Life2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,387
- 4,880
Baada ya Majimbo ya Kyiv kukombolewa Bucha ikiwemo ndani yake na kushuhudia mauaji ya halaiki yaliyofanywa na wanajeshi wa Urusi dhidi ya raia wa Ukraine sasa ni zamu ya Izium.
Kama hii ndio special operation aliyojinadi Putin itakua ya masaa 72 siku tatu ya kuua malaki ya raia wa Ukraine wasio na hatia hakika Mungu azidi kuwapa nguvu raia wa Ukraine wanapozidi kupambania nchi yao na uhuru wao wa kujitawala,wanapitia kipindi kigumu sana hakika.
Mbaya zaidi ni vita ambavyo Putin kakaa ikulu na kuamrisha wanajeshi wake nendeni mkaue huko Ukraine kwa kigezo cha Special Operation ile KAULI YA VITA ISIKIE KWA JIRANI SASA NDIO NAANZA KUAMINI,ndugu zangu vita ni mbaya vita haifai nashauri hata rafiki yako akikuchokoza kimbia nenda kalale.
Baada ya majuzi wanajeshi wa Ukraine kupiga Counter offensive ya nguvu na kuchukua asilimia kubwa ya jimbo la Khakhiv zaidi ya makaburi 400 ya halaiki yamepatikana msituni huku mengi baada ya kufukuliwa wamekutwa raia wa Ukraine wakiwa wamezikwa tena wengine ni watoto hapo kuna familia/koo zimefutika kabisa kwa idadi wanasema ni maelfu ya watu.
Baada ya Mariopol na Kherson kukombolewa tutashuhudia maafa mengine ya mauaji ya halaiki kwa raia wasio na hatia, nlitegemea hili nafikiri kati ya majeshi wasio na nidhamu/weredi ni wanajeshi wa Rusia sababu nyepesi tu jeshi lina vikundi vingi sana mara Wagner group, Kaydrov...nk wakipigana kwa makubaliano ya kulipwa hawa watajali pesa na uporaji tu.
Kwa mfano wa karibu Wagner group wameanza kupita magerezani na kutafuta wafungwa kwa kigezo baada ya vita kwisha kama hujafa unatolewa gerezani ndio msamaha wako.
Poleni sana wa UKRAINE kwa mnayo pitia
Aljazeera news saa tatu. Grave after grave, local police says 440 bodies has been found.
Kama hii ndio special operation aliyojinadi Putin itakua ya masaa 72 siku tatu ya kuua malaki ya raia wa Ukraine wasio na hatia hakika Mungu azidi kuwapa nguvu raia wa Ukraine wanapozidi kupambania nchi yao na uhuru wao wa kujitawala,wanapitia kipindi kigumu sana hakika.
Mbaya zaidi ni vita ambavyo Putin kakaa ikulu na kuamrisha wanajeshi wake nendeni mkaue huko Ukraine kwa kigezo cha Special Operation ile KAULI YA VITA ISIKIE KWA JIRANI SASA NDIO NAANZA KUAMINI,ndugu zangu vita ni mbaya vita haifai nashauri hata rafiki yako akikuchokoza kimbia nenda kalale.
Baada ya majuzi wanajeshi wa Ukraine kupiga Counter offensive ya nguvu na kuchukua asilimia kubwa ya jimbo la Khakhiv zaidi ya makaburi 400 ya halaiki yamepatikana msituni huku mengi baada ya kufukuliwa wamekutwa raia wa Ukraine wakiwa wamezikwa tena wengine ni watoto hapo kuna familia/koo zimefutika kabisa kwa idadi wanasema ni maelfu ya watu.
Baada ya Mariopol na Kherson kukombolewa tutashuhudia maafa mengine ya mauaji ya halaiki kwa raia wasio na hatia, nlitegemea hili nafikiri kati ya majeshi wasio na nidhamu/weredi ni wanajeshi wa Rusia sababu nyepesi tu jeshi lina vikundi vingi sana mara Wagner group, Kaydrov...nk wakipigana kwa makubaliano ya kulipwa hawa watajali pesa na uporaji tu.
Kwa mfano wa karibu Wagner group wameanza kupita magerezani na kutafuta wafungwa kwa kigezo baada ya vita kwisha kama hujafa unatolewa gerezani ndio msamaha wako.
Poleni sana wa UKRAINE kwa mnayo pitia
Aljazeera news saa tatu. Grave after grave, local police says 440 bodies has been found.