Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,091
- 136,650
NN wewe mchokozi sana, unataka uzi ufungwe tena?
mbona mimi sijawahi kupata hiyo ban
mbona mimi sijawahi kupata hiyo ban
Ila kweli hata mimi nimegundua kuwa NN sio mchokozi kama nilivyokuwa nafikiria hapo zamani,.. Nnachojua ni kuwa ukichokozwa kesi yako huwa haimaliziki mapema...Mimi wala sio mchokozi kihivyo. Mara nyingi huwa nachokozwa. Na nikichokozwa it's on. We'll go rounds.
Sitaki uzi ufungwe ila nitashangaa usipofungwa maana hawa watawala na viranja wa JF huwa hawapendi kukosolewa (ingawa wao nahisi watakuwa na mtazamo tofauti).
Ila kwa vile nimeshasema kuwa nitashangaa kama uzi hautafungwa, sitashangaa pia wakiuacha uendelee ili kuonyesha tu nilikuwa na makosa katika kusadiki kwangu kuwa utafungwa.
Tusubiri tuone.
Mambo swahiba.Ooooh!
Oooooh!
Mambo swahiba.
NN samahani kwa kuchakachua uzi wako..
Hilo la ban mie sina cha kuchangia manake nimewahi kulimwa mara 1 na ile kweli niliistahili so sikuona tatizo na ingenishangaza kama mods wasingenilima ile ban...
mambo mabaya. Humuoni swahiba wetu nyani ana malalamiko.
Wee Mwajuma acha uchokozi wako bana
Nimewahi asee, mwaka jana , miezi ya mwisho mwisho! Nilijichanganya jukwaa la siasa nkajifanya nimekunywa maji ya bendera... Nilikuwa mstari wa mbele natetea chama kwa zaidi ya masaa ma3, mwisho wa siku nikaambulia ban...Na wewe umewahi kuwekwa lupango? Lini ilikuwa? No way bana....it can't be. Yaani wewe na ban hata hamuendani kabisa.
NN ni mtu mwema swahiba, ukiona analalamika ujue mods wamemtendea ndivyo sivyo...mambo mabaya. Humuoni swahiba wetu nyani ana malalamiko.
unakohoa au unashangaa??Ooooh!
Oooooh!
Mmmh, kama hatakuja mkaanga sumu muda si mrefu, sijui.
Naskia israel wa ban au unyakuo wa sredi akizunguka zunguka hapa.
Nawapa pole in advance.