Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Chanzo cha mauaji hayo inadaiwa ni mzozo ulitokea baada ya Regina kumfuata James lindoni kudai fedha za matumizi ya mtoto.
Akizungumza tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Longinus Tibishubwamu alisema lilitokea mjini Babati jana saa 12. 30 jioni.
Alisema askari huyo alikuwa lindoni katika Benki ya NMB tawi la Babati, Mtaa wa Usalama Kata ya Bagara.
Kaimu Kamanda Tibishubwamu alisema marehemu Regina alikuwa mkazi wa Mtaa wa Ngarenaro mjini Babati.
Alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa kabla ya kifo cha mwanamke huyo kulitokea mzozo kati ya wawili hao kuhusu fedha za matumizi ya mtoto.
"Wakati wakiendelea na mzozo ndipo askari kwa kutumia silaha aliyokuwa nayo alimpiga Regina risasi nne kwenye paji la uso, kifuani na shingoni", alisema
Baada ya tukio hilo, alisema mtuhumiwa aliitelekeza silaha lindoni na kwenda kujisalimisha polisi na askari waliokwemda eneo la tukio ndiyo walioichukua huku pia wakiokota maganda matatu ya risasi.
Kaimu Kamanda Tibishubwamu alisema mtuhumiwa yuko mahabusu kwa mahojiano kabla ya hatua nyingine kuchukuliwa na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali mjini wa Babati Mrara.