EricMan
JF-Expert Member
- Oct 5, 2017
- 1,725
- 2,924
Baba mzazi wa Mtanzania aliyeuawa huko Israel, Joshua Mollel yuko nchini humo kwa mwaliko wa Wizara Mambo ya Nje ya nchi hiyo ambapo akiwa huko alishiriki hafla ya kutoa heshima kwa Watanzania wawili waliouawa kwenye mapigano kati ya Israel na Hamas huko Gaza.
Desemba 14, 2023, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, January Makamba alieleza kwamba walipokea taarifa kutoka Serikali ya Israel ikiwajulisha kwamba Joshua aliuawa na Hamas tangu Oktoba 7, 2023.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumatano Desemba27, 2023, Naibu Balozi wa Israel katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda, Dvora Dorsman Yarkoni amesema Loitu Mollel ambaye ni baba mzazi wa Joshua Mollel yuko Israel alikokwenda kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo.
Amesema katika ziara yake, Mollel ameshiriki hafla kutoa heshima kwa Watanzania wawili waliouawa na kikundi cha Hamas huko Gaza (Clemence Mtenga na Joshua Mollel), hafla iliyoongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Eli Cohen.
(Imeandikwa na Peter Elias na Sute Kamwelwe)
mwananchiupdates
Desemba 14, 2023, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, January Makamba alieleza kwamba walipokea taarifa kutoka Serikali ya Israel ikiwajulisha kwamba Joshua aliuawa na Hamas tangu Oktoba 7, 2023.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumatano Desemba27, 2023, Naibu Balozi wa Israel katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda, Dvora Dorsman Yarkoni amesema Loitu Mollel ambaye ni baba mzazi wa Joshua Mollel yuko Israel alikokwenda kwa mwaliko wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo.
Amesema katika ziara yake, Mollel ameshiriki hafla kutoa heshima kwa Watanzania wawili waliouawa na kikundi cha Hamas huko Gaza (Clemence Mtenga na Joshua Mollel), hafla iliyoongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Eli Cohen.
(Imeandikwa na Peter Elias na Sute Kamwelwe)
mwananchiupdates