Tetesi: Baada ya kutishwa, Ruge Mutahaba muda mfupi ujao anaenda kupingana na ushahidi uliokuwepo

Status
Not open for further replies.

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
60,426
120,782
Katika hali ya kushangaza kabisa baada ya tukio zima la kutia aibu kama siyo pia la kusikitisha ambalo lilifanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda ( siyo jina lake halisi ) juzi usiku katika Kituo cha tv cha Clouds muda mfupi ujao Bosi na Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti Bwana Ruge Mutahaba anaenda kumtetea Makonda.

Kwa habari za Kiuchunguzi kabisa zinasema kwamba ni kweli tukio lilifanyika na hata Mabosi Wakuu wa Clouds Media Group Kusaga na Mutahaba walikasirishwa mno na Kiktendo kilichofanywa na Makonda lakini baada ya mmoja wao kuitwa na KUTISHWA na wenye Mamlaka na hii nchi hatimaye Ndugu Ruge Mutahaba amekubali KUUPINDISHA ukweli wote ambao kimsingi Watanzania wengi tumeuona.

Katika Interview ambayo Ruge Mutahaba anaenda kuifanya muda mfupi ujao tegemeeni haya yafuatayo:

  1. Anaenda kumtetea kwa nguvu zote Makonda huku akitumia muda mwingi kumsifia.
  2. Anaenda kusema tukio halikutokea Clouds bali lilitengenezwa tu.
  3. Anaenda kusema Makonda hana Uadui na Clouds Media Group.
  4. Anaenda kusema Makonda anafanya Kazi nzuri kwa Tanzania.
  5. Anaenda kumgeuka Mchungaji Gwajima kwa nguvu zake zote.
Ili kuonyesha kuwa Clouds Media Group WAMETISHWA kinyume na hali ambayo ilikuwepo jana asubuhi Ofisini Kwao ambapo karibia Wafanyakazi wote walihamaki na kumlaumu sana Makonda asubuhi hii hii katika Kipindi cha Clouds tv 360 Watangazaji Sam Sasali, Babie Kabae na Hassan Ngoma wametumia muda mwingi kuweza kupinga tukio zima huku wakitucheka sisi Watanzania ambao kiukweli tukio zima tumelipata ile ile juzi usiku na wakimtetea sana Mkuu wa Mkoa Makonda.

Pole sana Ruge Mutahaba najua umetishwa mno jana huku pia ukiogopa kupoteza MASLAHI yako na kibaya zaidi najua umekubali yaishe ILI tu Makonda asiliibue lile sakata lako ambalo nafahamu unalijua mno ambalo linakusaidia pia kukuweka hapa mjini.

Kwa kukusaidia tu tuna Watu wetu hapo hapo Mjengoni Kwako Clouds Media Group ambao wametupa UKWELI wote. Tunasubiri ufanye hiyo propaganda yako ili na sisi tusiopenda UNAFIKI wako / wenu TUFUNGUKE zaidi.
 
Hongera kwa Clouds kama nao hawatasikiliza ya mtandaoni. Clouds ni tishio kwa kazi nzuri wanayofanya ilivyo juu kupita kampuni zingine.

Na kupendwa kwa kipindi hicho na Rais pia ukaribu wa Rac nae kupenda kutumia.

Ndio imeleta haya ya kukuzwa. Inaonekana clouds kuna wafanyakazi wamechoka kazi, wachakachuliwe kwa kula hongo kuchafua kampuni hiyo.

Clip ya video inaonyesha utulivu, namba moja aliye kaa reception amekaa ametulia na Mh. Makonda kaingia kama walivyomzoea. Na ni kiongozi ulini muhimu sanaaaa kwake.

Nyie mnaokuza mambo ndio mjitafakari.

Ooh na vyeti feki navyo mlitengeneza bila kutumia akili,halafu eti nyie wasomi ha ha haaaaa

Makonda oyeeeeeee


Update: naona uzi umepewa u breaking news

Kwa lipi? Ili mtibue ya 360 au hamjui ya Malaika yamekuwepo tangu?

Update:

Ooh now tetesi...bora iwe hivyo as ni uongo mtupu huyu tunamjua zake ha ha haaaa
 
SIJUI KUHUSU HILO ATAKALOONGEA RUGE, LAKINI KWAMBA MAKONDA AMETETEWA KWENYE CLOUDS 360 LEO HII TAREHE 20/3/2017 SIO KWELI, NIMEANGALIA KIPINDI NA SIJASIKIA MAHALI AKITETEWA- SINA HAKIKA KAMA UMEANGALIA WEWE MWENYEWE AU UMEHADITHIWA!!
 
Anaanza kwa kutaja Malkia wa Nguvu.
Ni watu wa fursa. Kwa kujua kwamba kwa leo watakuwa na audience kubwa inayosubiri kwa hamu kusikia kile kilichotokea wao wametumia fursa hiyo kufanya kampeni ya Malkia wa Nguvu kwanza.
 
Leo ndiyo siku ambayo Ruge anajenga au anabomoa

Amini maneno yangu Mkuu usipoteze muda wako kutegemea kusikia jipya kutoka kwa Ruge kwani kilichofanyika jana siku nzima dhidi yake tunakijua. Hawezi kummaliza Mkuu wa Mkoa Makonda wakati Kituo chake cha Clouds Media Group kinafaidika 100% Economically kwa kuwa Kwao tu karibu na Makonda na kwa kukusaidia tu Mkuu ni kwamba kuna Projects kadhaa ambazo Makonda anaenda kuzifanya na Clouds Media Group na ambazo zitawapatia Pesa nyingi sana Kampuni. Wafanyakazi karibia wote hapo wameshalishwa maneno ya Kipropaganda ili kuweza kumtetea Makonda kwa upamoja wao ili tu wamsaidie asiweze kutumbuliwa na Mteule wake kisha na wao maslahi yao yakawa shakani.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom