father superior
Member
- Dec 13, 2015
- 21
- 2
Wasalaam wanajamii forum wote.
Leo ni mara yangu ya kwanza kuleta mada hapa na ninakiri kuwa nilikuwa msomaji tu wa kawaida.
Nina tatizo kubwa linalonisumbua kwa sasa. Mimi ni mwanamke. Nilikuwa na mpenzi tuliedumu nae mwaka mmoja na nusu, mimi nikimpenda kweli ila sijui kwa mwenzangu ingawa naye nilizoea kusikia akiniambia hivyo. Miezi miwili iliyopita tuligombana.
Chanzo ikiwa ni yeye. Akidai kuwa anahitaji kuwa huru tu ingawa hana msichana mwingine. Niliomba msamaha kwa yote niliyomfnyia mpaka kufikia huko lakini hakuridhia. Tukaachana ila tukiendelea kuwasiliana na kusaidiana kama zamani. Ukaribu bado ulikuwepo ila haukua ule wa kimapenzi.
Mwenzangu aliendelea kuwa na furaha na hata mara nyingine aliongea vitu ambavyo nilihisi alitaka nimwonee wivu. Hali hiyo ikanikera na tukagombana tena na kumtukana juu. Ukaribu wetu ukapungua kwa kiwango kikubwa na hata simu hatukupigiana kwa muda wa mwezi mmoja.
Kiukweli nilimmisi muda huo nikatamani tena niwe karibu nae. Jana usiku nimempigia simu na kumuomba samahani, cha ajabu ananiambia yeye hana shida kabisa na mimi na bado anapenda kuwa karibu yangu. Usiku mzima ananitumia message kunitania hili na lile ingawa si za kimapenzi.
Hivi huyu mtu bado ananipenda kweli?
Msaada tafadhali.
Leo ni mara yangu ya kwanza kuleta mada hapa na ninakiri kuwa nilikuwa msomaji tu wa kawaida.
Nina tatizo kubwa linalonisumbua kwa sasa. Mimi ni mwanamke. Nilikuwa na mpenzi tuliedumu nae mwaka mmoja na nusu, mimi nikimpenda kweli ila sijui kwa mwenzangu ingawa naye nilizoea kusikia akiniambia hivyo. Miezi miwili iliyopita tuligombana.
Chanzo ikiwa ni yeye. Akidai kuwa anahitaji kuwa huru tu ingawa hana msichana mwingine. Niliomba msamaha kwa yote niliyomfnyia mpaka kufikia huko lakini hakuridhia. Tukaachana ila tukiendelea kuwasiliana na kusaidiana kama zamani. Ukaribu bado ulikuwepo ila haukua ule wa kimapenzi.
Mwenzangu aliendelea kuwa na furaha na hata mara nyingine aliongea vitu ambavyo nilihisi alitaka nimwonee wivu. Hali hiyo ikanikera na tukagombana tena na kumtukana juu. Ukaribu wetu ukapungua kwa kiwango kikubwa na hata simu hatukupigiana kwa muda wa mwezi mmoja.
Kiukweli nilimmisi muda huo nikatamani tena niwe karibu nae. Jana usiku nimempigia simu na kumuomba samahani, cha ajabu ananiambia yeye hana shida kabisa na mimi na bado anapenda kuwa karibu yangu. Usiku mzima ananitumia message kunitania hili na lile ingawa si za kimapenzi.
Hivi huyu mtu bado ananipenda kweli?
Msaada tafadhali.