha hizi," alisema Buhure.
Alisema Tanesco ilipaswa kuonyesha gharama halisi na badala yake wametumia gharama za ziada za kulisha umeme wa dharura kutoka kwa kampuni za Symbion na Aggreko pamoja na mafuta ya mitambo yao.
"Hali kama ikiachwa na Tanesco kuruhusiwa kupandisha umeme, inaweza ikaleta madhara makubwa na hata kuathiri uchumi wa nchi na inaweza kuwafanya wawekezaji wasivutiwe tena kuja nchini kwa kuogopa gharama za uendeshaji," alifafanua Buhure.
Naye Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Watumiaji Huduma zinazodhibitiwa na Ewura, Profesa Jamidu Katima, alisema kutokana na utafiti uliofanyika imebainika kuwa Tanesco imeshindwa kutoa mchanganuo unaosababishwa na gharama za umeme wa dharura.
"Gharama za Tanesco kuzalisha umeme ni sh 139,293 huku mapendekezo ya mwaka 2012 ni 248,536 sawa na asimilia 74.84, hizi ni baadhi tu ya gharama ambazo hazipaswi kuongezeka na hazina uhusiano na dharura iliyopo hivi sasa nchini," alisema Profesa Katima.
Alisema baraza hilo linapinga hatua ya watumiaji wengine kulipia gharama za wafanyakazi wa Tanesco zipatazo sh bilioni 16 huku ikiitaka Ewura kutoyakubali maombi hayo.
Awali akiwasilisha mada katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhando, alisema Tanzania imekuwa ikitoza gharama za chini kwa watumiaji wa umeme ikiwa tofauti na nchi nyingine.
"Kutokana na hali hii, tunaiomba Ewura iidhinishe ongezeko la bei ya dharura, ambapo bei ya wastani ya kuuza umeme hivi sasa ni sh 141 kwa uniti ipande hadi sh 359 kwa uniti kuanzia Januari 2012, na sababu kubwa ni kuiwezesha Tanesco kukabiliana na gharama za uendeshaji kutokana na juhudi za kuondoa mgawo wa umeme," alisema Mhando.
Hatua ya kupingwa ongezeko la umeme, imekuja siku chache tu baada ya mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (CHADEMA) kupinga hatua hiyo, akieleza kuwa itawaumiza wananchi wa kipato cha chini.
Mnyika alisema badala ya kupandisha, serikali kupitia shirika hilo, ingetafuta mbinu nyingine za kupata fedha za kuendeshea shughuli za Tanesco badala ya kuwaongezea wananchi bei ya umeme.