Pole sana mkuu umefikwa kisawasawa. Ukiona mtu kafikiria mpaka kukumbuka kwao si mchezo. Hayo yamekufika kwa sababu ukweli ni kwamba darisalama si salama tena. Darisalama imekufa na sasa ni mashamba ya mpunga kama ulivyosema.
Darisalama imeuawa na uongozi wenu wa kuoneana haya katika kutimiza majukumu. Unamwona mtu anajenga mjengo kwenye barabara ya watu wengine, weye unakenua meno kucheka tu kwani amekupa kitu kidogo. Mtu anajenga ukuta kuzuia maji, halafu anamimina msingi mita 6 juu kabla ya kuanza ujenzi wa nyumba huku akijua kuwa mafuriko yatakuja tu, hivyo yasimsumbue, nyiye mmekaa kimyaa ati ana vihela vyake vya escrow.
Sintamsahau yule mama mh. mkubwa vile alifunga barabara kwa ajili watu wasione anachojenga, mwisho ile njia imejakufa kienyeji. Darisalama mhhhhh. RIP darisalama umekufa na uzuri wote ulee