Baniani mbaya kiatu chake dawa

Chibudee

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2016
Posts
1,775
Reaction score
2,408
Leo katika pita pita zangu huko mitandaoni nimekutana na hii picha yenye caption ya aina yake.

Ineelezea mazingira halisi ya binadamu na tabia zetu unaweza tenda wema kwa moyo na kujitolea lakini bado ukaonekana si kitu na ukalipwa fedheha na kejeli vile vile.

Lakini picha hii na caption yake inatufunza jambo kwanza kabisa tusichoke kusaidiana panapohitajika msaada.

Lakini zaidi usipende wema wa malipo sababu utaisononesha nafsi bure jifunze kutenda na kuenda zako.

Kwani baniani mbaya kiatu chake dawa.

Jioni njema wakuu



Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…