Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,461
- 272,006
Imeandikwa tangu enzi na enzi kwamba Shetani hana rafiki , leo usemi huu umedhihirika , Dr Gwajima aliyekuwa upande wa wananchi akashiriki kampeni ya Mungu ya kung'oa ccm madarakani 2015 , akaungana na wananchi kusisitiza wenye vyeti feki kuondolewa baadaye akawageuka wananchi pamoja na Mungu na kuamua kuungana tena na wale wale aliopambana nao ! Haifahamiki kama alilipwa chochote ama aliahidiwa nafuu yoyote .
Sasa leo wamemtengenezea sinema mpya baada ya ishu ya madawa ya kulevya kushindikana , haijalishi kama watafaulu ama watafeli lakini hii ni ishara ya Mungu kuchukizwa na usaliti wake , ikumbukwe kwamba Yesu Kristo pamoja na uwezo wake mkubwa kuliko Gwajima hakuwahi hata mara moja kumsaliti Mungu , hakuwahi kuungana na watekaji hata kwa ahadi gani .
Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kwamba anayefuatia ni Zakaria Kakobe , lengo kuu likiwa ni kuwadhalilisha wote waliojifanya kupigania wananchi huko mwanzo na sasa wameungana na watawala ili kuwaonyesha wananchi kwamba kumbe watu hawa si lolote na wala hawakuwa lolote
Sasa leo wamemtengenezea sinema mpya baada ya ishu ya madawa ya kulevya kushindikana , haijalishi kama watafaulu ama watafeli lakini hii ni ishara ya Mungu kuchukizwa na usaliti wake , ikumbukwe kwamba Yesu Kristo pamoja na uwezo wake mkubwa kuliko Gwajima hakuwahi hata mara moja kumsaliti Mungu , hakuwahi kuungana na watekaji hata kwa ahadi gani .
Taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha kwamba anayefuatia ni Zakaria Kakobe , lengo kuu likiwa ni kuwadhalilisha wote waliojifanya kupigania wananchi huko mwanzo na sasa wameungana na watawala ili kuwaonyesha wananchi kwamba kumbe watu hawa si lolote na wala hawakuwa lolote