Baniani mbaya, kiatu chake dawa: Wa kushukuriwa ni Lowassa

Kama si lowassa // RAIS angelikuwa membe as for their planed,tungedumaa kwa miaka 10 tena huku R1,akiendelea kukuimu urais.
 
Magufuli mbn toka kitambo ndo maamuzi yake ayo lowasa awezia..Msikosehe heshima kabisa kwa utendaji wake kuhusisha na mtu ambae alisha shindwa toka zamani..
 
TUPATUPA-MZEE WA LUMUMBA; kwanza nakupongeza kwa andiko lako la ukweli,ingawa mimi si muumini wa chama lako la kijani.Tunachohitaji ni mabaliko ya kweli ili tupate maaendeleo kama Taifa..Prezda ameanza ameanza vizuri....Kama tuna mapenzi na nchi yetu lazima tukubali kumuunga mkono POMBE MAGUFULI,amethubutu amtangulie Mungu pele atafanikiwa tu.....
 
Mbona sikuwahi kumsikia Lowassa akikemea ufisadi na rushwa? Hata alipohojiwa maswali na mtangazaji wa BBC, Zuhura Yunus bado tu alikwepa kuzungumzia ufisadi na rushwa? Nadhani Lowassa ni wa kupuuzwa tu. Hakuna chochote ambacho Lowassa amefanya ili kumchora rais wa Tanzania. Rais Dkt Magufuli anakemea rushwa, anakemea ufisadi, ukwepaji kodi na matumizi ya hovyo ya fedha ya umma. Vitu ambavyo Lowassa asingethubutu kupambana navyo kamwe.
 
Jamani mi naona aloandika mzee Tupa Tupa ni ya kweli ila tuendelee kuvuta subira walau 100 days tutatoa tasmini yetu . sisi wapinzani ndo tunachokitaka nchi iendeshwe kwa haki na usawa, wasiwepo mabwenyenye katika nchi yetu. Nawasilisha
 
hebu wataalam wa uchumi wanifahamishe
uchumi wa nchi je unakuzwa kwa kubana matumizi ama kwa kufungua mianya mingi ya kuingiza pato ikiwemo pato la kigeni?
kwa mfano:

nyumbani wazazi huwa wanatumia hela kwa uangalifu huku wakiwa wanatafuta mbinu mbadala za kukuza kipato manake with time matumizi na gharama za maisha huwa zinapanda.

je katika uchumi wa taifa hili limekaaje?

Uelewa wako mdogo sana wewe mwanamama kuhusu masuala ya uchumi. Hivi unajiona wewe unajua sana kuliko wachumi wetu!? Maana swali umeliuliza kwa namna ya kukosoa as if you know best! Inasikitisha kuona mtu huelewi umuhimu wa ku-cut public expenditure ili ku-stabilise economy na kushusha inflation kwa large percentage. Anachofanya Dkt Magufuli kwa maana nyingine ni masahihisho ya kile ambacho rais mstaafu Kikwete alikikosea. Kuruhusu sana pesa kwenye economy bila control yoyote ina madhara zaidi kuliko kubana matumizi.

Hatua ambazo Dkt Magufuli anafanya kwa sasa za kupunguza pesa kwenye mzunguko kwa sisi wenye akili kubwa tunajua faida yake. Nyinyi wengine ngojeeni matokeo...maana hata nikijaribu kukuelewesha hapa bila shaka hutoelewa. Hivyo relax usubiri positive impact ya hatua za rais.
 
Ni kwa kiasi kikubwa Mkuu Lizaboni. Let us call a spade a spade, not a big spoon!

Mzee Tupatupa

Mbona sijawahi kusikia Lowassa akikemea ufisadi na rushwa na hata kukemea wakwepaji kodi? Huyo Lowassa ni fisadi ndio maana hayo maeneo hakuwahi kuyagusia. Tafadhali koma kufananisha matendo ya Dkt Magufuli na maneno ya fisadi Lowassa.
 
Last edited by a moderator:
Mimi na Lowassa picha hazipandi. Sijawahi na wala sitawahi kumuunga mkono Lowassa katika harakati zake za kisiasa. Lakini, kwakuwa mimi ni muumini wa ukweli daima, namsifu Lowassa kwa kumchora Rais wa Tanzania ambaye kiukweli sasa tumempata. Tumempata Rais aliyesemwa na kuchorwa na Lowassa. Ni Dr. John Pombe Magufuli. Wa awamu ya tano hapa Tanzania.

Ndugu Edward Ngoyai Lowassa, alipokuwa CCM, alikuwa ni mwanachama wa kwanza kutangaza nia ya kuwania Urais kupitia CCM. Alitangaza nia tarehe 30/5/2015 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Lowassa, wakati akitangaza nia, alimchora Rais atakiwaye Tanzania kama ni Rais mwenye uthubutu, imara, mwenye kutoa jambo likatekelezwa na kadhalika. Rais kweli kweli.

Lowassa, hata kwenye kampeni zake akiwa CHADEMA, kuanzia mwanzo hadi mwisho, alikuwa akihubiri mabadiliko ya kimfumo na kisera. Nasema kwa kujiamini kuwa ni Lowassa ndiye mwanzilishi wa Rais tuliyempata na 'mhubiri' wa sera ya mabadiliko ya kimfumo na kisera. Ilifikia mahali, CCM kupitia kwa Dr. Magufuli wetu, tukakubali kuendana na hali halisi. 'Tukaiba' sera za CHADEMA na sisi kuanza kuhubiri mabadiliko. Tukaongeza kuwa mabadiliko ya 'kweli'. Ikalipa.

Mambo anayoyafanya Rais Magufuli ni mambo mazito. Yanabadili mfumo na sera. Mambo ya kukataza, kufuta, kubadili na kuanzisha mengine ni mambo yanayogusa moja kwa moja sera na mfumo uliokuwepo. Si mchoro wa Lowassa huu? Namsifu Rais Magufuli kwa 'kukopi na kupesti' mambo na kusonga mbele. Anakopi na kupesti kile wananchi walikuwa wakikisubiri na kutamani kwa muda mrefu.

Tumsifu mkimbiaji lakini tusisahau anayemkimbiza. Sifa tumpe Rais wetu kwa kufanya mambo mazuri na makubwa. Lakini, Lowassa ndiye aliyetuonesha kuwa yawezekana!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

-kucopy na kupaste hapana. ingekuwa hivo asingefuta shamrashamra za sherehe maana Lowasa kutangaza nia tu alitumia mamilioni ya fedha. kukusanya sahihi za wadhamini ndo usiseme. naona Magufuri anatekeleza ya moyoni mwake.
 
yabidi kuelewa pia kuna watu wapo kwaajili yakujua nani anajua zaidia yake yani kama chki n balansi ndio maana unakuta mtu anauliza kitu najibu lipo hapo hapo,
 
Wewe mnafiki si ulisema mabadiliko hayawezi kutokea ndani ya CCM? Leo unarudi kinyumenyume....inaonekana kile kidawati chako cha pale ufipa kimeanza kukuchosha
Naona CCM kwa CCM mmeanza kuparuana, teh teh tehe!

MZEE TUPATUPA wa Lumumba ni mwana CCM kindakindaki, wewe maamuna wa juzi tu huwezi kumkaribia hata robo kiukada, ila mara nyingi huwa anaponzwa na tabia yake ya kusema ukweli.
 
VUTA-NKUVUTE, ni mapema mno kusema lolote, ni mapema mno kusema tumepata raisi tuliemhitaji, naona hata media sana wanaanza kumbeba mheshimiwa raisi, bado, JK nae alianza kwa kasi hii hii, usishangae pumzi ikakata mapema kuliko hata JK!
 
Last edited by a moderator:
Mabadiliko ya kweli yanaletwa na CCM. Uroho na tamaa ya madaraka vimemponza Lowasa. Aende zake. Magufuli anasifika kwa utendaji wake kila alipokuwa. Huyo Lowasa ni bla blaa tu. CCM haikukosea kumsimamisha Magufuli

Magufuli pia amshukuru Lowassa kwa kumpa kura za ushindi kule dodoma lowassa alipokatwa.
 
Wakushukuriwa ni Mungu, maana aliyopanga yametimia sawa sawa na maombi ya Watanzania
 
Naona CCM kwa CCM mmeanza kuparuana, teh teh tehe!

MZEE TUPATUPA wa Lumumba ni mwana CCM kindakindaki, wewe maamuna wa juzi tu huwezi kumkaribia hata robo kiukada, ila mara nyingi huwa anaponzwa na tabia yake ya kusema ukweli.

Hahahahaaa hii sidhani kama DuppyConqueror ataweza kujibu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom