Tuandamane
JF-Expert Member
- Feb 2, 2008
- 1,220
- 52
Mbunge alalamikia kutukanwa na wananchi
JIBU LA SWALI LA MBUNGE JIMBO LA ILALA
MBUNGE wa Ilala, Musa Azzan Zungu (CCM), amelalamikia kutukanwa na wananchi wake kutokana na kutokarabatiwa kwa Barabara ya Uhuru jijini Dar es Salaam, ambayo ni kero kwa wananchi hao.
Akiuliza swali la nyongeza bungeni jana, mbunge huyo alisema kuwa ubovu wa barabara hiyo umekuwa ukimsababishia matatizo na kutoelewana na wananchi wake, ambapo baadhi yao wamefikia hatua ya kumtolea lugha ya matusi kutokana na kutokarabatiwa kwa barabara hiyo.
Aliiomba serikali kutoa kipaumbele kwa barabara hiyo muhimu na yenye historia katika nchi, ambayo pia itasaidia kuwapunguzia kero wananchi katika jimbo lake.
Hivi mimi mbunge natukanwa kwa kosa gani hasa? Naomba serikali iingilie kati ujenzi wa barabara hii na iitazame kwa jicho la huruma, alisema.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Celina Kombani, alisema kuwa serikali ikipata fedha itatoa kipaumbele katika barabara hiyo, ili kumsaidia mbunge kuepukana na matusi hayo ya wapiga kura.
Swali hilo la nyongeza liliulizwa kufuatia swali la msingi lililoulizwa na Mbunge wa Masasi, Raynald Mrope (CCM), aliyetaka kujua mpango wa Serikali katika kuzifanyia ukarabati barabara za Masasi na zile zilizopo Masasi Magharibi.
Akijibu swali hilo, Kombani alisema katika mwaka wa fedha 2007/08, fedha zimetolewa kufanya matengenezo ya kawaida kwa kilometa 488 kwa gharama ya sh milioni 327.5, ambapo matengenezo hayo yatalenga sehemu korofi, madaraja, makalavati na matengenezo ya muda maalumu.
Maoni ya Wasomaji
khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.... yani kumbe mpaka wabunge watukanwe ndio barabara ipewe kipaumbele kutengenezwa?????????
jamani tunakwenda wapi
JIBU LA SWALI LA MBUNGE JIMBO LA ILALA
MBUNGE wa Ilala, Musa Azzan Zungu (CCM), amelalamikia kutukanwa na wananchi wake kutokana na kutokarabatiwa kwa Barabara ya Uhuru jijini Dar es Salaam, ambayo ni kero kwa wananchi hao.
Akiuliza swali la nyongeza bungeni jana, mbunge huyo alisema kuwa ubovu wa barabara hiyo umekuwa ukimsababishia matatizo na kutoelewana na wananchi wake, ambapo baadhi yao wamefikia hatua ya kumtolea lugha ya matusi kutokana na kutokarabatiwa kwa barabara hiyo.
Aliiomba serikali kutoa kipaumbele kwa barabara hiyo muhimu na yenye historia katika nchi, ambayo pia itasaidia kuwapunguzia kero wananchi katika jimbo lake.
Hivi mimi mbunge natukanwa kwa kosa gani hasa? Naomba serikali iingilie kati ujenzi wa barabara hii na iitazame kwa jicho la huruma, alisema.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Celina Kombani, alisema kuwa serikali ikipata fedha itatoa kipaumbele katika barabara hiyo, ili kumsaidia mbunge kuepukana na matusi hayo ya wapiga kura.
Swali hilo la nyongeza liliulizwa kufuatia swali la msingi lililoulizwa na Mbunge wa Masasi, Raynald Mrope (CCM), aliyetaka kujua mpango wa Serikali katika kuzifanyia ukarabati barabara za Masasi na zile zilizopo Masasi Magharibi.
Akijibu swali hilo, Kombani alisema katika mwaka wa fedha 2007/08, fedha zimetolewa kufanya matengenezo ya kawaida kwa kilometa 488 kwa gharama ya sh milioni 327.5, ambapo matengenezo hayo yatalenga sehemu korofi, madaraja, makalavati na matengenezo ya muda maalumu.
Maoni ya Wasomaji
khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.... yani kumbe mpaka wabunge watukanwe ndio barabara ipewe kipaumbele kutengenezwa?????????
jamani tunakwenda wapi