Athari ya kuoa mapema kwa vijana

Athari ya kuoa mapema kwa vijana

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,156
Reaction score
55,652
Unakuta kijana kula yake ni ya shida, halafu anakimbilia kuoa akitegemea maisha yanaweza kubadilika na kuwa mazuri; hii ni sawa sawa na kubahatisha.

Unakuta kijana anaanza kuchakaa mapema, kutokana na kujibebesha majukumu ambayo bado kuyapangilia.

Nashauri vijana tuoe tukishakuwa na uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku, hakuna mapenzi yasiyohitaji hela; lasivyo utapigiwa mpaka uchanganikiwe.
 
Hata ukiisha kuwa na uhakika wa milo mitatu kama hauna jaliwa la kuoa hautaowa.
Kuoa ni majaliwa kama yalivyo majaliwa mengine.

Nimekaa na mwanamke kwa miaka kumi sasa tokea 2009 nikiwa sina uhakika wa hio milo mitatu na pengine hata huo mmoja! Lakini tumeweza kutoboa japo sio kwa ukamilifu wa moja kwa moja lakini kuna uafadhali wa kijana kuoa mapema.

Ila tu kwa wenye akili ya kuanzisha familia sio kila anaweza kuoa anatakiwa kuoa, maana ndani ya kuoa kuna zaidi ya hio kuoa. Ndio maana mleta mada umekuja na hitimisho hili lakini sio kila anaweza kuoa anapaswa kuoa hata kama anao uwezo kiasi gani la! Bali kwa waliojaliwa. Na hawa huwa hawahitaji kuwa na kitu zaidi ya moyo.
 
Unakuta kijana kula yake ni ya shida, halafu anakimbilia kuoa akitegemea maisha yanaweza kubadilika na kuwa mazuri; hii ni sawa sawa na kubahatisha.

Unakuta kijana anaanza kuchakaa mapema, kutokana na kujibebesha majukumu ambayo bado kuyapangilia.

Nashauri vijana tuoe tukishakuwa na uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku, hakuna mapenzi yasiyohitaji hela; lasivyo utapigiwa mpaka uchanganikiwe.
Kuna faida kubwa sana kwa kijana kuoa mapema,moja wapo kuondokana na Zinaa)
Hili swala la ridhiki yupo mbora na mpangaji kama umekosa basi umekosa....!
 
Mkuu sometimez vijana wanawahi kuoa kutokana na influence ya wazazi au watu wa karibu..utasikia wewe ngoja ushtuke una miaka 40 huna mtoto wala nn
Ndio, yaani ukiwa na miaka arubani na huna mtoto umepata hasara ya maisha hata km unapesa vipi, umri wako tayali unakua umeenda sana Kwa wew kuihudumia familia yako. Watoto wako utawalea ukiwa babu

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
 
Unakuta kijana kula yake ni ya shida, halafu anakimbilia kuoa akitegemea maisha yanaweza kubadilika na kuwa mazuri; hii ni sawa sawa na kubahatisha.

Unakuta kijana anaanza kuchakaa mapema, kutokana na kujibebesha majukumu ambayo bado kuyapangilia.

Nashauri vijana tuoe tukishakuwa na uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku, hakuna mapenzi yasiyohitaji hela; lasivyo utapigiwa mpaka uchanganikiwe.
Ila pia ukioa mapema makes more sense.otherwise utatumia pension kusomeshea,hiyo ni hatari zaidi asikwambie mtu
 
kuoa mapema kwa wengine kunawasaidia kufocus katika utafutaji wa fedha, kuliko kuhangaika na wanawake, sababu anae mwanamke wake nyumbani.....

Pia kuwa na your own team (family hata ya mke na mume tu bila watoto) ni very special thing kama mtatengeneza akili moja kupambana na maisha

Sema pia kuwahi kuoa inabidi uwe na moyo wa upambanaji sana, usitegemee kitu kimoja ndio kikuingizie pesa, maana mahitaji yanaongezeka kila wakati na familia yako ikiishaanza karibisha watoto basi hata ndoto zako nyingine zinaweza kufa bila kupambana

So ni 50/50 inategemea na jinsi utakavyojipanga na upambanaji wako basi.
 
Mbona mnatutisha ambao hatujaoa na tunapenda kuoa ila kesho yetu ni ya kuungaunga sana, umri nao unasogea, tufanyeje sasa
 
O
Mbona mnatutisha ambao hatujaoa na tunapenda kuoa ila kesho yetu ni ya kuungaunga sana, umri nao unasogea, tufanyeje sasa
Oa mapema mkuu usiwe na hofu ya ridhiki,hakuna kiumbe anatoa ridhiki ispokuwa muumbaji tu...

Kwanza itakupa chachu ya kupambana
Pili itakupa moyo kutulia
Tatu utaepukana na maradhi
Nne utawalewa watoto wako mapema..
 
Unakuta kijana kula yake ni ya shida, halafu anakimbilia kuoa akitegemea maisha yanaweza kubadilika na kuwa mazuri; hii ni sawa sawa na kubahatisha.

Unakuta kijana anaanza kuchakaa mapema, kutokana na kujibebesha majukumu ambayo bado kuyapangilia.

Nashauri vijana tuoe tukishakuwa na uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku, hakuna mapenzi yasiyohitaji hela; lasivyo utapigiwa mpaka uchanganikiwe.
Kuchelewa kuoa Ni kujichelewesha kuanza majukumu.Nakuchelewa kuanza majukumu maana yake Ni kuchelewa kumaliza majukumu.Oa ukiwa bado una nguvu ya kupambana kutafuta pesa na kulea watoto.Cha msingi Ni kutafuta mke mwenye akili ya maisha na sio wale wakaa vibarazani kupaka inna na kupiga umbea..
 
Kuchelewa kuoa Ni kujichelewesha kuanza majukumu.Nakuchelewa kuanza majukumu maana yake Ni kuchelewa kumaliza majukumu.Oa ukiwa bado una nguvu ya kupambana kutafuta pesa na kulea watoto.Cha msingi Ni kutafuta mke mwenye akili ya maisha na sio wale wakaa vibarazani kupaka inna na kupiga umbea..
Mtoa mada hajawa specific kuoa mapema kuanzia umri wa miaka mingapi minimum ,na kuchelewa kuoa n miaka mingapi maximum,mn kuna vijana wanaoa ana miaka 16 au 17 hzo zinaitwa ndoa za utotoni je nako nikuwahi kuoa?
 
Back
Top Bottom