Baada ya Yanga kutolewa,hiki ndo ninachokiamini...

Baada ya Yanga kutolewa,hiki ndo ninachokiamini...

Anselm

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2010
Posts
1,710
Reaction score
291
Yanga imetolewa kwa penalt na bingwa mtetezi Al-Ahly ya Misri katika mazingira ambayo wenyewe walikuwa na nafasi kubwa sana ya kuvuka,kwasababu zifuatazo:-
1. Binafsi ninaamini ki'viwango Yanga ilikuwa vizuri kuliko Al-Ahly, mechi zote 2 ya Dar-es-salaam na ya Misri zinathibitisha hilo.
2. Kisaikolojia walikuwa vizuri kuliko wapinzani wao kwani katika mechi 5 za mwisho kabla ya mechi ya leo Yanga walikuwa wameshinda zote ukilinganisha na wapinzani wao walioshinda 1,wakadroo 1 na kufungwa 3,kwahiyo spirit ya ushindi ilikuwa imewaweka vizuri zaidi Yanga kuliko Al-Ahly.
3.Katika msimu huu Yanga imekusanya wachezaji wote makini ambao team ya level yake ingehitaji kuwa nao,wachezaji ambao wangetosha kuiweka Club yao kwenye ramani ya soka la Africa just kwa kumtoa bingwa mtetezi tu.
4.Financially Yanga iko vizuri,wanapata kila kitu wanachohitaji kutoka kwa Viongozi wao ikiwemo mishahara kwa wakati,posho kwa matokeo mazuri na maandalizi yanayoeleweka,kambi ya Uturuki ni uthibitisho wa hili, ukilinganisha na wapinzani wao ambao inasemekana wamechoka kweli.
5.Walikuwa na akiba ya ushindi wa nyumbani wa goli 1-0
6.Kuwang'oa Waarabu wanaosadikika kuweka record fulani ya Dunia kungewafanya wachezaji wa Yanga kuwa gumzo hivyo kuwa kwenye nafasi ya kijiweka sokoni zaidi kuelekea kwenye soka la kimataifa.
Inasikitisha sana kuona team yenye kila kitu inashindwa kuvuka kikwazo cha team isiyo kwenye kiwango kama ya Al-Ahly hii ya sasa hivi,uzembe,uzembe,uzembe....
Kwanini uzembe:-
1. Kwajinsi Al-Ahly walivyocheza game ya Dsm,Yanga walikuwa na uwezo wa kupata ushindi wa zaidi ya goli moja...umakini zaidi na ufahamu wa kutambua umuhimu wa ushindi wenye afya unapocheza nyumbani ulikuwa unaweza kuwapatia Yanga ushindi wa si chini ya magoli ma'3 siku ile,magoli mawili tu yangetosha kuwang'oa waarabu.
2.Katika mechi ya muhimu kama ile...mpinzani wako anatangulia kukosa penalt mara 2,mara zote na wewe unakosa ku'equalize ni uzembe unaosikitisha sana.
3. Nk,nk
Ninapata mashaka, kwa kushindwa kuwang'oa Waarabu mwaka huu inaweza kupita miaka hata 50 kwa Yanga kuja kuwatoa Waarabu kwenye mashindano ya kimataifa.
Xssyyyyzzzzzuu!!!!!!!!
 
Yanga imetolewa kwa penalt na bingwa mtetezi Al-Ahly ya Misri katika mazingira ambayo wenyewe walikuwa na nafasi kubwa sana ya kuvuka,kwasababu zifuatazo:-
1. Binafsi ninaamini ki'viwango Yanga ilikuwa vizuri kuliko Al-Ahly, mechi zote 2 ya Dar-es-salaam na ya Misri zinathibitisha hilo.
2. Kisaikolojia walikuwa vizuri kuliko wapinzani wao kwani katika mechi 5 za mwisho kabla ya mechi ya leo Yanga walikuwa wameshinda zote ukilinganisha na wapinzani wao walioshinda 1,wakadroo 1 na kufungwa 3,kwahiyo spirit ya ushindi ilikuwa imewaweka vizuri zaidi Yanga kuliko Al-Ahly.
3.Katika msimu huu Yanga imekusanya wachezaji wote makini ambao team ya level yake ingehitaji kuwa nao,wachezaji ambao wangetosha kuiweka Club yao kwenye ramani ya soka la Africa just kwa kumtoa bingwa mtetezi tu.
4.Financially Yanga iko vizuri,wanapata kila kitu wanachohitaji kutoka kwa Viongozi wao ikiwemo mishahara kwa wakati,posho kwa matokeo mazuri na maandalizi yanayoeleweka,kambi ya Uturuki ni uthibitisho wa hili, ukilinganisha na wapinzani wao ambao inasemekana wamechoka kweli.
5.Walikuwa na akiba ya ushindi wa nyumbani wa goli 1-0
6.Kuwang'oa Waarabu wanaosadikika kuweka record fulani ya Dunia kungewafanya wachezaji wa Yanga kuwa gumzo hivyo kuwa kwenye nafasi ya kijiweka sokoni zaidi kuelekea kwenye soka la kimataifa.
Inasikitisha sana kuona team yenye kila kitu inashindwa kuvuka kikwazo cha team isiyo kwenye kiwango kama ya Al-Ahly hii ya sasa hivi,uzembe,uzembe,uzembe....
Kwanini uzembe:-
1. Kwajinsi Al-Ahly walivyocheza game ya Dsm,Yanga walikuwa na uwezo wa kupata ushindi wa zaidi ya goli moja...umakini zaidi na ufahamu wa kutambua umuhimu wa ushindi wenye afya unapocheza nyumbani ulikuwa unaweza kuwapatia Yanga ushindi wa si chini ya magoli ma'3 siku ile,magoli mawili tu yangetosha kuwang'oa waarabu.
2.Katika mechi ya muhimu kama ile...mpinzani wako anatangulia kukosa penalt mara 2,mara zote na wewe unakosa ku'equalize ni uzembe unaosikitisha sana.
3. Nk,nk
Ninapata mashaka, kwa kushindwa kuwang'oa Waarabu mwaka huu inaweza kupita miaka hata 50 kwa Yanga kuja kuwatoa Waarabu kwenye mashindano ya kimataifa.
Xssyyyyzzzzzuu!!!!!!!!

Bado inawezekana mkuu usichoke/usiogope bado watakuwa mabingwa na timu hii na kocha huyu mzungu na mkwasa wamebadilisha timu so tutafanya mambo tuu hata wachezaji wameumia but its part of the game
 
Umesema ukweli na umechambua vizuri mkuu, ingawa sote inatuuma lakini ikumbukwe kuwa wakati mwingine bahati inanafasi yake. Hata leo umemeona Mancity ikichapwa uwanja wa nyumbani na timu ya daraja la kwanza ambayo imezidiwa kila kitu na Mancity. Bado naona pia nje ya mpira pia tunahitaji watu pyschology ili kuwaweka sawa wachezaji wetu kujua umuhimu wa mechi kama hizi.
 
Wakiacha kale ka mchezo uliotuambia kwenye post yako baada ya mpira wataanza kushinda.
 
March 19 azam anawasubiri hapa. Kipre Tcheche kama namuona vile
 
Kwa kweli inasikitisha na inakatisha tamaa..., Al Ahly walikuwa weupe na wabovu kabisa!! Yanga wanakikosi kizuri na bora lakini mbinu na umakini ni zero... Kikosi hiki na mazingira kama haya wangekuwa Simba tungekuwa tunazungumza mengine sasa hivi...!!

Tatizo la YANGA ni uongozi kuendeshwa kwa porojo za kwenye magazeti badala ya kujiwekea mikakati ya ushindi uwanjani... Wamemsakama Bin Zubeiry na kuwatangazia wanaYanga wasusie blog yake, kisa amewaandika vibaya!!!? Upuuzi kama huu hutasikia hata siku moja kwa viongozi wa Simba!!
 
Inabidi tujaribu michezo mengine!Tanzania soka hatuliwezi huo ndio ukweli.Kama wachezaji ni wale wale,makosa yale yale,mashindano yale yale lakini hatujifunzi.
Sijui tuna laana au ni nini kwa sababu kila tukijaribu,hamna kitu!!!
Nina hasira natamani hata niibamize hii macbook yangu.
 
Maneno ya mkosaji ,mpira hauchezwi magazetini kajipangeni upya. REST IN HELL YANGA.
 
Rudini kwenu au unajiona na wewe mtz...time will come Kama Uganda na Idd Amini
 
Mi nahisi LABDA kuna maarifa nje ya uwanja yalifanyika either tulihongwa au sijui nini,Haiwezakani kutowashinda,Nina mashaka makubwa sana na ile mechi,Hivi kweli tulishindwa kumalizia zile penati,
Wachezaji wetu kweli hawana MORALI na ushindi,Kweli sisi ni vichwa vya wendawazimu.
Soka la kibongo sitaki tena,Nimeumia sana
Sorry ,it hurts
 
Sitaki kabisa kusikia! Unapaisha penalt muhimu kma ile wakati unajua unaandika historia ya kuwafunga waarabu? wanakosa nawe unaosa kuwasawazishia? No NO very boring!
 
Mi nahisi LABDA kuna maarifa nje ya uwanja yalifanyika either tulihongwa au sijui nini,Haiwezakani kutowashinda,Nina mashaka makubwa sana na ile mechi,Hivi kweli tulishindwa kumalizia zile penati,
Wachezaji wetu kweli hawana MORALI na ushindi,Kweli sisi ni vichwa vya wendawazimu.
Soka la kibongo sitaki tena,Nimeumia sana
Sorry ,it hurts

Nimekubali wabongo tunapenda mpira, ila mpira umetufanya tusiwe na furaha. Sijui tufanyeje?, kuacha haiwezekani bora tuendelee tu ipo siku. Ni vizuri mpira ule ulichezwa usiku wakati nimeshakula maana sidhani kama ningepata hamu ya kula. Very sorry!!!
 
Sitaki kabisa kusikia! Unapaisha penalt muhimu kma ile wakati unajua unaandika historia ya kuwafunga waarabu? wanakosa nawe unaosa kuwasawazishia? No NO very boring!

Muulize John Terry final UEFA na Roberto Baggio Final ya Kombe la Dunia au Bastian Schweinsteiger final za UEFA na Abuubakar Salum SURE BOY Kagame Cup Final Zanzibar. Jinsi penati ya mwisho inavtokuwa kaa la moto
 
Mi nahisi LABDA kuna maarifa nje ya uwanja yalifanyika either tulihongwa au sijui nini,Haiwezakani kutowashinda,Nina mashaka makubwa sana na ile mechi,Hivi kweli tulishindwa kumalizia zile penati,
Wachezaji wetu kweli hawana MORALI na ushindi,Kweli sisi ni vichwa vya wendawazimu.
Soka la kibongo sitaki tena,Nimeumia sana
Sorry ,it hurts

Hakuna kitu kama hicho vijana wamepigana lakini bahati aikuwa yao. Nakumbuka AL AHLY kuitoa Yanga sio stori kabisa ila Yanga kuitoa AL AHLY Ingekuwa bonge la stori ndani na nje ya bara la Africa
 
Tatizo dida aliroga alipoweka dawa. Akajiroga na yeye mwenyewe.
 
Kwa kweli inasikitisha na inakatisha tamaa..., Al Ahly walikuwa weupe na wabovu kabisa!! Yanga wanakikosi kizuri na bora lakini mbinu na umakini ni zero... Kikosi hiki na mazingira kama haya wangekuwa Simba tungekuwa tunazungumza mengine sasa hivi...!! Tatizo la YANGA ni uongozi kuendeshwa kwa porojo za kwenye magazeti badala ya kujiwekea mikakati ya ushindi uwanjani... Wamemsakama Bin Zubeiry na kuwatangazia wanaYanga wasusie blog yake, kisa amewaandika vibaya!!!? Upuuzi kama huu hutasikia hata siku moja kwa viongozi wa Simba!!
Acha kuandika unafki ww?, kati ya viongozi wa yanga na simba nani anaendekeza porojo ss hivi? hv tungeshinda jana ungeandikaje??
 
Sitaki kabisa kusikia! Unapaisha penalt muhimu kma ile wakati unajua unaandika historia ya kuwafunga waarabu? wanakosa nawe unaosa kuwasawazishia? No NO very boring!

inauma mkuu lakini we have to accept it.
no way,
 
Mi nahisi LABDA kuna maarifa nje ya uwanja yalifanyika either tulihongwa au sijui nini,Haiwezakani kutowashinda,Nina mashaka makubwa sana na ile mechi,Hivi kweli tulishindwa kumalizia zile penati,
Wachezaji wetu kweli hawana MORALI na ushindi,Kweli sisi ni vichwa vya wendawazimu.
Soka la kibongo sitaki tena,Nimeumia sana
Sorry ,it hurts

manji ni mwarabu na ndiye aliyehongwa ile mechi na waarabu wenzie...
 
Back
Top Bottom