Babu na serikali

Babu na serikali

Najijua

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
1,040
Reaction score
182
Najiuliza serikali ina ajenda gani na babu wa Loliondo, ifike wakati apewe Ulinzi na kutumia magari ya serikali?
Wataalamu wangapi na wakuu wa idara nyeti za nchi hii hawapewi hudma na unyeti anaopewa babu?

Au serikali imeoteshwa kumlinda na kumbeba? Nasema haya kwa kuwa jana amepelekwa Babati kuhudhuria msiba wa mtoto wake kwa gari la Halmashauri akiwa chini ya Ulinzi wa wana usalama na polisi kuelekea Babati.
 
najiuliza serikali ina ajenda gani na babu wa Loliondo ifike wakati apewe Ulinzi na kutumia magari ya serikali? Wataalamu wangapi na wakuu wa idara nyeti za nchi hii hawapewi hudma na unyeti anaopewa babu?au serikali imeoteshwa kumlinda na kumbeba?Nasema haya kwa kuwa jana amepelekwa Babati kuhudhuria msiba wa mtoto wake kwa gari la Halmashauri akiwa chini ya Ulinzi wa wana usalama na polisi kuelekea Babati

Sio vibaya pia kujua ni fedha kiasi gani, Halmashauri inavuna kutokana na Babu kufanya huduma ndani ya wilaya hiyo.
 
Mzee, suala la Babu lazima uliangalie kutoka pande mbalimbali. Kwa wengine babu ni mganga-mponyaji, kwa wengine babu ni chanzo cha mapato/ uchumi. Nadhani uhusiano wa babu na serikali uko zaidi kwenye uchumi. Halmashauri na wenyeji / wafanya biashara wa maeneo hayo wanajipatia mapato ya kodi kwa njia ya babu. Huyu ni wa muhimu sana. Lazima alindwe kwani ni investment kubwa. Ni chanzo cha ajira na mapato.
 
Babu ni zaidi ya hao ulio wataja kazi yake inaonekana na imeigusa serikali
 
Wangapi wana investements za kuingizia nchi mapatao makubwa kama TCC na TBL mbona hawapewi ulinzi?wangapi wanafanya uponyaji na utabibu na hawathaminiki?wako wapi Tz Heart Institute na Dr. Masau, serikali inapeleka wagonjwa wa moyo nje bado?au ni sera ya serikali na babu kwa sekta ya Afya?
 
amini usiamini babu ni tofauti inabidi apewe ulinzi madhubuti hawajakosea.
 
Bruker peleka hoja yako PCCB kuwa serikali inatumia vibaya rasilimali fedha ambazo ni kodi ya watz then jibu lake litakuwa hivi kila raia ana haki ya kulindwa na kuhakikishiwa usalama na serikali hasa pale inapoitajika kwa lazima kama hutak kuamin kasome katiba. kama umechukia babu kupewa ulinzi nenda kwa sheikh yahya amroge.
 
Bruker peleka hoja yako PCCB kuwa serikali inatumia vibaya rasilimali fedha ambazo ni kodi ya watz then jibu lake litakuwa hivi kila raia ana haki ya kulindwa na kuhakikishiwa usalama na serikali hasa pale inapoitajika kwa lazima kama hutak kuamin kasome katiba. kama umechukia babu kupewa ulinzi nenda kwa sheikh yahya amroge.
shk yahya hamuwezi Ambilikile kwa uchawi! Unajua babu ndie mkuu wa wachawi EA. Babu anajini mkubwa sana huwa anamjia usingizini, mwenyewe anamwita Mungu.unaona hata serikali kairoga! Inafanya anavyo taka. Sijawahi kuona serikali inayo support ushirikina duniani, kama chazo mapato mbona kina nengi na bakharesa hawajapewa ulinzi.
 
jamani huyu babu ananivutia ile mbaya. Lazima nifanye mchakato niwe mamsap wake maana sijamsikia bibi tangu nianze kumsikia babu
 
Najiuliza serikali ina ajenda gani na babu wa Loliondo, ifike wakati apewe Ulinzi na kutumia magari ya serikali?
Wataalamu wangapi na wakuu wa idara nyeti za nchi hii hawapewi hudma na unyeti anaopewa babu?

Au serikali imeoteshwa kumlinda na kumbeba? Nasema haya kwa kuwa jana amepelekwa Babati kuhudhuria msiba wa mtoto wake kwa gari la Halmashauri akiwa chini ya Ulinzi wa wana usalama na polisi kuelekea Babati.


Biashara kubwa inafanywa na vigogo huko Loliondo hasa ya usafiri. Uwanja wa ndege wa Arusha daima una chopper za faster za kwenda Loliondo. Unazani ni wamachinga wenye hizo chopper? Lazima wamlinde. Viongozi wenye Landcruzer nao zote wameziamishia kwenye trip za Loliondo!
 
Back
Top Bottom