Bajeti ya Serikali mwaka wa fedha 2016/2017 itatisha sana

Hatukusanyi 1.8 ndyo kwanza tunahangaika kupata 1.3. Pili kumbuka madeni namiradi iliyokwama kaka yani mpka magufuli aanze kutekeleza miradi yake itakuwa kwenye bajet ya tatu 2018/19
 
Kwa misingi mibovu ya kiuchumi iliyobomolewa na Kikwete na kuwekwa mipya na mizuri hili la bajeti kujitegemea ndiyo lilikuwa lengo, hata ukitazama Kikwete alipochukuwa tulikuwa wategemezi wa takriban asilimia 50 ya bajeti lakini katuacha tunategemea tunategemea kama asilimia 10 tu.

Kweli nimeamini kuna watu wehu hapa nchini na hawataisha. Ila tutaheshimiana tu na itajulikana nani ni nani na alikuwa anafanaya nini
 
Uza mashangingi yote,nunua vitara na rav4,asietaka apande basi

Sawa, lakini wasinunue vitara na rav 4 , nyumbu (Kiwanda cha Jeshi) wapewe fungu la kutosha watengeneze magari ya kiraia na kwa viongozi wetu pia ...! Yaani hapo tutajitegemea asilimia 100. TUJITEGEMEE....! Inawezekan
 
JERUSALEMU

Hongera kwa posti nzuri haya ndio mambo ya kuongelea hapa.
Ni kweli sekta ya utalii inapoteza mapato mengi sana kuna nchi zinaendeshwa kwa kutumia utalii pekeyake.
Pia usisahau sekta ya UVUVI.
 
Kwa sababu waliandika bajeti yetu ni trilion 23 wakati hatuwezi kukusanya hata trilion 11 kwa mwaka ( wastani kwa mwezi ni mil 900). Uwe unatumia akili na macho ili uweze kung'amua mambo ya kisanii!

Huo si ukweli. Kafanye tena homework yako.
 
Hiyo ni kwa TRA peke yake, kumbuka serikali ina magawio ilikowekeza, mashiraka ya umma, bonds n.k, mikopo etc tutafika tu usihofu

nataka kukubaliana na hilo, ila hapo hapo kuna mikopo ya nje na bado kuna kampeni ya kuomba kusamehewa hiyo mikopo.
 
Labda nikusaidie kihesabu hapo..
ikiwa makusanyo yataendelea kuwa angalau 1.3T, then kwa mwaka ni 15.6T pungufu ya 6.4T kufikia 22T. Sasa kama ataendelea kubana matumizi na kuyapunguza yasiyo ya lazima kuna uwezekano mkubwa wa kuokoa hata 2-3T (mfano kukata safari zisizo na umuhimu, mashangingi, maadhimisho yasiyo ya lazima, n.k.)
Aidha, akiongeza ukusanyaji mapato katika sekta nyingine mfano madini, utalii, mauzo ya gas nje, mazao ya misitu, kilimo, ufugaji, n.k. hakika hiyo pungufu kuna uwezekano mkubwa sana wa kuimaliza ama kubakisha pengo dogo sana.
Jambo jema ni pale itakapofikia kukusanya angalau 1.6T kwa mwezi, kweli itakuwa ni neema kubwa kwa nchi hasahasa ikiwa usimamizi utaendelea kufanyika kwa ufanisi.

nadhani ni vizuri wamebadilisha na jina la Wizara, kipato sio kila kitu, kinaitaji "mipango" kwahiyo kuita wizara ya Fedha na Mipango ni sahihi kabisa.

mtu anaweza kupokea 500K kwa mwezi akafanya makubwa kuliko anayelipwa Milioni 2. nimeona.

MKpo from Local banks na mashirika ya umma kama PSPF, NSSF, NHIF nk.

mkopo, sasa kila mwaka bajeti inaongezeka mkopo wa mwaka jana au miaka 10 iliyopita utalipwa lini, hiki kipato cha 1.3T ni kidogo sana. inahitajika mipango sahihi.

Watu watashangaa, JPM ndio kwanza ameanza kazi baada ya miezi 6 mtaona. Kuna sehemu bado hajazishika vizuri kama vile kwenye utalii, ukifika Serengeti pale uone foleni ya kulipa ya watalii utajiuliza hivi kweli zile pesa zote zinakwenda serikalini au kuna wajanja wachache pale wanafanya mchezo, hii nchi bana tutaelewana tu tuombe uzima wa JPM kuwashughulikia hawa waliofikiri wana hati miliki ya hii nchi. Hiyo bajeti ya T22 ni cha mtoto.

pesa za serengeti sio zote zinapelekwa hazina, mbuga zina wafanyakazi pia wanahitaji kulipwa mishahara, kama ulivyosikia TANAPA wanahangaika na mishahara, sasa ukiangalia geti la Serengeti usijiulize maswali sana, kwa kifupi ni hazitoshi.

Mkuu bajeti yetu huwa ni tegemezi kwa asilimia 48 (48%). Usishangae, hiyo 22tn 52% tu ndiyo mapato ya ndani.

ndio nafahamu hilo na ndio mana maelezo ya Raisi yameonyesha kwanini ni tegemezi, na kuna uwezekano pia bajeti ikawa ni ya kimaandishi tu. namba zinasomwa bungeni lakini ukweli ni mwingine.

Bila shaka ulisha wahi kusikia 1. Nakisi ya bajeti ie badjet deficit 2. Bajeti ya Tz hufadhiliwa kwa kiwango cha 30+%

mipango dhabiti itasaidia. ila makusanyo yanaonekana kidogo sana, ngoja tuone sector zote zina potential ya kuchangia kiasi gani chini ya Raisi Magufuli kisha tutaona kama inawezekana.
 
Mimi nasoma bajeti kila mwaka, nilishangaa sana Raisi aliposema mapato ya mwezi yanakaribia 1.3 Trillion.

Nikajiuliza kama matumizi ni 22T kama mwaka jana na tunakusanya 1.3 kwenye mwezi mzuri, inamaana hiyo tofauti ya pesa itatoka wapi? Au bajeti yetu ni maandishi tu?

Kama matumizi ya serikali kwa mwaka ni 22T, na inaendelea kuongezeka kila mwaka by the way, inabidi tukusanye sio chini ya 1.8 trillion kila mwezi.

Kutoka bageti ya 2015/2016
1. Bageti yote pamoja na miradi ya maendeleo ni tr 22..
2. Kuendesha serikali tuu ..mishahara etc ilikua ni tr 16
3. Wastani wa mapato ilikua ni tr12

Hii ina maana kwa serikali iliyo pita kuendesha serikali tuu ilihitaji tr4 kutoka kwa wahisani..

Kwa wastani wa makusanyo ya mapato ya tr 1.4 serikali itakua imesha jihakiishia kujiendesha yenyewe isipo kuwa miradi ya maendeleo..

Sasa kama serikali itakusanya wastani wa tr 1.8 kwa mwezi.. hapo ni pazuri kwa maana kwamba inaweza kujiendesha na kufadhili miradi ya maendeleo yenyewe..

Kumbuka kuwa matumizi ya kuendesha serikali kwa tr16 yalikua yamejaa anasa nyingi sana.. kwa jinsi magufuli alivyo bana matumizi pamoja na kuwa kuna mambo yameongezeka kama elimu bure bado naamini bageti ya kuendesha serikali itakua chini ya tr16..

Kwa msingi huo serikali ikiweza kukusanya tr30 kwa mwaka maana yake serikali haita kuwa ombaomba wala kukopa kwa ajili ya miradi ya maendeleo labda wahisani wanitolee bila malipo yoyote..

Big up magufuli..
 
kuanzia Julai, 2016 kima cha chini kitakuwa Tsh 630,000/= kwa sekta ya umma na Tsh 540,000/= sekta bibafsi.

PAYE itashuka hadi 8%
 
Kwa misingi mibovu ya kiuchumi iliyobomolewa na Kikwete na kuwekwa mipya na mizuri hili la bajeti kujitegemea ndiyo lilikuwa lengo, hata ukitazama Kikwete alipochukuwa tulikuwa wategemezi wa takriban asilimia 50 ya bajeti lakini katuacha tunategemea tunategemea kama asilimia 10 tu.
acha ujinga wako na ujinga wa mpenda chini wako...a.k.a mpenda Kati...si ajabu ashakutafuna wewe
 
Ujenzi na miundombinu naomba atenge hata trilion 6 ili mifumo ya maji taka majiji yote iwekwe upya pamoja na kuboresha minor roads
 
Wafanyabiashara wengi huku mtaani hawalipi kodi,pia wafanyabiashara hawana EFD kwahiyo serikali inakosa VAT 18%,Kwenye mauziano/kupangisha hapa serikali inakosa fedha nyingi sana,Waziri wa fedha na kamishina wa TRA wayafanyie kazi hayo mambo ASAP maana watapunguza PAYE na kutoa 50mils kila kijiji.
 
Kwa misingi mibovu ya kiuchumi iliyobomolewa na Kikwete na kuwekwa mipya na mizuri hili la bajeti kujitegemea ndiyo lilikuwa lengo, hata ukitazama Kikwete alipochukuwa tulikuwa wategemezi wa takriban asilimia 50 ya bajeti lakini katuacha tunategemea tunategemea kama asilimia 10 tu.

Mbona unazuuunguka si uende tu moja kwa moja kwenye dhamira yako
 
Back
Top Bottom