Bar yateketezwa kwa moto Zanzibar

M-bongotz

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
1,734
405
Kuna taarifa zimetolewa kama Breking news kwenye radio one kuwa kuna bar moja kubwa na maarufu huko Zanzibar imeteketezwa kwa moto, inasemekana ni bar ya nne kuteketezwa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu.,mlio huko Zenji hebu mtujuze kinachoendelea.
 
Ni gymcarner club malindi wateja tumesepa na bili
Kuna taarifa zimetolewa kama Breking news kwenye radio one kuwa kuna bar moja kubwa na maarufu huko Zanzibar imeteketezwa kwa moto, inasemekana ni bar ya nne kuteketezwa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu.,mlio huko Zenji hebu mtujuze kinachoendelea.
 
Ila jamaa wana maisha ya kijima kweli
Ivi kufunga ni suala la nchi au mtu binafsi?
 
Mimi sipo zanzibar na hizo taarifa ndio nazisikia ila kama ni kweli hiyo bar ni ya nne kwa mwezi huu kuchomwa moto basi zanzibar sio sehemu ya tanzania maana sasa huo ni udini. Kuwa kisiwa chenye chimbuko la uislamu isiwe tabu hao wapuuzi wakumbuke kuwa pia huko kuna watu wengi tu wenye imani tofauti na yakwao ambao wanahaki za kimsingi kuishi maisha yenye uhuru pasipo kujali ni kipindi gani. Inamaana kama ni mwezi mtukufu basi na wengine ndio wasifanye starehe zao? Basi kitangazwe kama ni kisiwa cha kiislamu kinachoongozwa na sheria na kanuni za dini ya kiislamu ili tujue moja! Yaani kila mwaka zanzibar katika mwezi kama huu wa mfungo ni shida tupu hebu waache ujinga!
 
Hawa ndugu zetu na underground movements zao wanajua kweli wanachokifanya,ni wabaya kuliko ugonjwa wa AIDS
 
Na huo Muungano nao isiwe ni nongwa na kisingizio za kutuharibia mila zetu na taratibu zetu za maisha. Sizungumzii suala la dini hapa. Lakini katika mwezi kama huu wa Ramadhan tokea mababu na mababu zetu walikuwa na utaratibu wa kufunga mikahawa yote kufunga sehemu zote za starehe kwa wakati huu. Na wakiristo walikuwepo hapa na wamekuwepo tokea Muungano haupo hadi kuja kwa Muungano huu uliodumu kwa miaka zaidi ya 40. Utaratibu huu umekuwa ukiheshimiwa huko nyuma (ndani ya Muungano) . La kushangaa sasa (miaka hii ya 2000-2010) tunaona hii kebehi ya kupuuza maadili na taratibu zetu za maisha Zanzibar. Hili halivumiliki, hata iwe kwa kisingizo cha Muungano na uhuru wa mtu kufanya atakacho. Kuchoma moto si kitendo ki\zuri ni uvunjaji wa sheria. Lakini pia kuvunjwa utaratibu wetu (kwa kebehi tu) ni uvunjajii wa sheria kwa mtizamo wetu. Tuweni na mizani na tuwe waungwana wa kutumia busara. hivi kuna tatizo gani tukakubali kufunga mabaa na kuheshimu taratibu za wenzetu wenyejii wa Zanzibar?
 
Usikute kuna mkono wa al shabaab, this terrorist group is penetrating into our territory very slowly. Wamehodhi biashara za bureau de change Livingstone yooote na mind you their rates are negotiable. Kuna hotel mtaa wa kwanza kutoka uhuru / livingstone kama unakwenda kidongo chekundu on your right (second or third bldg) al huba kama hujui kisomali it'll be the nightmare. Kuna nyingine inaitwa TANSOMA kule karibia Gold Star (nyerere road) lile lilikuwa godown wamenunua hawa majangili wa baharini. Maneno tunayasikia huku mtaani, and these pirates are randomly buying beacg plots along the north coast shores - kuanzia Tegeta mpaka Bagamoyo. Sijui huko ZNZ wana nini.
Al shabaab, the East African al Qaeda. Gadffi kawalaumu al - Qaeda kwa kuanguka kwake!
 
Back
Top Bottom