Bakari Shime aliwahi kufanikiwa katika lipi ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,600
218,005
Kuboronga kwa Serengeti Boys kwenye michuano ya vijana hakuwezi kupita tu hivi hivi kama upepo bila kujadiliwa .

Mafanikio ya timu yoyote ya soka kwa kiwango kikubwa huchangiwa na kocha wa timu husika , ikumbukwe pia kwamba ubovu wa kocha waweza kuchangia kuboronga kwa timu.

Leo sina mengi sana , nimeangalia wale vijana wakicheza na Niger kupitia ZBC2 , Nikashangaa na kujiuliza walifikaje kwenye michuano Mikubwa kama ile , wakati natafakari nikagundua kwamba walitokea JUU YA MEZA .

Baada ya hapo nikaanza kufuatilia mafanikio ya kocha wake aitwaye Bakari Shime , kiukweli mpaka sasa sijaona mafanikio ya mtu huyu kiasi cha kupewa kazi ya kufundisha timu hii , Shime aliyewahi kufundisha JKT RUVU ( niko tayari kusahihishwa ) , timu inayopanda na kushuka ligi kuu hana na wala hajawahi kuwa na uwezo wa kufundisha soka , kama kuna anayefahamu mafanikio yake atuwekee hapa.

Inakuwaje mtu asiye na sifa yoyote kukabidhiwa timu ya Taifa ? Ukiangalia wale vijana walivyokuwa wanacheza utagundua jambo moja tu , kwamba waliambiwa wakishinda watapata hela na kwenda kombe la dunia , baaaasi !!!! Wala hawakuambiwa wacheze vipi ili washinde , hata kupiga mpira juu hawakuweza !

Ni kweli kwamba wapo wanaoshinda mamilioni ya hela kwa Kubeti , baada ya kutumia tsh 500 , lakini si kwenye soka , soka inataka uwekezaji wa kweli hasa , Wachezaji waandaliwe kwa kiwango cha juu tena chini ya Mwl anayejua aliyezungukwa na historia yenye mafanikio haswa , haya mambo ya Bahatisha Ndulute hayatatufikisha popote , ni bora kujitoa kuliko kudhalilishwa mara kwa mara .

Natanguliza uzalendo , asanteni .
 
Kuboronga kwa Serengeti Boys kwenye michuano ya vijana hakuwezi kupita tu hivi hivi kama upepo bila kujadiliwa .

Mafanikio ya timu yoyote ya soka kwa kiwango kikubwa huchangiwa na kocha wa timu husika , ikumbukwe pia kwamba ubovu wa kocha waweza kuchangia kuboronga kwa timu.

Leo sina mengi sana , nimeangalia wale vijana wakicheza na Niger kupitia ZBC2 , Nikashangaa na kujiuliza walifikaje kwenye michuano Mikubwa kama ile , wakati natafakari nikagundua kwamba walitokea JUU YA MEZA .

Baada ya hapo nikaanza kufuatilia mafanikio ya kocha wake aitwaye Bakari Shime , kiukweli mpaka sasa sijaona mafanikio ya mtu huyu kiasi cha kupewa kazi ya kufundisha timu hii , Shime aliyewahi kufundisha JKT RUVU ( niko tayari kusahihishwa ) , timu inayopanda na kushuka ligi kuu hana na wala hajawahi kuwa na uwezo wa kufundisha soka , kama kuna anayefahamu mafanikio yake atuwekee hapa.

Inakuwaje mtu asiye na sifa yoyote kukabidhiwa timu ya Taifa ? Ukiangalia wale vijana walivyokuwa wanacheza utagundua jambo moja tu , kwamba waliambiwa wakishinda watapata hela na kwenda kombe la dunia , baaaasi !!!! Wala hawakuambiwa wacheze vipi ili washinde , hata kupiga mpira juu hawakuweza !

Ni kweli kwamba wapo wanaoshinda mamilioni ya hela kwa Kubeti , baada ya kutumia tsh 500 , lakini si kwenye soka , soka inataka uwekezaji wa kweli hasa , Wachezaji waandaliwe kwa kiwango cha juu tena chini ya Mwl anayejua aliyezungukwa na historia yenye mafanikio haswa , haya mambo ya Bahatisha Ndulute hayatatufikisha popote , ni bora kujitoa kuliko kudhalilishwa mara kwa mara .

Natanguliza uzalendo , asanteni .

Wamejitahidi, wamecheza mechi nyingi za majaribio tena na timu kubwa tu na wameshinda. Mpira uko hivyo, jana haikuwa siku yao, tukubali kushindwa na tuwapongeze vijana wetu. Kutokujali mafanikio yao kufika pale sio sawa kabisa, kwani ilikuwaje wao ndio waende baada ya kutolewa hiyo timu nyingine? Acha hizo mkuu.
 
Tuwape moyo hata hapo walipofikia binafsi naona wako vzur pakurekebisha n padogo tuu.. Mbona kim pousen hujamsema alianza nao mapema
 
Tuwape moyo hata hapo walipofikia binafsi naona wako vzur pakurekebisha n padogo tuu.. Mbona kim pousen hujamsema alianza nao mapema
Huyu aliwahi kufundisha Taifa Stars na hakuna alichokifanya , na katika hili naiomba TAKUKURU ICHUNGUZE MKATABA WA KIM POULSEN , mtu aliyeshindwa kufundisha , lakini akarudi kwa njia ya panya , Kwangu mimi Sunday Kayuni ni bora kuliko huyu .
 
Huyu aliwahi kufundisha Taifa Stars na hakuna alichokifanya , na katika hili naiomba TAKUKURU ICHUNGUZE MKATABA WA KIM POULSEN , mtu aliyeshindwa kufundisha , lakini akarudi kwa njia ya panya , Kwangu mimi Sunday Kayuni ni bora kuliko huyu .
haya ungeandka tang mwanzo yangekua na maana ila kwasasa ntakuona mnafiki tu
 
Huyu aliwahi kufundisha Taifa Stars na hakuna alichokifanya , na katika hili naiomba TAKUKURU ICHUNGUZE MKATABA WA KIM POULSEN , mtu aliyeshindwa kufundisha , lakini akarudi kwa njia ya panya , Kwangu mimi Sunday Kayuni ni bora kuliko huyu .

Hujui unachesema. Tatizo ni TFF sio Kim Poulsen.

Kim ndio amefikisha timu hapo swala ni TFF badala ya kumpa Kim team wamempa Bakari Shime na Kim kama mshauri wa bvench la ufundi.

Kilichotokea jana, nilikijadili na Malinzi kabla ya mechi. Wasicheze mchezo wa kujilinda.

Bakari Shime amazozana na Kim akikataa ushauri na badala yako akafanya mabadiliko kwenye vikosi karibia kila mechi.

Jana alimuweka Straika wa timu "Yohan Mkomola" eti anamuweka kwa mechi zijazo na kumuanzisha Ibrahim Abdalla Ally ambaye alimtoa dk46.

Pia alimuanzisha Zebery ADA badala ya Enrique Vitalis Nkosi aliyeanza mechi ya Angola then kaawaambia wadefend na pia hataki ushauri wa KIM.
 
Wamejitahidi, wamecheza mechi nyingi za majaribio tena na timu kubwa tu na wameshinda. Mpira uko hivyo, jana haikuwa siku yao, tukubali kushindwa na tuwapongeze vijana wetu. Kutokujali mafanikio yao kufika pale sio sawa kabisa, kwani ilikuwaje wao ndio waende baada ya kutolewa hiyo timu nyingine? Acha hizo mkuu.
Mfumo waliotumia kipindi chote cha maandalizi ilikuwa wanacheza Mpira wao taratibu sasa Jana wamechezesha Mpira usio na mipango wa kubutua na kukimbilia mbele... Na kocha anaonekana kuridhika maana yake walifuata maelekezo yake
 
Back
Top Bottom