Ndugu waungwana,
Hivi Serikali na Bunge wanamatatizo gani na namba??
Kiini cha andiko langu,
Bajeti kwa mwaka 2016/17 ilikuwa Tillioni 29.5, mwaka huu unao anza July 31.7
Nukuu kutoka taarifa ya Waziri wa fedha Bungeni Dodoma
"Taarifa za awali zinaonesha kuwa, Pato la Taifa kwa mwaka 2016 lilikua kwa wastani wa asilimia 7.0, sawa na ilivyokuwa mwaka 2015. Hali hii imechangiwa na kasi kubwa ya ukuaji katika shughuli za: Uchimbaji Madini na Mawe (asilimia 16.5); Usafirishaji na Hifadhi ya Mizigo (asilimia 15.6); Habari na Mawasiliano (asilimia 13.5); na Huduma za Kifedha (asilimia 11.3). Aidha, kwa upande wa utekelezaji wa azma ya Taifa ya kujenga uchumi wa viwanda, shughuli za uzalishaji viwandani zilizidi kuimarika, zikiongezeka kwa asilimia 7.8, ikilinganishwa na asilimia 6.5 mwaka 2015"
"Kwa mwaka 2016/17 Serikali ilitenga shilingi bilioni 11,820.503 kwa ajili ya bajeti ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 8,702.697 zilikuwa za ndani na bilioni 3,117.805 fedha za nje. Hadi Februari 2017, fedha zilizokuwa zimetolewa ni shilingi bilioni 3,975.4, ikijumuisha fedha zilizotolewa kwa Halmashauri, sawa na asilimia 34 ya bajeti ya maendeleo. Kati ya kiasi hicho, fedha za ndani zilikuwa shilingi bilioni 3,103.6 na fedha za nje shilingi bilioni 871.8"
"Hadi kufikia Februari 2017, mapato kutoka vyanzo vyote yalifikia sh. bilioni 15,372.4 sawa na asilimia 79 ya lengo la kipindi hicho. Kati ya hizo:
- (i) Mapato ya kodi yalifikia shilingi bilioni 9,306.0 sawa na asilimia 95 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 9,764.2;
- (ii) Mapato yasiyo ya kodi yalifikia shilingi bilioni 1,305.7 sawa na asilimia 72.5 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 1,806.2;
- (iii) Mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa yalikuwa shilingi bilioni 310.6 sawa na asilimia 70 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 443.6;
- (iv) Mikopo ya ndani ilifikia shilingi bilioni 3,506.7 sawa na asilimia 78 ya makadirio ya shilingi bilioni 4,479.6 katika kipindi hicho; na
- (v) Misaada na mikopo nafuu kutoka kwa Washirika wa Maendeleo ilikuwa shilingi bilioni 1,253.6, sawa na asilimia 40 ya lengo la kipindi hicho la shilingi bilioni 3,117.2"
Hapa somo la historia linahusika. Kama katika historia ya mapato yetu hatujawahi kukusanya zaidi ya Tsh 20 Tillioni, iweje tupange bajeti ya Tillioni 32 kasoro???
Kuna miujiza gani tutafanya kufikia mapato hayo ili hali historia ya nyuma na mwelekeo wa hali ya uchumi siku zijazo havitupi matumaini hayo???
Watalaam wetu vipi jamani? Hili nalo linahitaji shule?
Katika familia, kuna watu wanapanga bajeti zao za mwaka kuna mapato na matumizi. Lazima uweke mapato na matumizi yanayo endana na uhalisia wa mambo. Kuna kupata zaidi au kidogo pia kuna kutumia zaidi kuliko au kidogo kuliko makadirio. Ila tofauti hizi siyo kubwa kiasi hicho karibu mara mbili ya uhalisia wa mambo, iweje kwa Serikali hata kama ni Nchi?
Hii ni kuishi kwa matumaini. Tunalisha akiri zetu kuwa hiki nakile kitafanyika ila kila mwaka hatufikii malengo hayo. Kwa nini tusipange kulingana na mapato yetu???
Kama huna uwezo wa kukusanya zaidi ya tillioni 17 kwa mwaka kwa nini usipange bajeti chini ya Tillioni 17?