Mimi ni Mmiliki wa kisimbuzi cha Azam, nimelipia package ya Sports. Cha kushangaza napata Azam Sport HD, Man Utd, Liverpool TV na Madrid TV.
Naomba kuuliza, hivi Fox Sport siyo channel ya michezo au Kombat Sport, MCS International Sport, hizi channel si za sports?
Kwanini hamziweki kwenye package ya sports?
Acheni kutuibia, kama mmeshasema channel za sports ni elfu 15, basi tuwekeeni channel zote za sports, na sio kutupiga changa la macho na hiyo Azam HD pekee. Au nyie hizi channel mnaziitaje kama sio za sports?
Acheni utapeli wa mchana kweupe tuwekeeni hizo channel kwenye package ya sports.
Au mmeanza kulewa Sifa kama DSTV?
Asante mkuu nilikuwa sijaiona hii post yako.
Kwanza AZAM ndio habari ya mjini,ukiikosa AZAM Tv basi jua dunia ya kasi imekuacha mbali sana.
Haya hoja yako:-
Siku zote maskini kama mie ukimpa offer basi na yeye atatoa offer yake ya kulazimisha na kufanya haelewi ulichomuambia na hii hadi kwenye kampuni za sim ni tatizo,na ndio maana huwekewa maneno ya Kigezo na masharti kuzingatiwa.
Azam walitangaza offer kulingana na marketing strategic plan zao kwa wateja wao kwa kipindi husika.Na kwa taarifa yako tu mkuu,Hawa jamaa huwa hawakurupuki.Ila kama umenunua Decoder juzi naweza kusema wewe ni mgeni kwao,ila sie tulionunua zamani tunaona kasi yao ya ajabu.
Kuhusu Channels za Sports,wao hawakusema kwamba wataweka zote,waliweka kwa maelezo yao.
Hata Dstv ambapo watu wanalipa zaidi ya laki moja kwa mwezi pia Channels nyingi tu za michezo hawana,ila sema tu kwa vile wamechukua zile maarufu ndio tunaona wamekamilika.Sasa itakuwa hiyo tsh:elf 15?
la pili hakuna mtoa huduma yoyote Duniani wa Television mwenye Channels zote za michezo,hilo Tambua kwanza.
Sasa kaka hujaibiwa kitu,na ndio maana umetoka Dstv umehamia Azam ulimwengu wa burudani,mambo huku Azam ni taratibu ila kwa uhakika.
Unanikumbusha wakati nasoma High School,ilikuwa kila siku ni ugali maharage,baada ya muda ikaja offer ya Wali na nyama kwa wiki mara moja,aisee tuli enjoy mpaka basi,yaani ikifika jioni unakoga kwanza ndio unakula kwa pozzz.
Sasa kilichofuata baada ya kuzoe,watu wakaanza kusema nyama zenyewe unapewa vipande viwili tuu,mara nyama zenyewe mafuta hazina,mara nyama zakulala,wengine walienda mbali na kusema nyama za mbwa.Sasa binaadam kama wewe wapo wengi,unalipa kidogo unataka makubwa.
Ushauri:
Jaribuni sana kufuatilia vipindi vya AZAM,huwa wanatoa maelezo na mikakati yao ya baadae,ndio utajua wapi wanaelekea,ila ukikurupushwa na mtu tu kwa kukusifia ubora wa AZAM bila kujua ndio matokeo yake haya.
Najua hizo Channels una refer kwenye Cables ambazo wale ni wazee wa kufvyonza,sasa huwezi kulinganisha na Brands kubwa kama hizi ambazo zinaheshim sana Rights za chennels husika.
Kuna channels hasa nyingi za Sports huwa kuna makubalianao ya kuzilipia na mazungumzo huenda Taratibu na ndio maana AZAM waliahidi kwamba ARSENAL TV nao wapo kwenye mazungumzo ili kujua itakuwaje hapo mbele.
Sasa usifikirie kusema sports chennes basi ni kugeuza Satelite ya AZAM na kurusha zote.
Vumilia kaka makubwa yanakuja,uliona macoverage ya kufa mtu kwenye uchaguzi.Basi hao ndio AZAM TEAM
Zanzibar Spices
Mwana familia wa wateja wa AZAM Tv