Azam TV acheni kutuchakachua

Azam TV acheni kutuchakachua

Ta Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 17, 2011
Posts
3,547
Reaction score
2,194
Mimi ni Mmiliki wa kisimbuzi cha Azam, nimelipia package ya Sports. Cha kushangaza napata Azam Sport HD, Man Utd, Liverpool TV na Madrid TV.

Naomba kuuliza, hivi Fox Sport siyo channel ya michezo au Kombat Sport, MCS International Sport, hizi channel si za sports?

Kwanini hamziweki kwenye package ya sports?

Acheni kutuibia, kama mmeshasema channel za sports ni elfu 15, basi tuwekeeni channel zote za sports, na sio kutupiga changa la macho na hiyo Azam HD pekee. Au nyie hizi channel mnaziitaje kama sio za sports?

Acheni utapeli wa mchana kweupe tuwekeeni hizo channel kwenye package ya sports.

Au mmeanza kulewa Sifa kama DSTV?
 
Azam leteni majibu mbona vingine mnajibu fasta tu?
 
wewe ulitaka vipi labda manake zinapatikana still
 
Kila kitu Tanzania ni uamuzi tuu wa mtoa huduma, anawaibia wananchi na serikali kuu inaona lakini hakuna usimamizi.
 
Bora uwaambie mkuu kwa sababu na mimi hapa nilikuwa najiandaa kulipia hiyo azam sport kumbe ovyo tu!?
 
Mimi ni Mmiliki wa kisimbuzi cha Azam, nimelipia package ya Sports. Cha kushangaza napata Azam Sport HD, Man Utd, Liverpool TV na Madrid TV.

Naomba kuuliza, hivi Fox Sport siyo channel ya michezo au Kombat Sport, MCS International Sport, hizi channel si za sports?

Kwanini hamziweki kwenye package ya sports?

Acheni kutuibia, kama mmeshasema channel za sports ni elfu 15, basi tuwekeeni channel zote za sports, na sio kutupiga changa la macho na hiyo Azam HD pekee. Au nyie hizi channel mnaziitaje kama sio za sports?

Acheni utapeli wa mchana kweupe tuwekeeni hizo channel kwenye package ya sports.

Au mmeanza kulewa Sifa kama DSTV?

Wabongo sijui tuko vipi, ina maana ulilipia hiyo package bila kujua contents zake? Ndio maana kuna "Vigezo na masharti kuzingatiwa."
 
Mimi receiver yangu iliungua lkn cha ajabu eti hazitengenezeki na wala hawauzi mbadala kama Dstv,badilikeni bwana
 
Mimi receiver yangu iliungua lkn cha ajabu eti hazitengenezeki na wala hawauzi mbadala kama Dstv,badilikeni bwana

Unashangaa ilo Mkuu? Hata kuhamisha channel huwezi Mkuu cjui receiver yao ni ya kihindi au kichina!
 
wewe ulitaka vipi labda manake zinapatikana still

Nilikuwa namaanisha wanaposema ukitaka channel za michezo unalipia elf 15, lakini cha ajabu channel zingine za michezo hazipo kwenye iyo package ingawa n za michezo kama fox sport, kombat sport Na MCs sport au wewe unatafisiri VP mkuu
 
Bora uwaambie mkuu kwa sababu na mimi hapa nilikuwa najiandaa kulipia hiyo azam sport kumbe ovyo tu!?

Hapo utapata Azam HD, man u, Liverpool, Madrid tu basi zingine utazisikia kwa jirani
 
Back
Top Bottom