kubwa jinga jr
JF-Expert Member
- Mar 19, 2017
- 292
- 309
- Thread starter
- #21
Amani kwenu wadau
Miaka ya nyuma kidogo baada ya kutokea lile sakata lilopelekea kujiudhulu kwa waziri mkuu,na hiyo ni baada ya kusomwa ile ripoti tata ya tume iliongozwa na mwakyembe,
Baada ya pale kulitokea mambo mengi
Miaka ya nyuma kidogo baada ya kutokea lile sakata lilopelekea kujiudhulu kwa waziri mkuu,na hiyo ni baada ya kusomwa ile ripoti tata ya tume iliongozwa na mwakyembe,
Baada ya pale kulitokea mambo mengi
wadau amani kwenu
jana niliamka mapema asubuhi nikaamua kufanya usafi kuzuunguka nyumba yangu kabla ya kufungua biashara yangu duka
Baada ya kufanya usafi mama watoto akaniambia chai na mihogo tayari,nikamjibu anipelekee maji ya kuoga kwanza ili nikimaliza chai nifungue biashara moja kwa moja,bas mama watoto akatekeleza yale maagizo
Nikaingia chooni nikatupa taulo yangu juu ya mlango si mnajua vyoo vyetu vya mikoani nikaamua nikate gogo kidogo,wakati nimechuchumaa ghafla nikasikia nywiiiiiii yaani kwenye pumbu ,kama mtu aliechomwa sindano kwenye pumbu maumivu yake
Nikaruka kimo cha ng'ombe mtoto nikanguuka kwa kishindo,mara wife na watoto na shemeji zangu wakanikuta nimekaa chini nimenyoosha miguu na pumbu zimelala sakafuni,mke akauliza mbona nimepiga yowe na kishindo nikamjibu nimeumwa na dondola alietokea ndani ya shimo la choo akalishambulia pumbu
Kuoga ikashindikana kufika ndani maumivu yake si ya kupima wife akasema hii si bure kuna mkono wa mtu lazima twende kwa mtaalamu kijiji cha pili,basi tukakubaliana tukaelekea kwa mzee mwanafulangenge fykeo,kufika pale akaangalia tv yake ya asili,akasema ni husda kwa kuwa pale kijijini nakuja kwa kasi hivyo nichanjwe chale saba kwenye pumbu kuondoa husda
Baada ya hapo maumivu yamepungua ila pumbu limevimba kama boga
Yote hii husda inakuja kwa vile kilimo kimenikubali na trip za dar kila mwezi kuuza mazao,nina duka nachaji simu na bodaboda,masister duu wa kijiji nao wanashoboka basi ni hofu hofu kijijini kiukweli nakimbiza na nimekamata na nimefunga dishi kwa ajili vijana waburudike
Bado najiuliza sijui ingekuwaje kama yule dondola angemuuma wife sehemu za siri,
Ni hivyo vidogo tu tayari vitimbwi vimeanza je nikiingiza vitz sports rim si ndio watanifukia asubuhi yule dondola si wa kawaida nduguzanguni