Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,277
- 105,475
Kuna mambo mawili makubwa ambayo yamejadiliwa sana hapa.Moja ni placebo effect na pili ni psychological cure.
Katika matibabu ya Babu hakuna rituals zinazofanyika ila ni kunywa maji yaliyotokana na mmea.
Kama tunavyofahamu dawa nyingi zimetokana na mimea,cinchona kwa quinine na hata artemisia annua kwa dawa hizi mpya za malaria.
Kwakuwa kuna mti unaochemshwa suala la placebo halipo.Kuhusu suala la psychological effect linaweza likawa na mshiko kwa watu wazima zaidi lakini vipi kwa watoto ambao wameonekana kupata nafuu??
Binafsi naamini inaweza ikawa na efficacy fulani ingawa ni mapema ila napingana kuwa inatibu magonjwa mengi.Kwa nilowahoji watu wa pressure na sukari wanapata nafuu ila pumu hakuna nafuu.
Tatizo babu anaintroduce some supernatural elements katika dawa yake. Mimi sina tatizo na herbalism, nishasema hapo juu, kwani herbalism ina a scientific base, unakunywa maji ya mmea, mmea una kemikali zina react na mwili wako, zinaua vidudu, unapona. Hili sina tatizo nalo.
Tatizo la babu anataka ku present tiba na uponyaji wake kama muujiza wa mungu, watu hatuamini hata kama mungu yupo na ukishaanza kuongea habari za mungu na imani tunaona hata watakaopona watapona kwa placebo effect tu, na huwezi kuponya chronic diseases apart from the statistical fluke ya kupata afadhali na badala ya kufa miezi mitatu mtu anakaa mzima miaka mitatu.