Nimemskiliza Fr. Charles Kitima, nimemsikiliza Dr. Wilbroad Slaa, nimemsikiliza Adv. Boniface Mwambukusi, nimemsikiliza Mange Kimambi, nimemsikiliza Rostam Aziz, nimemsikiliza Tundu Lissu, nimemsikiliza Freeman Mbowe.
Nimelisikiza Bunge, nimemsikiliza RC Albert Chalamila, nimemsikiliza Rais Samia Suluhu Hassan, nimeskiliza Gerson Msigwa Msemaji wa Serikali, na nimemsikiliza Salim Asas; to mention a few.
Baada ya kuwasikiliza, nimetafiti, nimelinganisha, nimetofautisha kauli zao, fikra zao, hoja zao, na matendo yao, nikapata majawabu haya:
1. Mkataba wa Bandari haujitetei wenyewe, ni mkataba wa kifisadi unaohitaji nyongeza ya maneno ili uwe halali na ukubalike kwa Watanzania. Watanzania wameukataa.
2. Nchi kwa sasa haina uongozi madhubuti; nchi inajiongoza yenyewe.
3. Kuna kikundi cha wahuni wachache wanapora rasilimali za nchi na wanaziweka kwenye mikono ya wageni kwa jina la uwekezaji.
4. Katiba ya nchi na sheria za nchi zimeanajisika. Utawala bora na utawala wa sheria umetoweshwa kwa ulafi wa maslahi ya watu binafsi.
5. Taifa linahitaji hatua za haraka na dharura kuikwamua nchi na machafuko yanayoweza kutokea muda wowote kuanzia sasa. Umaskini umekithiri, achilia mbali pengo kubwa la walionacho na wasio nacho linavyoongezeka kwa kasi.
6. Wakati umefika raia wote wa Tanzania kuamka kudai haki ya nchi yao. Kurejesha mamlaka, madaraka, na nguvu mkononi mwao kutoka kwa viongozi walioko madarakani.
7. Naunga Mkono Mawakili wazalendo Adv. Emmanuel Chengula, Adv. Boniface Mwambukusi, Adv. Livino Ngalimtumba, na Adv. Alfonce Lusako wanaokusudia kufungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam "Under Extreme Certificate of Urgency" ili Mahakama ikatupe tafsiri ya huu mkataba unaweka rehani usalama wa nchi. Bunge la JMT limewasaliti wananchi badala ya kuisimamia serikali. Iingie mikataba mizuri, Bunge limegeuka kuwa "Genge la serikali" la kupingana na wananchi.