Wakuu
picha hizi za mnato zinaonesha Shule ya Msingi Ikwazu iliyoko Kijiji cha Ikwazu kata anayotokea bwana mkubwa.
View attachment 148439
Hichi kibanda kinachoonekana miti tu hapa chini ambacho unaweza kukiita jengo ukipenda, kilikuwa ni nyumba ya Mwalimu ambaye amelazimika kuhama baada ya jengo hilo kubakia hivyo lilivyo.
Kwa hali hii kuichagua ccm ni kujidhalilisha
View attachment 148443
Kahamia sehemu moja inaitwa Kimange ambapo kidogo ni centre lakini ili afike shuleni hapo anapaswa kusafiri mwendo wa takriban km 25 kwenye njia mbovu inayohusisha majaruba. Ujinga huu wa ccm ulinifanya niukatae na kukata tamaa ya kushika kalamu.
Ni katika njia hiyo msafara wa Chadema uliokuwa unakwenda Ikwazu kwenye kampeni za nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu na mkutano wa hadhara ulilazimika kuacha magari na kutembea kwa miguu ili kuweza kufika upande kijijini hapo. Ilikuwa ni baada ya kukwama kweli kweli kwenye zile njia/majaruba.
Picha zingine zinaonesha madarasa na majengo ya shule hiyo ambayo ina madarasa saba mwalimu mmoja.
Picha zingine zinaonesha mandhari ya kijiji chenyewe cha Ikwazu. Needlessly to say...one could witness the highest level of poverty.
Kwa mazingira haya ambayo yanawakilisha maeneo mengi nchini, CCM na Kikwete walipaswa kuwa positive na kukubaliana na wazo la Dokta Slaa juu ya sera ya kuboresha makazi kwa wananchi kwa kupunguza au kuondoa kodi kwenye bidhaa za ujenzi km nondo, mabati, saruji na mbao ili wananchi wamudu kujenga makazi bora.
Mtakumbuka wakati ule Dokta Slaa alisema kwa standard za kimataifa, makazi duni ni dalili za nchi kuwa na umaskini.
Wananchi katika maeneo hayo wamehoji inakuwaje Mwenyekiti wa CCM anaweza kupata ujasiri wa kutumia mamilioni kujenga jengo la kuchezea ngoma lakini ameshindwa kusaidia watoto kupata mazingira ya kupata elimu bora au wananchi kupata makazi bora.
Wanahoji CCM wanapata wapi ujasiri wa kuja kuomba kura tena kwa kumtanguliza mgombea asiyejua wananchi hao wanaishi na kuvumilia matatizo gani, maana maisha yao na yake ni mbingu na ardhi.
View attachment 148449
NAMNA CHADEMA ILIVYOSHAMBULIA KWA KIKWETE- MAENEO YOTE HAYO YAKO KWENYE KATA INAKOISHI FAMILIA YA RAIS KIKWETE
Hapa Kamanda Mathayo Torongey akimwaga sera za chama chake kwa wananchi wa Lugoba.
View attachment 148452 View attachment 148453
Hapo juu Kamanda Mathayo Torongey akisalimiana na maelfu ya wananchi wa Lugoba kwenye kampeni zilizofanyika Lugoba.
View attachment 148455
Mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mathayo Torongey akisalimiana na mmoja wa wakazi wa kijii cha Makombe juzi.
Mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mathayo Torongey, akiwahutubia wananhi wa kijiji cha Goba katika mkutano wa kamoeni juzi.
Mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mathayo Torongey, akisdalimiana na wananchi wa kijiji cha Lugoba, baada ya mkutano wa kampeni kijijini hapo juzi.
CHAGUA CHADEMA, CHAGUA UZALENDO