Developer IOS
JF-Expert Member
- Jun 20, 2017
- 1,457
- 1,409
Habar RC wetu mchapakazi jasiri na mwenye kujituma usioogopa kuhatarisha maisha yako kwa ajili ya taifa hili.Pole sana na majukumu makubwa ya kazi ya kuwatetea wanyonge na vijana wa kitanzania.Hongera sana kwa jitihada zako za kutengeneza dar mpya ya mfano wa kuigwa hongera sana kwa ushindi wa kishindo ulioupata kwenye vita yako dhidi ya madawa ya kulevya licha ya upinzani mkubwa ulioupata unastahili kuitwa simba wa vita.
Vita ya madawa ya kulevya imefanikiwa kwa kiasi kikubwa matokeo chanya tunayaona ni wakati wa kutangaza vita mpya katika mkoa wetu yenye lengo la kumkomboa kijana wa kitanzania na kupunguza uhalifu mwisho kuifanya dar kuwa sehemu salama zaidi.Nia tunayo uwezo tunao na sababu tunayo.
Sisi tunaotoka maeneo yaliyoathiriwa kwa kiasi kikubwa na uhalifu tunaelewa na tunafahamu madhara ya uuzwaji kiholela wa dawa aina ya valium aka mbandandu.Mbandandu imekuwa kichocheo kikubwa cha vitendo vya uhalifu.Wahalifu wengi hutumia dawa hizi ili kuondoa roho ya huruma ukiingia mingo zake harudishi panga nyuma.Tunakuomba Mh makonda uingilie kati hili ikiwezekana utafutwe utaratibu mzuri wa kuuza kwa wenye uhitaji wa dawa hizi katika mkoa wetu.
Vijana tupo tutakupa ushirikiano kuhakikisha dar inakuwa mahali salama zaidi.
Kwa pamoja nina imani tutaijenga dar mpya ambayo itakuwa mfano mzuri wa kuigwa Africa nzima
Vita ya madawa ya kulevya imefanikiwa kwa kiasi kikubwa matokeo chanya tunayaona ni wakati wa kutangaza vita mpya katika mkoa wetu yenye lengo la kumkomboa kijana wa kitanzania na kupunguza uhalifu mwisho kuifanya dar kuwa sehemu salama zaidi.Nia tunayo uwezo tunao na sababu tunayo.
Sisi tunaotoka maeneo yaliyoathiriwa kwa kiasi kikubwa na uhalifu tunaelewa na tunafahamu madhara ya uuzwaji kiholela wa dawa aina ya valium aka mbandandu.Mbandandu imekuwa kichocheo kikubwa cha vitendo vya uhalifu.Wahalifu wengi hutumia dawa hizi ili kuondoa roho ya huruma ukiingia mingo zake harudishi panga nyuma.Tunakuomba Mh makonda uingilie kati hili ikiwezekana utafutwe utaratibu mzuri wa kuuza kwa wenye uhitaji wa dawa hizi katika mkoa wetu.
Vijana tupo tutakupa ushirikiano kuhakikisha dar inakuwa mahali salama zaidi.
Kwa pamoja nina imani tutaijenga dar mpya ambayo itakuwa mfano mzuri wa kuigwa Africa nzima