Badilisha Nyumba Yako kwa Kusave Space na Furniture Zetu – Imetengenezwa Kwa Ajili Yako

Badilisha Nyumba Yako kwa Kusave Space na Furniture Zetu – Imetengenezwa Kwa Ajili Yako

TRABSOH

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
376
Reaction score
587
Unasumbuka na nafasi ndogo nyumbani? Umekuwa ukitamani fanicha ambazo hazichukui nafasi kubwa lakini bado zinapendeza na kudumu?
Afro Eco Wood Designs imekuletea suluhisho: fanicha za kisasa zenye ubunifu wa hali ya juu zinazokufaa wewe unayeishi kwenye nyumba yenye nafasi ndogo – iwe ni chumba kimoja (self-contained), studio apartment au nyumba ndogo ya familia.
Tunatengeneza:
  • Meza zinazokunjwa (foldable)
  • Vitanda vya chini vyenye droo za kuhifadhia vitu
  • Makabati madogo yenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi
  • Racks na shelves zinazopandikizwa ukutani
  • Viti vinavyoweza kutumika kama sehemu ya kuhifadhi (multi-functional)
Kila bidhaa hutengenezwa kwa mikono ya wataalamu wa fanicha na teknolojia ya kisasa, kwa kutumia mbao na vifaa rafiki kwa mazingira – tukijali nyumba yako na mustakabali wa dunia pia.
Unahitaji fanicha ya aina gani? Tunabuni kulingana na mahitaji yako binafsi!
Wasiliana nasi sasa upate ushauri BURE kabla ya kufanya mabadiliko nyumbani.
Afro Eco Wood Designs – Tunabadili Maisha kwa Ubunifu.

58c50cbb-0ce2-4432-a4f8-9306c57610a8.png
f355d981-0204-47c7-a626-83c959c7e914.png

Mawqsiliano : 0753322920
Morogoro Tanzania
 
Unasumbuka na nafasi ndogo nyumbani? Umekuwa ukitamani fanicha ambazo hazichukui nafasi kubwa lakini bado zinapendeza na kudumu?
Afro Eco Wood Designs imekuletea suluhisho: fanicha za kisasa zenye ubunifu wa hali ya juu zinazokufaa wewe unayeishi kwenye nyumba yenye nafasi ndogo – iwe ni chumba kimoja (self-contained), studio apartment au nyumba ndogo ya familia.
Tunatengeneza:
  • Meza zinazokunjwa (foldable)
  • Vitanda vya chini vyenye droo za kuhifadhia vitu
  • Makabati madogo yenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi
  • Racks na shelves zinazopandikizwa ukutani
  • Viti vinavyoweza kutumika kama sehemu ya kuhifadhi (multi-functional)
Kila bidhaa hutengenezwa kwa mikono ya wataalamu wa fanicha na teknolojia ya kisasa, kwa kutumia mbao na vifaa rafiki kwa mazingira – tukijali nyumba yako na mustakabali wa dunia pia.
Unahitaji fanicha ya aina gani? Tunabuni kulingana na mahitaji yako binafsi!
Wasiliana nasi sasa upate ushauri BURE kabla ya kufanya mabadiliko nyumbani.
Afro Eco Wood Designs – Tunabadili Maisha kwa Ubunifu.

View attachment 3343442View attachment 3343444
Mawqsiliano : 0753322920
Morogoro Tanzania
Sijaona sofa kitanda
 
shukrani kwa taarifa,
weka picha za tanzania tuone,
.hiZo picha hapo juu ni za mbefele😳
Kaka hiii ni computer hii ni design tu ukitaka inaweza kukufikia kama kilivyo mimi sio fundi wa mtaani mimi ni mtaalamu kabisaa wa furniture design and manufacturing , kama una lolote uliza
 
Achana na hizo Picha za kudownload kwenye mtandao,weka kazi zako halisi mkuu
 
Kaka hiii ni computer hii ni design tu ukitaka inaweza kukufikia kama kilivyo mimi sio fundi wa mtaani mimi ni mtaalamu kabisaa wa furniture design and manufacturing , kama una lolote uliza
swali lilitaka uweke picha ya kilichotengezwa tayari,
 
swali lilitaka uweke picha ya kilichotengezwa tayari,
Sawa nmekuelewa ndugu ila tunatofautiana hapa , siwezi kutengeneza nikakiweka hapo na kikaaa kikakosa mteja na mimi nishaingia gharama, kwahiyo naanda Michoro na 3d design natangaza ukipenda na tukakubaliana bei kinatengenezwa unakuja kukiona usiporidhika nacho au kikiwa tofauti na matarajio yako unakiacha hamna shida
 
weka picha sasa, la sivyo utaonekana Winga jonas lunyamila
Naelewa unachomaanisha kaka, ila kama umesoma tangazo langu ni tunabuni kulingana na mteja anavotamani na sehemu yake ilivyo hiii sio biashara ya furniture tu ni zaidi ya hapo ni huduma tofauti na ilivyozoeleka. Na ndo biashara naanza uzi huu utakua endelevu kila project itakayokamilisha nitaweka ushahidi hapa
 
Na bei ya bidhaa nakupa hesabu ya material na kila kitu na bei ya utengenezaji wewe utaangalia uhalisia kama kuna chambe za uwinga
 
Kaka kwa sasa vitanda vya sofa hatu deal navyo ndomana sijaweka hapo.
Nilimaanisha kitanda cum sofa.
yaani sofa ambalo unaweza kulikunjua likwa kitanda.
 
Kaka hiii ni computer hii ni design tu ukitaka inaweza kukufikia kama kilivyo mimi sio fundi wa mtaani mimi ni mtaalamu kabisaa wa furniture design and manufacturing , kama una lolote uliza
Ni vizuri ukaweka sample ya vitu ulivyotengeneza. Hata kwenye mtandao kuna ramani na design za nyumba ambazo ni nzuri sana lakini ukimwambia fundi ajenge itoke hivyo anashindwa. Bla hata wewe unajua huna huo uwezo ndiyo maana unaweka za computer.
 
hizo picha hapo juu teknolojia yake ni kiwandani kabisa, mbongo hawezi toa hivyo, labda nusu yake au robo,, hizo picha zimenyoka sana, mafundi wetu bado sana kufikia hapo,, waliopo mvutane vutane hadi kikamilike jasho likutoke,, mbao wakiweka siku mbili unawasikia wadudu wanatafuna,,
 
hizo picha hapo juu teknolojia yake ni kiwandani kabisa, mbongo hawezi toa hivyo, labda nusu yake au robo,, hizo picha zimenyoka sana, mafundi wetu bado sana kufikia hapo,, waliopo mvutane vutane hadi kikamilike jasho likutoke,, mbao wakiweka siku mbili unawasikia wadudu wanatafuna,,
Sawa kaka nmekuelewa sana na Asante kwa mrejesho wako ninaweza kupata namba yako na nikianza projects zangu uje kuona na kuwa shahidi na mteja wangu wa kwanza?
 
Ni vizuri ukaweka sample ya vitu ulivyotengeneza. Hata kwenye mtandao kuna ramani na design za nyumba ambazo ni nzuri sana lakini ukimwambia fundi ajenge itoke hivyo anashindwa. Bla hata wewe unajua huna huo uwezo ndiyo maana unaweka za computer.
Asante kwa mawazo yako na nmpokea mawazo haya, nikiweza kukupa kitu kama kilivyo kwenye picha hizo unaweza kuwa mteja wangu ?
 
Back
Top Bottom