Baba alitafutiwa mke

Baba alitafutiwa mke

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
527
Reaction score
596
Baba yangu alimpenda sana mama, na alitoa ahadi ya kumuoa endapo angerudi kutoka masomoni kutoka ughaibuni.

Nilikua kichanga kidogo sana nyakati hizo ila nilihisi upendo wa baba, na hii ilijidhihirisha pia kwa ndugu zangu.

ndugu zake baba hawakumpenda mama, na hivyo kumchagulia baba mke mwingine wakati yeye bado yu masomoni, mama aliumia sana na alisononeka kweli.

Enzi hizo mzee hakuweza kuwabishia nduguze as Mama(bibi) yake alisimamamia hilo.

Miaka michache baadae baba aliaga dunia huku akiwa na ndoa ya mwanamke asiye chaguo lake.

Namshukuru sana baba yangu kwa kumpenda mama, ila namlaumu sana kwa kushindwa kujisimamia kwenye maamuzi.

RIP BABA.
 
RIP baba JJB ...

kijana itakuwaje wewe sasa mama yako akikuchagulia mke ambaye hakuwa chaguo lako?
 
Last edited by a moderator:
Miaka ya nyuma kuna sehemu ulikuwa huruhusiwi kuoa hata kama huyo mwanamke umempenda na ana heshima kiasi gani! Yawezekana mama yako alitoka sehemu ambayo dingi haruhusiwi kugusa wala kutaja hilo eneo. Na kipindi hicho mama akisema huwezi kubishana naye.
 
Mwanaume kiwa WEAK kweye decision WANAWAKE WATAKUENDESHA SANAAA! Si MAMA YAKO, MKEO, MAMA MKWE, DADA ZAKO, SHEMEJI ZAKO, HADI WAFAGIZI NA WAPIKA CHAI OISINI KWENU WATAKUKALIA KICHWANI.!!!!!!!!

Mwanaume unatakiwa uwe DECISIVE NA UNA MSIMAMO NA ITAKADI ZAKO, kiasi kwamba mwanmke yeyote unampeleka kwa itikadi zako.
 
Mwanaume lazima ujitambue kwa kuwa na misimamo na itikadi zako
Ukishaongea hakuna wa kuongea tena baada yako yanayofuta ni utekelezaj tu
 
Mimi nawasubiri tu waje waanze kuleta zegwe kwa laaziz wangu,potelea mbali bora na undugu wenyewe ufe
 
Weka picha

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Mwanaume kiwa WEAK kweye decision WANAWAKE WATAKUENDESHA SANAAA! Si MAMA YAKO, MKEO, MAMA MKWE, DADA ZAKO, SHEMEJI ZAKO, HADI WAFAGIZI NA WAPIKA CHAI OISINI KWENU WATAKUKALIA KICHWANI.!!!!!!!!

Mwanaume unatakiwa uwe DECISIVE NA UNA MSIMAMO NA ITAKADI ZAKO, kiasi kwamba mwanmke yeyote unampeleka kwa itikadi zako.

Well said mama!
 
Washukuru bibi na babu yako wasingemtafutia mke baba yako usingezaliwa.
 
^^
Wakati Baba anagundua Babu alikuwa sahihi, anae mtoto anaeamini Baba yake hakuwa sahihi, mpaka mtoto akiwa Baba ndio atafahamu uzito wa kuwa Baba, ndipo atajua Baba alikuwa sahihi
^^
 
Nadhani inategemea na malezi alio lelewa mwanamme,mimi kwa mfano mume wangu mwanzo aliponioa nilikua napata tabu sana ilikua nilitaka kwenda kuwaona wazee wangu ruksa lazima atoe babamkwe na ukimpigia simu anakwambia kuna ulazima gani kwenda yani kuna mgonjwa kuna harusi kuna nini? nilianza kumbadilisha mumewangu pole pole sasaivi ruksa kiatu changu nikisema leo naenda kumuona mama sawa naenda kwenu sawa,mkwe kasema kapewa ukweli katulia....
 
Nadhani inategemea na malezi alio lelewa mwanamme,mimi kwa mfano mume wangu mwanzo aliponioa nilikua napata tabu sana ilikua nilitaka kwenda kuwaona wazee wangu ruksa lazima atoe babamkwe na ukimpigia simu anakwambia kuna ulazima gani kwenda yani kuna mgonjwa kuna harusi kuna nini? nilianza kumbadilisha mumewangu pole pole sasaivi ruksa kiatu changu nikisema leo naenda kumuona mama sawa naenda kwenu sawa,mkwe kasema kapewa ukweli katulia....

power of love..
 
Back
Top Bottom