Baba Askofu Gwajima nina wasiwasi na wewe

Baba Askofu Gwajima nina wasiwasi na wewe

Kuwa masikini au tajiri ni tabia,na uchaguzi pia ukiwa na mawazo ya kimasikini lzm uwe masikini.
 
Watanzania tumezoea umaskini. Hata wewe ukifanya kazi na kutajirika,watasema umejiunga na freemason au unauza ngada.Haya mawazo ndiyo yaliyotudidimiza. Tubadili fikra! Nchi ikiwa na matajiri wengi haiyumbi kiuchumi . Gwajima Mungu kamzidishia acheni wivu.
 
Wasiwasi wangu unatokana na utajiri wako baba: Umenunua chopa, na sasa unataka kununua treni.

Baba hela ya kununua chopa na treni umeipata toka kwa waumini wako tu? Huuzi ngada?

Unataka kuniambia wewe ndiye mwenye waumini wengi sana kuliko Kadinali Pengo, Malasusa, Mwingira, Lwakatare, G. Davie, Mzee wa Upako, n.k?

Baba askofu, kweli sadaka ndiyo inakuwezesha kuwa unagharamia maafisa usalama wako, maafisa usalama wa Dr. Slaa kipindi kile mkiwa marafiki, kununua chopa na treni?

Serikali Ya Awamu Ya 5 Kwa Kujibana Sana, Ndo Imenunua Bomberdier 2. Mseveni Wa Uganda Nchi Yake Haina Ndege, Katumia Ndege Ya Kenya Kuja Tanzania Kufanya Ziara Ya Kiserikali. Sembuse Ww Gwajima??!!

Sadaka haitoshi baba askofu, na ndiyo maana hata jengo la kuabudia huna. Waamini wako wanapigwa jua, vumbi na mvua wakati wa ibada.

Baba nina wasi wasi na wewe kuwa huenda ni muuza ngada, ila hujagundulika tu.

Siku ukileta ushahidi wa vyeti vya D B uje pia na ushahidi kuwa sadaka yako inakupa kipato ulicho nacho.
Kwanini usiwe na wasi na Makonda?
 
Sasa ukijua utajiri wa Major 1 wa south afrika si ndo utachanyikiwa? Kuanzisha kanisa kunalipa balaa
 
Pengo hana kanisa
Gwajima anamiliki kanisa
Experience the difference mkuu
 
Aoneshe jinsi anavyolipa kodi ya serikali, asipepese macho kwa hilo.
 
Gwajima siyo mchungaji, bali anatumia Psychology of religious mobilisation with superstition clue techniques. It Includes use of:
1.Chuma ulete kupitia waumini hao hao tu.√
2.Ngada kwa wingiiii√
3.Freemanson club√
4.Umiliki wa chungu uvunguni chenye kutoa povu: ushirikina wa hali ya juu.√
wewe kama unajua hayo mbona bado uko masikini??
 
Eti baada ya Dr Gwajima kutiririka na Daudi Bashite ndipo D Bashite amekaa akijiuliza atoke vp dhid ya Gwajima eti huu ndio mtoko wake dhidi ya Baba Askofu.
 
Gwajima angekua na hayo makandokando husingemsikia baada ya kuachiwa, huyu ni mtu wa Mungu, anawanyoosha watawala. Ni nani mwenye ujasiri awe anauza madawa atoke aendelee kusema? Hauhitaji degree kupata jibu, pili wewe utakua bashite, weka vyeti hadharani mbona ni tendo la dk chache kuliko kuendelea kufukuzana na watu wa Mungu. Daudi Albert Bashite
 
Hivi Yale mambo ya kuiba dhambi,uzinzi dhambi bado yanahubiriwa? au issue ni jinsi ya kuwa Tajiri tu
 
Fanya simple mathematics!
Gwajima ana waumini wapatao 70,000 assume kila jpil kila mmoja anatoa sh1000/=
700,00*1000=70,000,000/= kwa jumapili moja!
Kwa mwezi 70,000,000*4=280,000,000/=
Kwa mwaka 280,000,000*12=3,360,000,000/=
Jamaa kwa mwaka anapata zaidi ya 3bn!
Bei ya helicopter kama ile yake ni around 2.8bn! Sasa yeye kaanza kuhubiri lini?
Kwa wastani wa makusanyo hayo atashindwa kununua treni...?
Kila muumini anatoa sh 500 ni wastani halisi zaidi.pia sio waumini wote wanahudhuria kila jumapili.labda kama anabiashara zingine za kuongezea kufikia hiyo 1000 uliyokadiria.
 
Back
Top Bottom