Barabara ya Banana-Kitunda-Kivule-Msongola: Halmashauri ya Ilala/ TARURA mtusaidie

Swash Bizo

Senior Member
Jan 29, 2011
141
93
Wakazi wa maeneo inapopita hii barabara kila mwaka kipindi cha mvua wanateseka sana na usafiri. Barabara ina mashimo mengi na makubwa yamejaa maji ya mvua yaliyotuama. Tunaamini Halmashauri ya Ilala/TARURA watasikia kilio cha wapiga kura wa jimbo la Ukonga na kuwarekebishia hii barabara katika hadhi ya lami. Nawasilisha.

Updates.....

TAARIFA KWA WAKAZI WA JIMBO LA UKONGA

Mbunge wa Jimbo la Ukonga na Naibu Waziri OR Tamisemi Mhe *Mwita Waitara* atafanya ziara Jimboni siku ya Jumamosi tar 25/05/2019 kuanzia saa 3 asubuhi kwa ratiba ifuatayo

Saa 3:00 asubuhi atakuwa kata ya Kivule mtaa wa Kelezange eneo la Matembele 2 ambapo atashuhudia makabidhiano ya barabara ya Kitunda - Kivule - Msongola kwa mkandarasi atakayejenga kwa kiwango cha lami.

Saa 6 mchana atakuwa Kata ya Msongola mtaa wa Yangeyange

Saa 7 mchana
atakuwa Kata ya Pugu kushuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa mradi mkubwa wa maji ya DAWASCO.

Saa 9 jioni
atakuwa Kata ya Buyuni mtaa wa Kigezi chini kuzungumza na wakazi wa kata ya Buyuni juu ya mradi wa umeme wa REA na changamoto zinazowakuta wananchi hao.

Saa 10:30 jioni
atatembelea Barabara ya Majohe Viwege kujionea Hali halisi ya barabara hiyo ilivyoaribikia na mvua.

Katika ziara hiyo, Mhe. Waitara atafuatana na wakuu wa Idara za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, TARURA, TANESCO pamoja na DAWASCO.

WANANCHI wa maeneo hayo pamoja na ya jirani mnaombwa kujitokeza kwa wingi katika mikutano hiyo

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ukonga
24/05/2019
 
Ila Chapombe katelekeza sana hiyo mitaa! Na hiyo barabara huwa inapangiwa fungu la lami lakini huwa haiwekwi. Sijui shida nini pale

Ila wangeweka lami pia kupitia Nyantira basi kungekuwa na daladala za kutoka Msongola hadi Tandika kupitia Fremu Kumi, Kivule, Kitunda shule, Nyantira, Kwa Mparange (Milanzi), kwa mama Kibonge , Davis Corner

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mm naona sasa hv tumuachie Mungu tu ...hamna namna

Sent usingJamii Forums mobile app
 
Wakazi wa maeneo inapopita hii barabara kila mwaka kipindi cha mvua wanateseka sana na usafiri. Barabara ina mengi na makubwa yamejaa maji ya mvua yaliyotuama. Tunaamini Halmashauri ya Ilala/TARURA watasikia kilio cha wapiga kura wa jimbo la Ukonga na kuwarekebishia hii barabara katika hadhi ya lami. Nawasilisha.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mbunge naibu Waziri, na bado mnapiga,malofa sana nyie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na wananchi wahuku kwakweli ni wavumilivu sana!

Mimi ninawazo, tupatikane wadau kasha’s wakazi wa huku tufahamiane ikibidi tufike kwa mkuu wa wilaya/ mbunge/diwani ama manager wa tarura waweze kutupa taarifa kamili.

HALI NI MBAYA MNO
 
Waitara mchumia tumbo kama wachumia tumbo wengine, aliondoka kwa mbwembwe anaenda kutuletea maendeleo ... Sasa hivi majibu yake ni yupo bizy na majukumu ya kitaifa
Ni limbukeni kiufupi..
 
Wakazi wa maeneo inapopita hii barabara kila mwaka kipindi cha mvua wanateseka sana na usafiri. Barabara ina mengi na makubwa yamejaa maji ya mvua yaliyotuama. Tunaamini Halmashauri ya Ilala/TARURA watasikia kilio cha wapiga kura wa jimbo la Ukonga na kuwarekebishia hii barabara katika hadhi ya lami. Nawasilisha.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hakika unaweza fikili huku kivule ni nchi nyingine na si Tanzania, HALI NI MBAYA MNOOOO we barabara gani mpaga bodaboda hawataki kupita? no public transport kabisaa na bado viongozi wakija wana level ili waheshimiwa waone mambo si mabaya sana , MUNGU anawaona
 
Hakika unaweza fikili huku kivule ni nchi nyingine na si Tanzania, HALI NI MBAYA MNOOOO we barabara gani mpaga bodaboda hawataki kupita? no public transport kabisaa na bado viongozi wakija wana level ili waheshimiwa waone mambo si mabaya sana , MUNGU anawaona
Sijapita hizi siku mbili za Mvua naamini Hali ni Mbaya zaidi sijui kama kutakuwa kuna gari linaenda kule
 
Na wananchi wahuku kwakweli ni wavumilivu sana!

Mimi ninawazo, tupatikane wadau kasha’s wakazi wa huku tufahamiane ikibidi tufike kwa mkuu wa wilaya/ mbunge/diwani ama manager wa tarura waweze kutupa taarifa kamili.

HALI NI MBAYA MNO
Wakurya wamejaa huko
 
Wakazi wa maeneo inapopita hii barabara kila mwaka kipindi cha mvua wanateseka sana na usafiri. Barabara ina mashimo mengi na makubwa yamejaa maji ya mvua yaliyotuama. Tunaamini Halmashauri ya Ilala/TARURA watasikia kilio cha wapiga kura wa jimbo la Ukonga na kuwarekebishia hii barabara katika hadhi ya lami. Nawasilisha.

Updates.....

*TAARIFA KWA WAKAZI WA JIMBO LA UKONGA*


Mbunge wa Jimbo la Ukonga na Naibu Waziri OR Tamisemi Mhe *Mwita Waitara* atafanya ziara Jimboni siku ya Jumamosi tar 25/05/2019 kuanzia saa 3 asubuhi kwa ratiba ifuatayo

*Saa 3:00 asubuh* atakuwa *kata ya Kivule mtaa wa kelezange* eneo la matembele 2 ambapo atashuhudia makabidhiano ya *barabara ya kitunda Kivule msongola* kwa mkandarasi atakayejenga kwa kiwango cha lami,

*Saa 6 mchana* atakuwa *kata ya Msongola* mtaa wa yangeyange

*Saa 7 mchana* atakuwa *kata ya pugu* kushuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa mradi mkubwa wa maji ya dawasco,

*Saa 9 jioni* atakuwa *kata ya buyuni mtaa wa kigezi chini* kuzungumza na wakazi wa kata ya buyuni juu ya mradi wa umeme wa rea na changamoto zinazowakuta wananchi hao

*Saa 10:30 jioni* atatembelea *barabara ya majohe viwege* kujionea Hali halisi ya barabara hiyo ilivyoaribikia na mvua,

Katika ziara hiyo Mhe Waitara atafatana na wakuu wa idara za halmashauri ya manispaa ya ilala, Tarura, tanesco pamoja na dawasco,

WANANCHI wa maeneo hayo pamoja na ya jirani mnaombwa kujitokeza kwa wingi katika mikutano hiyo

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ukonga
24/05/2019

Sent from my iPhone using JamiiForums

Sitoamini mpaka nione walau mita kumi za lami
 

Mambo ya kuwapa lowest bidders bila kujari kama kazi itafanyika ni tatizo. Naona CRB wameibuka
 
Back
Top Bottom