Bado wewe kuandamana

Bado wewe kuandamana

cenzo

Senior Member
Joined
May 7, 2015
Posts
124
Reaction score
28
Wazee wa JF Habari za leo,

Hivi hii nchi ni wapi tunaelekea?

Swali langu, hivi kweli hawa waandamaji wa miaka hii ni kweli wanatafuta haki zao au ni vibaraka tu wanaotumiwa na Wanasiasa? Nimeshuhudia leo pale Karume, jijini Dar es salaam walemavu wakiandamana na kudai haki zao zitekelezwe.

Swali langu; je, hapo miaka ya nyuma wananchi wa Tanzania hatukuzijua haki zetu?

Na kama ni kweli kuwa miaka ya sasa watu wamefunguka macho na masikio kwa kuzijua haki zao tofauti na zamani, basi ni vyema tukampongeza mheshimiwa rais kwa kutupa uhuru huu tulioukosa kwa miaka mingi.

Lakini pia nina wasiwasi na haya maandamano ya sikuhizi na hii migomo huenda tu ni chochezi au kampeni za wanasiasa fulani ili kuja kujikombea kura za uchaguzi.

Kwanini migomo na maandamano yamelipuka sana wakati huu tukielekea kwenye uchaguzi mkuu?

Mungu ibariki Tanzania na watu wake, dumisha upendo na umoja.
 
Mkuu hivi ni kweli huoni sababu ya watu kugoma na kuandamana au unatuzingua tu hapa

Wanafunzi wa elimu ya juu hawajapewa pesa kwa zaidi ya wiki tatu,na njia za kawaida za kufuatilia zimedunda,wanafanyaje?

Kuna sababu nyingi sana za kuigomea serikali sema waTZ ni wavumilivu sana
 
Wala sijaona Kuwa hawana sababu ya kuandamana ninachoshangaa je hizo haki hawakuzijuwa miaka yote isipokuwa wakati huu tukielekea kwenye uchaguzi mkuu
Huoni Kuwa ni kusababisha matatizo kwa taifa letu waungwana tujipende wenyewe na kujihurumia kabla haijafikia kuja kuonewa huruma na mataifa mengine kama tunavyowaonea huruma wenzetu walio kwenye machafuko

Amani ni tamu na machafuko ni machungu.
 
eti unasema rais ametoa uhuru? wewe upo dunia gani?? kikwete huyo unayemsifia amesaini sheria ya kufunga watu midomo!
 
Hali ilivyokuwa leo
 

Attachments

  • 1432242338740.jpg
    1432242338740.jpg
    35.2 KB · Views: 105
  • 1432242355807.jpg
    1432242355807.jpg
    44 KB · Views: 100
  • 1432242368698.jpg
    1432242368698.jpg
    57.1 KB · Views: 104
  • 1432242380697.jpg
    1432242380697.jpg
    56.1 KB · Views: 101
Ila hata mimi nalaani hii migomo na maandamano lakini nikikumbuka jinsi viongozi wanavyogawana hela zetu nafikia mahali nabariki migomo na maandamano ya watu kudai maslahi yao…ref.escrow,epa,richmond,rada etc.
 
Migomo lazima iwepo kwa sababu wananchi hawakumbukwi tena.

Inatia hasira sana kama vijana wanashindwa kuingia darasani kwa sababu ya njaa wakati mafisadi wamerelax tu hata kashfa iwe kubwa vp lakini mwisho wake ni kimya tu tangu watu waanze kusikia kashfa za ufisadi hakuna hata mmoja aliechukuliwa hatua na bado mtanzania katulia mpk wanazitaka hata hizo hela za mboga za wanafunzi chuo kikuu!!
 
Inatia hasira sana kama vijana wanashindwa kuingia darasani kwa sababu ya njaa wakati mafisadi wamerelax tu hata kashfa iwe kubwa vp lakini mwisho wake ni kimya tu tangu watu waanze kusikia kashfa za ufisadi hakuna hata mmoja aliechukuliwa hatua na bado mtanzania katulia mpk wanazitaka hata hizo hela za mboga za wanafunzi chuo kikuu!!

aibu alafu wanachofanyia hatuoni wanaenda kula bata visiwani uko missipii na mauze yao .. new TANZANIA IS COMING..
 
Wala sijaona Kuwa hawana sababu ya kuandamana ninachoshangaa je hizo haki hawakuzijuwa miaka yote isipokuwa wakati huu tukielekea kwenye uchaguzi mkuu
Huoni Kuwa ni kusababisha matatizo kwa taifa letu waungwana tujipende wenyewe na kujihurumia kabla haijafikia kuja kuonewa huruma na mataifa mengine kama tunavyowaonea huruma wenzetu walio kwenye machafuko

Amani ni tamu na machafuko ni machungu.

Naona ka hujui ulichokileta ili kijadiliwe na kama hujui bora ukae kimya maana hiyo unayoiita miaka ya nyuma sina uhakika kama ulikuwepo
 
Back
Top Bottom