Baadhi ya Wanawake ni Binadamu wa pekee sana, nawapa Pongezi muishi miaka mingi ya Kobe

smarte_r

JF-Expert Member
Nov 8, 2013
4,538
11,868
Kabla sijaenda kwenye mada, niseme tu ukweli, mimi ni kati ya wale wanaume wahongaji.

Nikiombwa pesa na mtoto wa kike, kama ninayo, nampa bila kusita.kwanini?, fatilia andiko langu.

Wiki kadhaa zilizopita nilisafiri kikazi ktk wilaya X inayopatikana mkoa flani hapa tz. nilifikia ktk lodge moja maarufu eneo lile.

Nilikaa pale kwa siku nane ili kukamilisha jambo lililonipeleka. siku zangu nne za mwanzo mambo yalienda vizuri, ila kuanzia siku ya tano, akiba yangu ya pesa ikakata.katika account yangu ofisi waliniwekea allowance ya siku nne tu za kuanzia.

Pesa ilikata baada kutokea dharula nyumbani kwangu iliyofanya nitume pesa nyingi kusolve.

Nikapiga simu headquarter ya taasisi ninayofanyia kazi kuwataarifu kuwa nimeishiwa fedha, wanitumie pesa nyingine ya allowance ili niweze ku survive kwa siku nne zilizobaki.

Headquarter wakaniambia request yangu ipo kitengo cha finance, itachukua siku tatu kuwa approved. nikasema sio kesi, nitasubiri.

Pale lodge mdada wa reception akawa ananisumbua kuulizia malipo ya siku zilizoongezeka. nikampiga kiswahili kwa kumuomba avute subira, akanielewa.

Wakati nikiwa nasubiri watu wa headquarter wafanye mambo, nikajiongeza kwa kuwapigia simu washkaji zangu kadhaa waniazime pesa kidogo ili ikiingia ile itakayotumwa na headquarter,niwarudishie.

Nikampigia simu colleague wangu mmoja hivi, nikamuomba aniazime laki moja. akanieleza mlolongo wa majukumu kibao yaliyopo mbele yake. ikaisha hivyo.

Nikamcheki mwanangu mwingine yupo wizara fulani, nilishawahi kumuazima pesa na mpaka leo hajanirudishia. Akanihaidi atanitumia, nimcheki mida ya jioni. ilipofika jioni kila nikimpigia hapokei, simu nane zote zileenda bila kupokelewa. nikakata tamaa.

Nikaona isiwe tabu, nikamcheki classmate wangu niliyesomanae chuo, kwa sasa ni ofisa wa shirika fulani. huyu jamaa nilijitoa sana wakati anaoa. pesa niliyo spend kwenye harusi yake ni mara mbili ya ile niliyotoa kwenye mchango.

Nikamueleza shida yangu, nikamuomba aniazime laki moja na nusu tu. akaja na story kibao za malalamiko.mara sijui ada za watoto, sijui gari lake bovu lipo gereji, sijui pesa yote kachukua wife wake kawekeza kwenye duka la nguo na blabla kama zote.nikajua sasa hapa naumbuka huku ugenini.

Nikasema acha nihamie kwa watoto wa kike ambao ninadate nao na wale niliowahi kudate nao. Nina michepuko kadhaa, ila katika jambo hili nilichagua watano tu wa kuwapigia.

Katika hawa watano,wanne ni waajiriwa na mmoja ni housewife. huyu housewife kwa sasa ni mke wa mtu. nilikuwa nadate nae zamani kabla hajaolewa. kwa sasa amebaki kuwa rafiki yangu wa kawaida, siku mojamoja huwa tunapigiana simu kujuliana hali.mumewe ni boss katika shirika fulani.

Nikamcheki mchepuko wangu wa kwanza ambaye ni supervisor ktk hotel fulani ya kitalii huko mbugani. nikamueleza jambo langu na nikamuomba aniazime laki moja kwa ahadi ya kuirudisha ndani ya siku chache.

Ndani ya dakika moja baada ya kumaliza maongezi yetu, muamala wa laki moja ukasoma kwenye simu yangu ukitoka kwake. nikamtumia text ya kumshukuru.

Nikampigia simu mchepuko wangu wa pili mfanyakazi wa shirika fulani serikalini. pia ni mweka hazina wa kikundi cha kufa na kuzikana cha kazini kwake. fedha zote za kikundi anadhibiti yeye.

Baada ya kumueleza suala langu akanitumia laki moja na nusu, ila alisisitiza niirejeshe ndani siku chache kwasababu sio pesa yake, ameitoa kwenye kikundi. nikamwambia asijari, nitairejesha.

Baadae nikampigia simu X wangu housewife ambaye kwa sasa ni mke wa mtu. tulipiga story ndefu ikiwemo kuulizana maendeleo ya watoto.

Kwa sasa yeye na mimi ni watu wazima, yeye ana watoto kadhaa na mimi ninao pia, huwa tuna kawaida ya kuulizana issue za maendeleo ya watoto wetu kila tunapogiana simu.

Baadae nikachomekea suala langu, nikamwambia nipo wilaya fulani kikazi ila nimekwama kifedha, nahitaji laki mbili iweze kunisogeza kwa siku kadhaa nikisubiri pesa kutoka ofisini.

Akaingiwa na huruma , halafu akaniuliza "hiyo laki mbili itakutosha kweli?, nakutumia laki tatu". Akanisihi niirudishe mapema kwasababu anaitoa kwenye fungu alilokabidhiwa na mumuwe kuhusu ujenzi wa nyumba yao nyingine. Baada ya dakika tano, muamala wa text ya laki tatu ukaingia kwenye simu yangu.

Mpaka hapo nikawa nimepata laki tano na nusu niliyoazimwa na wanawake. Nikabakiwa na wawili katika wale watano niliopanga kuwapigia.

ila kwa kuwa tayari nilikuwa nimeshapata pesa ya kunisogeza, nikawapigia kuwasilimia tu. sikugusia jambo lolote la kutaka waniazime pesa.

Nilichojifunza ktk jambo hili ni kwamba sisi wanaume(baadhi yetu), ni wazito kusaidiana. tunakuwa na visingizio vingi sana tunapopigiwa simu na washkaji zetu kutuomba tuwaazime pesa wakati wa dharula.

Mbaya zaidi unakuta mtu anakuhaidi atakutumia ndani ya mda fulani, ukifika huo mda ukipiga hapokei na simu anazima.

Baadhi ya wanawake wapo vizuri sana katika jambo hili, ni wepesi kuokoa jahazi. wameumbwa na huruma, wanatuokoa sana tupatapo dharula zinazohitaji pesa ya haraka.

Hii ndio sababu inayonifanya niwe nawahonga baadhi yao kila wanaponiomba pesa. nachukulia ni kama naweka akiba ambayo kuna siku itakuja kunisaidia.

Wahongaji wenzangu nasema uongo ndg zangu?.

Karibuni.

NB: pesa niliyoazima kutoka kwa hao wanawake, niliirejesha kwa wakati kama nilivyohaidi.
 
Hapo umerudishiwa ulizohonga kama ulijinasibu hapo juu kuwa wewe ni muhongaji mzuri...

Ipo hivi mwanamke akupi ela yake kizembe kama haujawahi kumpa pesa za hapa na pale.

Anyway Tutafute pesa bado muda upo.
haina shida, ndio faida ya kuwahonga. ndio maana wakanipa nilipowaomba.
 
Kwakua umetuambia kua wewe ni mhongaji mzuri, kongole kwako.
Swali ninalojiuliza ni kwamba, hao wanaume wenzio hua nao wakikuomba msaada wa kifedha unawapa au unawakazia?
Maana usikute wewe ni msoft kwa watoto wa kike lakini kwa masela unakuja na sababu kibao.
 
Back
Top Bottom