Baba yangu hataki nioe kabila tofauti na langu

Tatigha

JF-Expert Member
Jan 26, 2017
1,957
2,024
Wanajamii habari
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni miezi michache imepita toka ni hitimu shahada yangu na sasa hivi nafanya biashara zangu,
Kama mnavyojua umri unapokuruhusu kufanya jambo fulani basi sharti ufanye jambo hilo kwa wakati sahihi. Kwa sasa mimi natarajia kuoa ili niwe na msaidizi tujenge familia, na wakati niko chuo mwaka wa kwanza nilibahatika kukutana na msichana mmoja ambaye tulianza uhusiano, kiukweli uhusiano wetu toka tuanze umekua wa mafanikio sana sababu mchumba wangu huyo ndio amechangia kwa kiasi kikubwa mpaka mimi leo hii kumiliki biashara zangu binafsi.
Kwani alikua akinishauri mambo kadha wa kadha ambayo kiukweli yalizaa matunda na sisi kufikia hatua hii tuliyofikia, haya ni baadhi aliyoyafanya mchumba angu kipindi cha nyuma
1.mimi nikiwa first year yeye second year alinishauri na kunipa wazo la kufungua duka la nafaka, huku yeye akitoa nusu mtaji na mimi nikatoa nusu mtaji, tukafanya biashara na sasa iko mbali sana
2.kuna siku alitonya na kuniambia kwao Kuna banda liko wazi halina kazi kwa hiyo tunaweza kufuga kuku wa nyama na yeye atakua anasimamia kila kitu, kwa sababu namuamini nikafanya hivyo na kiukweli amesimamia shoo vizuri Sana mpaka nafurahi.

TATIZO LIKAANZA KUJITOKEZA
Sasa nije kwenye point iliyonifanya niombe ushauri, sasa kuna siku nimekaa na baba yangu nikamueleza juu ya mimi kuoa na mtu ambaye natarajia kumuoa. Kiukweli nilishangaa kuona mzee akinibadilikia akidai ni lazima nioe mkurya mwenzangu ndio yeye ataweza kushiriki katika hiyo harusi bila hivyo nisimjue, mchumba wangu ni mhaya kachanganya na mchaga.
Nilipo muuliza sababu ni nini mpaka nishindwe kuoa mtu wa kabila tofauti na langu, alichonijibu ni kwamba eti anataka akamilishe mila tu na si vinginevyo, yaani yuko radhi mimi nioe mtu ambaye sio sahihi ilimradi tu akamilishe mila, hivi hii ni sawa kweli??
Na mimi ni mtoto wa kwanza katika familia kwa hiyo nimeambiwa mimi ndio mfano kwa wadogo zangu sasa inabidi nioe mkurya mwenzangu, alafu kama nikitaka kumwoa huyo mchumba wangu ninaye mtaka basi nimwoe mke wa pili, na mimi siko tayari kuoa wake wawili.
Na akaniambia nisipo fanya hivyo nitapata shida sana endapo nitalazimisha kufanya navyotaka mimi.
Sasa ningependa kufahamu kwa wale vijana wenzangu wa kikurya ambao wameoa kabila tofauti alafu ni watoto wa kwanza katika familia walipata shida gani?

Hatua nilizochukua baada ya sakata hilo
1.nimeamua niishi na mchumba wangu hivyo hivyo, sihitaji harusi wala cha kwenda kuvalishana Pete kanisani, maana ndoa nimaridhiano baina ya Watu wawili, na sisi tumeridhiana na harusi sio chochote
2.mzee wangu amesema hanitambui mimi sio mwanae, kwa sababu nina kwangu na nina biashara zangu na kuna ndugu wengi tu wako upande wangu wala sioni shida, ila natafuta suluhu taratibu na nina imani muda ukifika atanielewa

Ushauri wenu
Je ni kipi ambacho nakosea hapo ili nijirekebishe? Vipi naweza kupata kweli tatizo kutokana na hii hali? Na ukizingatia binti wa watu nimetoka nae mbali na tumepanga mambo mengi sana, je ni sahihi kweli tuje tutengane eti kisa kutimiza mila?
Nitashukuru San kwa ushauri wenu wana jamvi
 
Muulize mshua yeye aliyeoa mke wa kabila lake ambaye ni mama yako amepata nini kwenye hizo mila ?
Halafu mwambie warioba alioa mchaga akawa wazuri mkuu na jaji mkubwa.....
Mwambie mzee dunia imebadikika ndio maana anapanda gari badala ya kutembea kwa miguu kilomita 20 kwenda 20 kurudi.....mabadiliko nayo yamechangia na yeye kubarikiwa na kila kubadilika.
Pia napata wasiwasi na uwezo wako wewe bwana harudi unayeshindwa kutetea hoja zako kwa point mpaka baba yako aliyekuwa na kukupeleka shule utapata elimu unashindwaje kumwelwwesha mzee wako mwenyewe....tumia akili na busara ulizozipata chuoni kutatua issue ndogo kama hii.
 
Nendeni kanisani mubariki ndoa yenu sherehe siyo lazima. Muone Paroko/mchungaji/pastor wako mpate wazimamizi wa ndoa yenu, mtakuwa na baraka na maendeleo ya juu na ya kipekee kwani kuzini mnamchukiza Mungu. All the best and best of baraka
 
Muulize mshua yeye aliyeoa mke wa kabila lake ambaye ni mama yako amepata nini kwenye hizo mila ?
Halafu mwambie warioba alioa mchaga akawa wazuri mkuu na jaji mkubwa.....
Mwambie mzee dunia imebadikika ndio maana anapanda gari badala ya kutembea kwa miguu kilomita 20 kwenda 20 kurudi.....mabadiliko nayo yamechangia na yeye kubarikiwa na kila kubadilika.
Pia napata wasiwasi na uwezo wako wewe bwana harudi unayeshindwa kutetea hoja zako kwa point mpaka baba yako aliyekuwa na kukupeleka shule utapata elimu unashindwaje kumwelwwesha mzee wako mwenyewe....tumia akili na busara ulizozipata chuoni kutatua issue ndogo kama hii.

Hebu oeni kwenu bwana...mnadhani dada zenu nani aoe?Acheni kukimbia majukumu,jukumu moja lako kama mtoto wa kiume ni kusaidia kuoa kwenu...acheni ufala
 
Muulize mshua yeye aliyeoa mke wa kabila lake ambaye ni mama yako amepata nini kwenye hizo mila ?
Halafu mwambie warioba alioa mchaga akawa wazuri mkuu na jaji mkubwa.....
Mwambie mzee dunia imebadikika ndio maana anapanda gari badala ya kutembea kwa miguu kilomita 20 kwenda 20 kurudi.....mabadiliko nayo yamechangia na yeye kubarikiwa na kila kubadilika.
Pia napata wasiwasi na uwezo wako wewe bwana harudi unayeshindwa kutetea hoja zako kwa point mpaka baba yako aliyekuwa na kukupeleka shule utapata elimu unashindwaje kumwelwwesha mzee wako mwenyewe....tumia akili na busara ulizozipata chuoni kutatua issue ndogo kama hii.
Mshua ni mgumu kuelewa sana na hataki kuzungumza na mimi akiwa mzima, ni mpaka alewe ndio anakua tayari kuzungumza na mimi, hivi unafikiri unaweza kumuelewesha mlevi akuelewe, mbona ndugu wengine ambao hawatumii kilevi wamenielewa ila tatizo ni yeye tu
 
Nendeni kanisani mubariki ndoa yenu sherehe siyo lazima. Muone Paroko/mchungaji/pastor wako mpate wazimamizi wa ndoa yenu, mtakuwa na baraka na maendeleo ya juu na ya kipekee kwani kuzini mnamchukiza Mungu. All the best and best of baraka
Kanisani itabidi tufanye hivyo mkuu ushauri wako nimeuchukua
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mshua ni mgumu kuelewa sana na hataki kuzungumza na mimi akiwa mzima, ni mpaka alewe ndio anakua tayari kuzungumza na mimi, hivi unafikiri unaweza kumuelewesha mlevi akuelewe, mbona ndugu wengine ambao hawatumii kilevi wamenielewa ila tatizo ni yeye tu
Hapo patamu na rahisi sana....pitia kwa washkaji zake wanaokunywa naye wampange kiaina na ikiwezekana tafuta siku umpeleke mchumba home hata asipofikia home afikie kwa shangazi ila make sure many anakutana naye na wife a display kiwango cha juu cha heshima lazma mshua atoe kibali
 
Sio vizuri kufanya harusi alafu baba yako asihudhurie, ni bora nisifanye tu
Sasa kama unaona ni bora usifanye mbona umeleta huu uzi apa? Cha kufanya wewe kama mmependana na uyo binti, na baba ataki umuoe kisa mambo ya kimila, jiulize. Unaamini kwenye izo mila au unaona hazina tija? Kama hauamini go and marry that girl. Mimi nimeshasema mambo ya kimila hayana nafasi kwangu, unaweza kujikuta una miungu mingi kweli kweli. Jiulize, unamwamini Mungu yupi? Wa mila au wa imani ya kidini uliyo nayo? Fanya maamuzi magumu
 
Sio vizuri kwenda kinyume na matakwa ya wazazi, lakini wazazi wengine wanachofanya siyo kabisa. Sa ukioa mwanamke wa kabila lako faida yake nini??? Watoto wenyewe sisi wa .com hata lugha na mila zetu hatuzijui... Kuumizana kichwa tu kwa kweli.
Mkuu, mi nadhani mkafunge tu ndoa kwa mwenyekiti mpate cheti na anzeni maisha yenu. Huna ata haja ya kuwaambia watu, tafuta shahidi wenu tu na mkaoane. Mzee akibadilisha mawazo huko mbele ndo muibariki ndoa yenu na kuafanya kasherehe.
 
Hapo patamu na rahisi sana....pitia kwa washkaji zake wanaokunywa naye wampange kiaina na ikiwezekana tafuta siku umpeleke mchumba home hata asipofikia home afikie kwa shangazi ila make sure many anakutana naye na wife a display kiwango cha juu cha heshima lazma mshua atoe kibali
Wanao kunywa nayo wote wana mawazo sawa, na wote ni kabila moja kwa hiyo nikifanya hivyo nitakua naruka mkojo na kukanyaga mavi
 
Sasa kama unaona ni bora usifanye mbona umeleta huu uzi apa? Cha kufanya wewe kama mmependana na uyo binti, na baba ataki umuoe kisa mambo ya kimila, jiulize. Unaamini kwenye izo mila au unaona hazina tija? Kama hauamini go and marry that girl. Mimi nimeshasema mambo ya kimila hayana nafasi kwangu, unaweza kujikuta una miungu mingi kweli kweli. Jiulize, unamwamini Mungu yupi? Wa mila au wa imani ya kidini uliyo nayo? Fanya maamuzi magumu
Hizo mila mimi wala sijui chochote, zaidi ya kuona zinapoteza wakati tu, Kuna mila ni nzuri na tunapaswa kuzifuata lakini Kuna zingine zinahitaji marekebisho ya kimila
 
Back
Top Bottom