Baada ya kukutana na mtu mwenye nyota ya simba

Baada ya kukutana na mtu mwenye nyota ya simba

gidume

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2017
Posts
743
Reaction score
915
Hii nyota ni very competitive na nyota yangu tena ni mpinzani haswa, leo kaningurumisha, nadhani siku ya leo ikiisha vizuri kesho nipikiwe pilau kusherekea.

Ilikua asubuhi nzuri baada ya kuamka na kwenda kazini, baada ya hapo asubuhi nikasema subiri nikapate bites mahali nikirudi ofisini nitulie, basi nikachukua usafiri kufika maeneo fulani hivi nikaona jengo ambalo watu wengi wanalichukia ambalo ni la mamlaka ya mapato Tanzania, kulikua na kakiporo cha submission ya kodi nikasema subir inikamalizie kabla nikikaa ofisini nimekaa.

Story inaanzia hapa baada ya kuingia ofisini nikamkuta dada fulani hivi ingawa ni wabkawaida sana ila anaonekana machachari sana, kuuliza shida yangu akasema leta documents kumpa nikaanza kuona analimbikiza penalty, huwaga nina tabia hata nikimjibu mtu vizuri yeye huwa anaona nimemjibu vibaya tu picha likaanzia hapo bana, kumbe nilikutana na mtu opposite katika nyota yangu ni Simba.

Siku ya leo siwezi kuisahau kwa mara ya kwanza tangu nianze kazi miaka mitatu, sasa basi huyu dada baada ya kunilimbikizia makodi nikamjibu simple tu "we naona hatutoelewana wacha niende ninapoenda nitakuja kucheki na wale wengine" basi nikaondoka kutoka kwa hiyo ofisi nikasepa zangu.

Nimefanya ya town nimerudi ofisini namaliza tu kunywa tea naona team ya watu kutoka TRA imevamia, wanataka details zao, basi nikawapa tumefanya malipo fresh, hapo nikaiona nguvu ya pussy, wametumwa na Manager Mkuu kuja kufunga ofisi bila complaints zozote mengine utayajua mbele ya safari.

Mmoja akauliza kuna mtu alikuja ofisini kuleta forms nikasema ni mimi akasema dooh basi umemjibu vibaya sana yule dada na barua hizi hapa sign mtakuja ofisini, nikasign kumbe ndio barua ya yule dada kaongeza penalty maradufu na limbikizo kama la mil 19 hivi wahasibu wanajua.

Sasa ofisi haina hio hela ya kulipa ghafla ivo, tunasubiri kwenda kupiga sound bila kutegemea kufanikiwa, inshu imeniangukia mimi kisa nimemjibu vbaya dada ndio sababu. Tukafunga safari na mkuu wangu kuja hadi ofisini kwao.

Yani Simba anavyotetemesha ni zaidi ya balaa, ni jina la ofisi yetu tu ndio imetawala maghorofa yote kwamba kuna mtu amekuja akajibu vibaya na kuleta fujo hapa mamlaka kwetu kule ofisi zaidi ya watu hamsini wananiangalia mimi kama kisa cha kufungwa kwa ofisi, what a shame.

Kwa mara ya pili leo nyota yangu imeangushwa na binti aisee, imebidi nitoke hata ndani ya jengo na kuomba ruhusa haiwezekani, hivyo nipo nipo tu leo ningekua na mwanamke mpenda chini angenilaumu maana hata angefanyaje isinge simama.

Ila kila lenye mwanzo lina mwisho.
 
Binafsi nazichukia ofisi za TRA kuliko kituo cha police..pole mkuu ila yatapita tu.
 
Trust me huyo demu ukimkazia kwa mtongozo, unampata
 
You should keep it calm. Alaf man madem wa hivyo ndio wale madem visirani, wao dogo kwao kubwa. Akiwa mpenz wako ndio kabisa utakoma, yaan visirani tu vya ajab ajabu
 
Hahahaaa pole mkuu.ila utakuwa na uwalakini wewe si bure kila unayemjibu anaona umemjibu vibaya mh tafakari:chukua hatua
 
You should keep it calm. Alaf man madem wa hivyo ndio wale madem visirani, wao dogo kwao kubwa. Akiwa mpenz wako ndio kabisa utakoma, yaan visirani tu vya ajab ajabu
Na kweli ni kisirani yan kuanzia naongea nae mara ya kwanza..ndio maana nikaona niondoke zangu nikwepe differences..ila ndio imekua kosa tena..
 
Hahahaaa pole mkuu.ila utakuwa na uwalakini wewe si bure kila unayemjibu anaona umemjibu vibaya mh tafakari:chukua hatua
Yani we acha tu..wengine wanasema naongea naringa,wengine wanasema nna lugha mbovu..basi ni atari tupu..lkn kiuhalisia me ni mkimya sanaa..sinaga story na raia..na kila mda nipo serious..sa cjui nn inafanya ivyo..
 
Yani we acha tu..wengine wanasema naongea naringa,wengine wanasema nna lugha mbovu..basi ni atari tupu..lkn kiuhalisia me ni mkimya sanaa..sinaga story na raia..na kila mda nipo serious..sa cjui nn inafanya ivyo..
Mkuu ni maumbile tu ya ukimya sema watu wanashindwa kujua,tatizo wanadamu wanapenda kushobokewa.
 
Pole sana mkuu, huyo demu atakiwa na nyota ya fisi, siiunajuaga fisi na simba wanavyo react
Hahaha yaani ni balaa aisee..nimetamani angekua mzuri ..sema ndio wakaiwa sana..kanichafulia siku cjui ata kesho naamkaje.
 
Back
Top Bottom