Azam vs yanga updates


Una akili nyingi sana wewe. Mungu akubariki sana.
 

Hiyo ni analysis yangu - siyo rule of thumb, kwa hiyo you are rightly entitled to your opinion.

Basis ya analysis yangu ni vitu vya msingi kwenye SWOT framework yangu.

Nikianzia kwa Mtibwa, kuna paragraph nimeelezea kwa nini siwategemei kuwepo hata kwenye tatu bora.

Kuhusu Coastal, etc sababu za kutowa-consider ni kama zile za Mtibwa. Pia kumbuka kuwa msimu bado hata nusu haujafika na mara nyingi "brutal reality" catches up with most of these so called "small teams" kadri msimu unavyosogea mbele.

Simba wako vizuri sana technically (thanks to the genius of Phiri) ingawa sina uhakika sana kwa upande wa uongozi wao. Wasipobadili benchi la ufundi wanaweza kufanya vizuri sana na hata kuchukua ubingwa, ingawa nawapa probability ndogo kulinganisha na Azam & Yanga.

Azam na Yanga wao wana depth ya kutosha kwenye vikosi vyao na kiufundi hawatofautiani sana. Kwa nini nimewapa Yanga nafasi kubwa kuliko Azam? Kwa vile trend ya miaka ya karibuni imeonyesha Yanga haichii ubingwa ukae "porini" kwa zaidi ya msimu mmoja - na hiyo ndiyo itakuwa motivating factor.

Ila kuelekea mwishoni itakuwa ni hotly contested 3-horse title race (i.e Azam, Simba & Yanga).
 
Sawa, ila tusisahau pia kuwa mpira unadunda, kwa maana ya kuwepo matokeo yasiyotabirika. Husemwa kuwa 'kama unatabirika, basi si mpira huo' (it is not football if it is predictable). Huenda kutotabirika huko ndiko kutakozinufaisha hata hizo timu ndogo tusizozipa nafasi licha ya kuwa juu hivi sasa.
 


Kwa jinsi ulivyofanya analysis, kuna kila sababu ya kukupongeza. Una akili sana ya mpira.
Ninakubaliana kwa kiwango kikubwa na kile ulichokielezea maana kadiri msimu unavyosonga ndivyo kile unachokiita brutal reality kitadhihirika kwa timu aina ya Mtibwa.

Kama ulivyosema, Simba wanaonekana wako vizuri kiufundi kuliko kiutawala. Wakitulia wanaweza kushangaza wengi. Na kitu kizuri kwa Simba ni kuwa 'inaweza' kuzifunga timu zote shindani kama Yanga na Azam kuliko Mtibwa kuzifunga tena Yanga, Simba au kupata matokeo mazuri dhidi ya Azam.

Kwa jinsi mambo yalivyo naipa nafasi zaidi Azam 35%, Yanga 30% na Simba 25% kuwa bigwa wa VPL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…