Bado hakomi kila mara anasombewa assets.

Bado hakomi kila mara anasombewa assets.

Nguva Jike

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2018
Posts
1,267
Reaction score
1,819
Habari za muda huu members.

Kuna jirani yangu hapa ninapoishi yeye ni mfanyakazi wa kampuni kubwa ya mabasi ya mikoani.

Kwa macho yangu jana ni mara ya tatu ndani ya miaka 2 ya ndoa mke anaenda kwao kukitokea maneno kidogo tu.

Mke anavizia jamaa akienda kazini huku nyuma anakodi guta anasomba vitu vyote vya ndani anasepa kwao.

Sasa najiuliza inakuwaje mtu anasomba vitu vyote vya ndani halafu unamfuata tena akifika mnaanza moja.

Namuonea mpaka huruma au kwasababu ana hela? Flat screen TV, freezer,makabati everything halafu unamfuata kwao.

Wazoefu nitoeni matongo tongo hapa.
 
Pambana na maisha yako.

Kwamba unataka sisi tufanyeje:
  • tumuonee huruma jamaa?
  • tukutoe wasiwasi kuwa hiyo ni kawaida kwenye maisha ya ndoa?
  • tumsifu jamaa kuwa mvumilivu kwenye ndoa?
  • Tumkandie mwanamke kuwa mcharuko?

Wewe una undugu nao?
 
Bila shaka huyo jamaa ni mwanachama wa kilauri😁
FB_IMG_17467920244536294.jpg
 
Huyo mwanamke ni kibaka na msaka mali kama wezi wengine.Anaondoka halafu jamaa anamfuata?Huyo jamaa kama si chizi basi kapigwa uzezeta.Furusha kibaka huyo!
 
Pambana na maisha yako.

Kwamba unataka sisi tufanyeje:
  • tumuonee huruma jamaa?
  • tukutoe wasiwasi kuwa hiyo ni kawaida kwenye maisha ya ndoa?
  • tumsifu jamaa kuwa mvumilivu kwenye ndoa?
  • Tumkandie mwanamke kuwa mcharuko?

Wewe una undugu nao?
Halafu kila mmoja na destiny yake hapa duniani, kufuatilia destiny za watu nikupoteza muda na kuendeleza umbea bilasababu. Kwenye nguvu za asili anayemtangaza jamaa hapa anasubiriwa na ya kwake. Tujifunze kutosema sema ya wengine hapa ulimwenguni, tutaishi kwa raha sana.
 
Ukifatilia matatizo ya wapendanao au ugomvi wao utaumbuka wewe hujui Nini tatizo
 
Pengine umekuja kutafuta faraja humu, achana nae huyo mke wako na ikijirudia usije tena kutuletea stori hizo .
 
Pambana na maisha yako.

Kwamba unataka sisi tufanyeje:
  • tumuonee huruma jamaa?
  • tukutoe wasiwasi kuwa hiyo ni kawaida kwenye maisha ya ndoa?
  • tumsifu jamaa kuwa mvumilivu kwenye ndoa?
  • Tumkandie mwanamke kuwa mcharuko?

Wewe una undugu nao?
Tuseme wanawake ni wa ajabu
 
Habari za muda huu members.

Kuna jirani yangu hapa ninapoishi yeye ni mfanyakazi wa kampuni kubwa ya mabasi ya mikoani.

Kwa macho yangu jana ni mara ya tatu ndani ya miaka 2 ya ndoa mke anaenda kwao kukitokea maneno kidogo tu.

Mke anavizia jamaa akienda kazini huku nyuma anakodi guta anasomba vitu vyote vya ndani anasepa kwao.

Sasa najiuliza inakuwaje mtu anasomba vitu vyote vya ndani halafu unamfuata tena akifika mnaanza moja.

Namuonea mpaka huruma au kwasababu ana hela? Flat screen TV, freezer,makabati everything halafu unamfuata kwao.

Wazoefu nitoeni matongo tongo hapa.
Ana Afya mbovu ya Akili!
 
Back
Top Bottom