Baada ya CCM kuzidiwa Kete na CHADEMA Arusha,sasa waja na Mbinu mbadala.soma hapa!!

sokoinei

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
1,832
566
Kweli waliosema ukishangaa ya MUSA utashuhudia ya Firauni hawakukosea.! Chama cha Mapinduzi baaada ya kuona kuwa Mbinu zote za kuichafua CHADEMA hapa Arusha Mjini zimeshindwa haswa kwa ile mbinu ya kuiita ni chama cha Wachagga leo nimeshuhudia kituko kingine.

Ikumbukwe kwamba CHADEMA walikuwa wakitumia uwanja wa NMC kama uwanja wao wa Mikutano mikubwa na midogo.
Lakini mwishoni mwa mwaka jana Mkuu wa mkoa na mkurugenzi walihalalisha uwanja huo wa NMC kufanywa Soko.

Baada ya hapo CHADEMA wakawa wanautumia uwanja wa shule ya Ngarenaro ambao mara zingine ulishindikana kutumiwa kwa ajili ya wanafunzi ambao wanakuwa shuleni siku za kazi.

Viwanja vya Soweto vipo chini ya AICC na na miaka yote vimekuwa vikutumika na watu kwa michezo mbalimbali bila masharti yeyote. Lakini cha kushangaza leo nikiwa napita maeneo yale nilifanikiwa kuona VIBAO VYA MATANGAZO vikiwa vimewekwa kuzunguka uwanja wote maneno yenyewe ni haya; ILANI. HAIRUHUSIWI KUFANYA MICHEZO AINA YEYOTE AU "SHUGHULI NYINGINE YEYOTE" KATIKA VIWANJA HIVI BILA IDHINI YA UONGOZI. BY UTAWALA WA AICC.

Hii yote ni mbinu inayofanywa na Ccm kuhakikisha kuwa CHADEMA hawapati eneo la karibu mjini hapa kufanya mikutano. Sasa uwanja wa shule ya Ngarenaro nao unazungushiwa uzio na manispaa ktk kilekile cha kuhakikisha kuwa CHADEMA wakitaks kufanya Mkutano wao basi either waende viwanja vya Suye au Kimandolu nje kabisa ya mji.

CHADEMA kwa Arusha ipo Mioyoni mwa watu na sio viwanjani. Kitendo cha Ccm na washirika wake kuzuia viwanja vyote kutotumika na CHADEMA hakutasababisha watu na wapenzi wa CHADEMA kuacha kuiunga Mkono.

Hii ni sawa na kujaza maji kwenye gunia wakati unajuwa kuwa huwezi kujaza hata ukitumia water pump!!
 
Chadema wakichukua nchi viwanja vyote ikiwemo uwanja wa sheikh amri abeid vinarudishwa kwa umma

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Na isiishie hapo itaifishe mali zote zilizopatikana kwa njia ya kifisadi..ITANGAZE KITU KAMA AZIMIO LA ARUSHA
 
nakubariana na wewe kamanda chadema nichama nasio viwanja ata wakifunga pote imani ya wananchi kwasasa iko chadema kazeni but
 
Bahati mbaya sana hivyo vikwazo vyote wanavyoviweka sasa, soon vitatumika against ccm wenyewe walioviweka.
 
Hayo yote yanaratibiwa na RC Malongo ila nawaambia ya kwamba HAKIKA MWISHO WAKE WAJA TU!
 
Wajinga wakubwa Kikwete na matala yake wamefyatuka akili ina maana watu wa Arusha hawaitaji kukkutana kwenye mambo yoyote wawafungie wananchi kwa sababu ya kujifurahisha watawala makaburu walifunga kila mahala wakasema waafrika hawapaswi kupita hapa na bado watu wakapata uhuru wa kweli itakuwa hao mamburura akina mulongo, wananvchi wanafahamu hira zao kwa hiyo hawatazuia kitu ,wajue wanao wazuia ndio walinzi wa maeneo hayo
 
Kwani tatizo ni nini?kufanya michezo na shuguli zingine kwa kufuata taratibu ndiyo kazi?Mi nilijua wamebadili kazi ya viwanja kama NMC.
 
Mbona hata Uchaguzi wa Madiwani Kata 4 bado? Siasa za Arusha bwana!!!!!!!

Ili kuikata ngebe Arusha ni kuiwekea TUME YA JIJI LA ARUSHA km ile ya Keenja km patatokea tena fujo 14/July ili vitu vyote mjue ni vyenu, maana badala ya kujenga nyumba moja mnang'ang'ania na kunyang'anyana fito ni lini mtajenga Mji wenu sio kuona watalii wakirandaranda na nyie mashuka mekundu hata mchana mnasahau hata kutenga Standa ya mabasi, mnaacha tunaibiwa mchana kweupe.

Nasikia mashamba ya burka kote mmegawa viwanja mkasahau hata kutenga eneo la stand kisa hatumtaki MEYA. Wenzenu wanapanua Miji na misongamano inawekwa nje kabisa ya miji, DSM, Morogoro, Gairo, Dodoma, Singida nk. Mji wa Arusha ni wa watu wote lakini umemezwa na wageni ambao si Waarusha wala Wameru na Wamaasai.

Arusha acheni tofauti za kisiasa jengeni Mji ni wenu.
 
Hayo yote yanaratibiwa na RC Malongo ila nawaambia ya kwamba HAKIKA MWISHO WAKE WAJA TU!

Juzi kati nusura alete zogo, manake TABOA waliadhimia kugomea kusafirisha abiria kisa huyo kwenye bold. Baada ya SUMATRA kutoa go-ahead ya Noah kubeba watu, yeye akajipa kimbelembele cha kutengeneza by laws kiasi cha kuleta mgongano.

Kiongozi mmoja wa TABOA aliongea na Radio One asubuhi ya wiki hiyo na kumkumbusha kwenye bold kwamba, yeye ni mkuu wa mkoa na sio SUMATRA. Inaelekea ana kiherehere sana huyo
 
Chadema wakichukua nchi viwanja vyote ikiwemo uwanja wa sheikh amri abeid vinarudishwa kwa umma

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Sio viwanja tuu mkuu zipo rasilimali nyingi sana za umma walipora wakati vikianzishwa vyama vingi hivo vyote ni vya kurudisha!
 
Kweli waliosema ukishangaa ya MUSA utashuhudia ya Firauni hawakukosea.! Chama cha Mapinduzi baaada ya kuona kuwa Mbinu zote za kuichafua CHADEMA hapa Arusha Mjini zimeshindwa haswa kwa ile mbinu ya kuiita ni chama cha Wachagga leo nimeshuhudia kituko kingine.

Ikumbukwe kwamba CHADEMA walikuwa wakitumia uwanja wa NMC kama uwanja wao wa Mikutano mikubwa na midogo.
Lakini mwishoni mwa mwaka jana Mkuu wa mkoa na mkurugenzi walihalalisha uwanja huo wa NMC kufanywa Soko.

Baada ya hapo CHADEMA wakawa wanautumia uwanja wa shule ya Ngarenaro ambao mara zingine ulishindikana kutumiwa kwa ajili ya wanafunzi ambao wanakuwa shuleni siku za kazi.

Viwanja vya Soweto vipo chini ya AICC na na miaka yote vimekuwa vikutumika na watu kwa michezo mbalimbali bila masharti yeyote. Lakini cha kushangaza leo nikiwa napita maeneo yale nilifanikiwa kuona VIBAO VYA MATANGAZO vikiwa vimewekwa kuzunguka uwanja wote maneno yenyewe ni haya; ILANI. HAIRUHUSIWI KUFANYA MICHEZO AINA YEYOTE AU "SHUGHULI NYINGINE YEYOTE" KATIKA VIWANJA HIVI BILA IDHINI YA UONGOZI. BY UTAWALA WA AICC.

Hii yote ni mbinu inayofanywa na Ccm kuhakikisha kuwa CHADEMA hawapati eneo la karibu mjini hapa kufanya mikutano. Sasa uwanja wa shule ya Ngarenaro nao unazungushiwa uzio na manispaa ktk kilekile cha kuhakikisha kuwa CHADEMA wakitaks kufanya Mkutano wao basi either waende viwanja vya Suye au Kimandolu nje kabisa ya mji.

CHADEMA kwa Arusha ipo Mioyoni mwa watu na sio viwanjani. Kitendo cha Ccm na washirika wake kuzuia viwanja vyote kutotumika na CHADEMA hakutasababisha watu na wapenzi wa CHADEMA kuacha kuiunga Mkono.

Hii ni sawa na kujaza maji kwenye gunia wakati unajuwa kuwa huwezi kujaza hata ukitumia water pump!!

TIME WILL TEL ukizingatia sasa tunapata mafunzo jkt, ccm siwanajivunia wazee wachache huko vijijin. chenye mwanzo kina mwisho
 
Back
Top Bottom