BAA KWENYE MAKAZI YA WATU: Serikali ilichukulie kwa uzito

msem

JF-Expert Member
Nov 7, 2015
1,833
1,628
Siku za karibuni tumesikia tamko la serikali kupitia baraza la mazingira (NEMC) likitoa tamko la kukazia marufuku ya kelele katika makazi ya watu na kwamba atakayekwenda kinyume atachukuliwa hatua kali.

Katika hili tunaipongeza serikali lakini tunaiomba serikali "kukaza buti" katika kanuni na sheria zake zinazokataza uwepo wa vitu hivi kwenye makazi ya watu kwani athari zake ni kubwa katika jamii,kwa uchache wa kuzitaja kero hizo ni kama kelele zinazobughudhi wanafunzi wanaojisomea majumbani na hata wagonjwa waliopumzika,mmomonyoko wa maadili kwa watoto wanaoishi jirani na baa hizi,taka zinazotupwa na kuzagaa hovyo katika maeneo jirani n.k.

Nionavyo mimi udhibiti wa vitu hivi kwenye makazi ni rahisi sana( kama kweli serikali ina nia ya dhati kutatua tatizo hili) na kama kukiwa na ufuatiliaji makini ndani ya masaa 24 vitu hivyo vitabaki kuwa historia kwenye maeneo ya makazi;kwa mfano,baraza la mazingira lingeweza "kuwatask" wenyeviti wa serikali za mitaa wakishirikiana na mabalozi wa nyumba kumi kuhakikisha kwamba wanatoa taarifa mara moja kwenye baraza pale inapobainika uwepo wa vitu hivi kwenye mitaa yao ili kwamba kama kitu cha namna hiyo kitaonekana kwenye mtaa husika basi viongozi hao wa mtaa wachukuliwe kuwa ni majipu yanayostahili kutumbuliwa mara moja,au kama viongozi wa mtaa wameshareport NEMC nayo ikashindwa kuchukua hatua basi ijulikane kuwa NEMC nayo ni jipu.

Kasi inayotumika kudhibiti ujenzi holela ingetumiwa na NEMC kwenye kero hii nadhani serikali ingekuwa imeshafunika "chapter" hii,lakini tumebaki tunaulizana wataanza lini manake tangu tangazo kutoka mpaka leo hatuoni utekelezaji.

Tuna imani na serikali yetu,tuna imani kwa usikivu wake italifanyia kazi tatizo hili,pamoja na kwamba wapo watakaoumia lakini ni wachache kulinganisha na wengi wanaoumizwa na hili.
 
Siungi mkono hoja
Huku ni kututafuta uchokozi sisi wanywaji! Ulitaka baa zijengwe mbugani kwani ni wanyama pori ndiyo wateja?
Ishauri basi serikali ipige marufuku kuwa na viungo vya uzazi kabla ya miaka 18 kwa kuwa havina matumizi kabla ya hapo.... fyuuuuuuuuuu!
 
Bar inakuumiza nini? Wewe kama huingii bar inakuhusu nini? Biashara nyingi za bar ziko kando ya barabara na sio pembeni mwa nyumba yako. Halafu pendekeza basi hata sehemu mbadala wa kuweka hizo baa. Au unafikiri haziko kwa mujibu wa sheria za nchi?

Unajua ni kiasi gani cha kodi TBL na wenye mabar wanalipa kama Kodi serikalini? Ukifunga hizo bar watauzia wapi hizo bia mmpate hizo kodi za kuwapeleka watoto wenu shule bure.

Nchi hii haina maeneo yaliyotengwa kwa bar, au kama zipo ndio hapo ilipo.Kama unaona kero si uhamie sehemu isiyo na bar? Au tuambie basi hiyo bar unayozungumzia wewe iko umbali gani toka kwako tujue unasumbukaje kama sio majungu, wivu na udini wa kupuuzi. Mbona usizungumzie malaoud spika kwenye misikiti iliyokaa kwenye makazi ya watu?
 
Well ndugu, kweli bar zimekuwa kero kiasi Fulani.

Sheria ya mazingira hairuhusu noise pollution inayozidi decibels flani (kiwango cha sauti). Bars hazitakiwi kubughudhi watu kwa masauti ya miziki.

Bars au pubs lazima zifuate sharia. Zinaweza kuweka sound proof na watu wakae ndani, wanywe na wapigiwe music bila kubughudhi watu. Wamiliki wengi wa bars, pubs na clubs wamekuwa hawawekezi vya kutosha kwenye sound proof.

Kero nyingine ni ya kunywa nje barabarani kwa mfano Sea park Kinondoni, MK Kijitonyama nk. Wakataze kabisa bars au pubs kuoperate maeneo ya wazi kwa usalama wa wanywaji kwa sababu ya vumbi na uchafu mwingine kuingia kwa chakula na vinywaji. Ukienda ulaya pubs ni za ndani na wanafuata sharia.
 
Well ndugu, kweli bar zimekuwa kero kiasi Fulani.

Sheria ya mazingira hairuhusu noise pollution inayozidi decibels flani (kiwango cha sauti). Bars hazitakiwi kubughudhi watu kwa masauti ya miziki.

Bars au pubs lazima zifuate sharia. Zinaweza kuweka sound proof na watu wakae ndani, wanywe na wapigiwe music bila kubughudhi watu. Wamiliki wengi wa bars, pubs na clubs wamekuwa hawawekezi vya kutosha kwenye sound proof.

Kero nyingine ni ya kunywa nje barabarani kwa mfano Sea park Kinondoni, MK Kijitonyama nk. Wakataze kabisa bars au pubs kuoperate maeneo ya wazi kwa usalama wa wanywaji kwa sababu ya vumbi na uchafu mwingine kuingia kwa chakula na vinywaji. Ukienda ulaya pubs ni za ndani na wanafuata sharia.
Well ndugu, kweli bar zimekuwa kero kiasi Fulani.

Sheria ya mazingira hairuhusu noise pollution inayozidi decibels flani (kiwango cha sauti). Bars hazitakiwi kubughudhi watu kwa masauti ya miziki.

Bars au pubs lazima zifuate sharia. Zinaweza kuweka sound proof na watu wakae ndani, wanywe na wapigiwe music bila kubughudhi watu. Wamiliki wengi wa bars, pubs na clubs wamekuwa hawawekezi vya kutosha kwenye sound proof.

Kero nyingine ni ya kunywa nje barabarani kwa mfano Sea park Kinondoni, MK Kijitonyama nk. Wakataze kabisa bars au pubs kuoperate maeneo ya wazi kwa usalama wa wanywaji kwa sababu ya vumbi na uchafu mwingine kuingia kwa chakula na vinywaji. Ukienda ulaya pubs ni za ndani na wanafuata sharia.
Bila kunywa sie mtasomesha bure watoto wenu? Bar ni hudumu za jamii, hazijengwi "Mbugani"
 
Back
Top Bottom