Bajeti ya Elimu kugomewa na wabunge wa CCM?

Bajeti ya Elimu kugomewa na wabunge wa CCM?

kukumweupe

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2020
Posts
439
Reaction score
599
Mbunge wa bukoba vijijini ambayepia ndio katibu wa wabunge wa ccm ametufukuza kazi walimu wote wa rweikiza school tuliokwenda kumshtaki kwa mkuu wa mkoa na kuwadanganya wale wa dar es salaam kuwa amewapanga wabunge wa ccm na kuwambia nini wasema mpaka serikali ikubali kubeba mzigo huo wa kuwalipa mishahara walimu wote wa shule binafsi wakiwamo wa shule anazo miliki ,st Anne Marie ,sun shine ,brilliant na hii ya hapa bukoba ya rwikiza ambayo inatumia jina lake.

Sisi walimu wa hapa bukoba ametufukuza wote baada ya kwenda kumshtaki kwani tangu mwaka huu uanze hajatulipa hata mia na wale wa kule dar es salaam amewambia atawafukuza kama sisi ikiwa wataendelea kumsumbua .sisi tutapambana naye mpaka kieleweke tu.

Akiwawahutubia walimu wa shule zake zilizopo jijini dar na pwani mbunge huyu ambaye ni mdhurumaji amesema kuwa wabunge wote wa ccm watakoa changia bajeti ya elimu amewambia nini waseme na wapambane mpaka serikali ikubali kuwalipa la sivyo bajeti haitapita kwani huo ndio msaada kwa walimu wake ,kwa wale waliotazama bunge siku ya ijumaa watakumbuka wabunge kama mwijage ambaye ni raifiki yake alivyoshupalia jambo hili na kesho ndio bajeti itapigiwa kura il.

Walimu wa shule za st maria ya huko dar es salaam .sun shine kibaha ,brilliant na hapa bukoba hazijalipwa kwa miezi mitatu huku sisi hajapewa hata shilling tangu mwaka huu uanze huku wazazi wamelipa pesa na ametufukuza baada ya kumshtaki kwa mkuu wetu wa mkoa Gaguti

Kesho waziri Ndalichako atasulubiwa na wanaccm wenzake ambao pesa wanakula na hawataki kutulipa,


Tusubili kesho


Kukumweupe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walimu husika mnahoja ya msingi madai yenu ila mmechanganya mjadala.Wawekezaji sector binafsi elimu wana hoja za msingi nyingi kuweza kupatiwa ruzuku na serikali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanajidanganya, serikali haiwez kuwalipa watu ambao haiwajui!
Ikifanya hivyo, basi itabid iwalipe wananchi wote, maana asilimia kuwa iko kwenye changamoto mbalimbali za kiuchumi!

Serikali waiache ishughulike kwanza na covid-19! Ila hizi habari ni porojo tu
 
ila tuache masihara ualimu bongo bahati mbaya, Yaani mtoto wako bora umpeleke veta mapemaaa kuliko kumpeleka A level then university akasome Bsc ed/ Baed
 
Anaangalia maslahi yake binafsi badala ya maslahi ya nchi. Ninachojua shule binafsi, wanafunzi wanalipa ada ya muhula kabla ya kwenda shule na wanaenda na pay-in slip kuonesha malipo.

Kwa maana hiyo, ada zipo shuleni na walimu wa shule hizo wanatakiwa kulipwa na shule na sio Serikali. Je, shule hizo zinawalipa walimu wao kupitia nini?
 
Malalamiko yenu walimu ni ya msingi. Kuna watu wanapenda dhuluma, ukidai haki yako unapewa vitisho au kufukuzwa kazi ila kwa uandishi wako nina mashaka kama wewe ni mwalimu kweli. Kama wewe ni mwalimu nawapa pole wazazi unaowafundishia watoto wao.
 
Nilivyo muelewa ni kwamba pamoja na kuwa mbunge huyu anapambana kuungamkono kutopitisha bajeti kama serikali haitoahidi kuwalipa walimu wa serikalini madai yao... Yeye binafsi hajawalipa walimu wa shule zake binafsi na wakidai maslahi yao anatishia kuwafukuza kazi!
 
Back
Top Bottom