Azam TV tafuteni wakalimani

Azam TV tafuteni wakalimani

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,618
Reaction score
39,977
Kinachoendelea hapa KMC Complex kwenye mahojiano baada ya Mechi ya KMC dhidi ya Singida BS Kati ya Mtangazaji na makocha Gamond na Maximo ni aibu.
 
Kinachoendelea hapa KMC Complex kwenye mahojiano baada ya Mechi ya KMC dhidi ya Singida BS Kati ya Mtangazaji na makocha Gamond na Maximo ni aibu.
Nenda ulaya uone kama kuna mtu atahangaika kukutafutia mkalimani.

Ifike hatua tutambue na kuthamini lugha yetu, hata kama English ndio global language huoni jinsi wanavyohakikisha wanajua kichina, kijerumani, kifaransa, kiarabu na lugha za watu wanaotambua thamani ya kuwa na utambulisho?
 
Sasa mbona hata huyo Maximo na Gamondi hawaongei Kiingereza kilichonyooka!! Halafu kwetu sisi, Kiingereza ni lugha ya pili! Kwa hiyo hakuna sababu ya kuwalazimisha watangazaji kuongea Kiingereza unachokitaka wewe. Muhimu concept imeeleweka!

Kwanza kulitakiwa kuwekwe sheria kwa makocha na wachezaji wote wa kigeni kupewa darasa maalum la kujifunza lugha ya Kiswahili, kama sehemu ya kuikuza na kuieneza ulimwenguni kote.
 
Nyie mnaojua french language tuambieni yule Pablo Almasi wa Crown Media anajua au vipi. kwakuwa mm kwny hiyo lugha ZERO namwona anajua sana nikimsikia anavyoflow
 
  • Thanks
Reactions: al1
Back
Top Bottom