Azimio la Arusha ni kichefuchefu???

Topical

JF-Expert Member
Dec 3, 2010
5,173
935
Nakisoma hichi kitabu ambacho kila mwanasiasa hasa wa ccm na chadema hupenda kuki-refer naona kichefuchefu nafikiri kuna haja ya kuipinga kwa nguvu zote ili isiendelee kupotosha vijana wetu kwani ina endekeza yafuatayo:-

a. Dhana ya usawa ambayo maana yake ni kumnyang'anya binadamu mwingine nyumba yake (case of msajili wa nyumba), watu walikopa na ku-save kujenga nyumba lakini ananyang'anywa ili awe sawa na wegine?? nonsense; wenyeji wazalendo wenye mashamba wananyang'anyi na kila moja kupewa ekari tano tu (case study of vijiji vya ujamaa kote nchini); vijiji vingi vimejengwa katika mashamba wenyeji ambao wameng'oa magogo kwa nguvu zao hivyo kuwafanya wenyeji wenye uwezo kuwa maskini kama wenzao..

-dhana hii imesababisha hata serikali kurithi tabia hii ya unyang'anya iliyotokana na arusha declaration mfano kuuza nyumba za umma kwa watu binafsi..

- dhana mbaya pia imesababisha hata serikali kurithi tabia ya kuuza na kunyang'anya wachimbaji wadogo wadogo mali na maeneo yao na kuwapa wawaekeji source ni tabia ya kufikiri kuwa serikali inaweza kudhulumu, kunyang'anya mali za watu binafsi na chanzo kikuu ni Arusha declaration ... hii na ni sumu kubwa kwa vijana wetu kuibeba

b. Dhana kwamba kiongozi hatakiwi kuwa na mali, na kuwa na mali ni disqualification ya kuwa kiongozi ni dhana yenye kuendekeza umaskini na ubaguzi. kwasababu si kila Tajiri ni mwizi na si kila maskini si mwizi. uwizi ni tabia na haitokani na uwezo..kuna viongozi wazuri tu wenye mali; ile kuweza kuongoza na kumanage mali ni sehemu ya uzoefu wa kuendesha mambo..

Napendekeza Arusha declaration ibakie kwenye archives kama sera ambayo tuliwahi kuitumia na haifai kutumiwa tena Tanzania; kwani ina upungufu mkubwa sana kwakuwa dhana yenyewe inaendekeza ubaguzi in the name of usawa..
 
The principles were set at the beginning of race in a view of developing in every possible way the community and not individuals.....before I say more can some great thinker upload this important document? Have enjoyed over time JF uploads and before I go deeper would appreciate appraising my self with the famous "Arusha Declaration"
 
Haaa haaa! Azimio la Arusha limeshazikwa na Azimio la Zanzibar, so there is nothing to worry about! Mafisadi endeleeni kukwapua mali na kujilimbikizia huko Off Shore maana Benki zetu hazina maana yoyote kwenu! Ipo siku mtauawa mkiwa kwenye mifereji ya maji taka kama Gadaffi ambaye utajiri wake haujumsaidia kukwepa kuonja mauti!
 
Back
Top Bottom