ATCL kwa mapungufu haya hamtadumu

ATCL kwa mapungufu haya hamtadumu

JOHNKEKE

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2011
Posts
1,310
Reaction score
1,466
Nimeamua kwa moyo safi kusafiri na ATCL kwa sababu nyingi tu, ambazo sitazitaja sababu ni uamuzi binafsi.

Kilichonisikitisha sana ni kwamba bado mko usingizini, business as usual!
Kwa muda wa wiki 2 sasa nimekuwa nikitembelea ofisi zenu katika moja ya mikoa ya kaskazini ili kununua return ticket ya Dsm, kwa kipindi cha kati ya tarehe 4/2 na 11/2.

Cha ajabu na kusikitisha mara kwa mara nimekuwa nikiambiwa labda uje kesho sababu makao makuu bado hawajaweka kwenye mtandao schedules za tarehe za mbele kuanza tarehe 9/2!

Na hata ukiingia kwenye website yao unashindwa kukata tiketi kwa tarehe hizo bila maelezo yeyote yanayoeleweka!

Wakati mashirika mengine ya ndege wala uhitaji kwenda ofisini, kuna options nyingi za kulipia tiketi.

Lawama hizi naitwisha menejimenti ya shirika, kama mmeshindwa kuwajibika si muachie ngazi!


UPDATES
Pamoja na juhudi zangu za kuitumia ATCL kwenda na kurudi, ilishindikana. Ikabidi nikate fastjet kwa kwenda.
Wakati wa kurudi tar 12/2 ndiyo kwa mara ya kwanza nikapanda ATCL. Niliyoyakuta huko ilinisikitisha zaidi!
Abiria hatukufika hata 20, nadhani tulikiwa 14 kwenye ndege inayobeba Abiria zaidi ya 60! Viti vingi vilikuwa vitupu! Kwa kweli roho iliniuma hasa nikikumbuka gharama ya kununua hizo ndege!
Ningekuwa nahusika ningem "fire" Business Director/Manager. Ndege ni nzuri, nauli ni cheap, sh 140,000 one way ukilinganisha na fastjet 220,000! bado inakosa abiria!
 
Alafu bado tunasikia hitlafu kila cku mimi nilikuwa nataka kusafir nayo nimeghairi bora nipande fast jet hamna duka la roho na bia zilivyo tamu niziache hiv hiv
 
Hiyo ndio shida ya serikali kujiingiza kwenye biashara za ushindani. Utakuta ATCL ni kichaka kinachoajiri wake na watoto wa wakubwa ambao hawachangii lolote kwenye ufanisi wa shirika. Hao ndio wanaotumia simu za shirika kuendeleza vikampuni na miradi binafsi, wanatumia computer za shirika kuchat kwenye social media. Baya zaidi watu hao hao hawawezwi kuwajibishwa kwa connections zao!
 
Mimi sitaraji jipya kwenye muundo huu wa utendaji na usimamizi. Masuala ya kitaaluma yanafanyika kisiasa na ya kisiasa yanafanywa kwa nguvu ya dola.

Ingia leo kwenye tovuti ya VETA na NIT, utashangaa na kama huna kitambi unaweza timua mbio. Chuo kinachojinasibu kuwa KINAFUNDISHA IT, website yake iko hoi. Lakini humo humo kwenye page ambazo hazijakuwa updated tangu 2009 utaona mtu kaandika wanafundisha WEB DESIGNING.

Hii ndio Tanzania na hao ndio watendaji wetu linapokuja suala la teknolojia ya mawasiliano. Jana nilienda HELSB kusubmit Payment Details za waajiriwa wa kampuni yetu wanaodaiwa. Nimewekwa kwenye benchi 67minutes nasubiri karani anatafuta taarifa za benki kwenye faili lenye kurasa si chini 200 kwa kalamu. Najiuliza, ufanisi uko wapi na yapi ni mazuri ya IT kwa nchi yetu?

Hapo ATCL si ajabu ukakuta vijamaa fulani vimeajiriwa kufanya wajibu huo. Vyenyewe vitakuwa aidha, vibrazamen au tuzee. Kama ni wazee, I reserve my comments na kama ni vijana basi huwa ni SSK (Suti Safi Kibaruani). Mashati saaafi ya dukani kama waimba kwaya, kikamba kimeshuka shingoni na kutokomea mfuko wa shati na kabeji saaaafi IT. Kazi kuvaa suruali za model na viatu vya kuchongoka mbele, website ya kampuni kichefuchefu. Wanapitapita tu makoridoni wakivuta muda ifike lunch time wakale juice na sambusa 2 kama mademu...pambaf!
 
Bado tupo nyuma sana.....hata kwenye mabasi ya mwendo haraka abiria wanahudumiwa kama ng'ombe jioni na asubuhi ni lazima kupigania,bora zingeachwa daladala zetu
 
Adminstration haija kaaa sawa maan kuna hudum nyingine mtrja hapaswi kusumbuka kabisa
 
Aaah
Alafu bado tunasikia hitlafu kila cku mimi nilikuwa nataka kusafir nayo nimeghairi bora nipande fast jet hamna duka la roho na bia zilivyo tamu niziache hiv hiv
Ah ah, bia! Siyo mke na watoto wapendwa?
 
Watanzania wengi bado tupo gizani katika mambo ya figisu figisu na hila zinazofanywa na makampuni makubwa na hata wapinzani toka nchi jirani ktk kuhakikisha wao wapo juu sikuzote so kinachotakiwa kikubwa ni kuwa wazi kama mkuu hapa alipoamua kuleta hili swala humu maana nikweli bado kuna vijihujuma vingi vinaendelea ilimradi tu kunafaisha watu flani flani adui wa maendeleo ya nchi yetu pendwa Tanzania
 
Hiyo ndio shida ya serikali kujiingiza kwenye biashara za ushindani. Utakuta ATCL ni kichaka kinachoajiri wake na watoto wa wakubwa ambao hawachangii lolote kwenye ufanisi wa shirika. Hao ndio wanaotumia simu za shirika kuendeleza vikampuni na miradi binafsi, wanatumia computer za shirika kuchat kwenye social media. Baya zaidi watu hao hao hawawezwi kuwajibishwa kwa connections zao!
Lakini kuna mashirika mengi ya ndege yanayomilikiwa na/kwa kiasi kikubwa na serikali na yanafanya vyema. Mfano Ethiopia, Kenya, Qatar Airways n.k

Mimi nafikiri ni kuongeza usimamizi na uwajibikaji.
 
Mimi sitaraji jipya kwenye muundo huu wa utendaji na usimamizi. Masuala ya kitaaluma yanafanyika kisiasa na ya kisiasa yanafanywa kwa nguvu ya dola.

Ingia leo kwenye tovuti ya VETA na NIT, utashangaa na kama huna kitambi unaweza timua mbio. Chuo kinachojinasibu kuwa KINAFUNDISHA IT, website yake iko hoi. Lakini humo humo kwenye page ambazo hazijakuwa updated tangu 2009 utaona mtu kaandika wanafundisha WEB DESIGNING.

Hii ndio Tanzania na hao ndio watendaji wetu linapokuja suala la teknolojia ya mawasiliano. Jana nilienda HELSB kusubmit Payment Details za waajiriwa wa kampuni yetu wanaodaiwa. Nimewekwa kwenye benchi 67minutes nasubiri karani anatafuta taarifa za benki kwenye faili lenye kurasa si chini 200 kwa kalamu. Najiuliza, ufanisi uko wapi na yapi ni mazuri ya IT kwa nchi yetu?

Hapo ATCL si ajabu ukakuta vijamaa fulani vimeajiriwa kufanya wajibu huo. Vyenyewe vitakuwa aidha, vibrazamen au tuzee. Kama ni wazee, I reserve my comments na kama ni vijana basi huwa ni SSK (Suti Safi Kibaruani). Mashati saaafi ya dukani kama waimba kwaya, kikamba kimeshuka shingoni na kutokomea mfuko wa shati na kabeji saaaafi IT. Kazi kuvaa suruali za model na viatu vya kuchongoka mbele, website ya kampuni kichefuchefu. Wanapitapita tu makoridoni wakivuta muda ifike lunch time wakale juice na sambusa 2 kama mademu...pambaf!
Mkuu umewapa za uso
 
Mimi sitaraji jipya kwenye muundo huu wa utendaji na usimamizi. Masuala ya kitaaluma yanafanyika kisiasa na ya kisiasa yanafanywa kwa nguvu ya dola.

Ingia leo kwenye tovuti ya VETA na NIT, utashangaa na kama huna kitambi unaweza timua mbio. Chuo kinachojinasibu kuwa KINAFUNDISHA IT, website yake iko hoi. Lakini humo humo kwenye page ambazo hazijakuwa updated tangu 2009 utaona mtu kaandika wanafundisha WEB DESIGNING.

Hii ndio Tanzania na hao ndio watendaji wetu linapokuja suala la teknolojia ya mawasiliano. Jana nilienda HELSB kusubmit Payment Details za waajiriwa wa kampuni yetu wanaodaiwa. Nimewekwa kwenye benchi 67minutes nasubiri karani anatafuta taarifa za benki kwenye faili lenye kurasa si chini 200 kwa kalamu. Najiuliza, ufanisi uko wapi na yapi ni mazuri ya IT kwa nchi yetu?

Hapo ATCL si ajabu ukakuta vijamaa fulani vimeajiriwa kufanya wajibu huo. Vyenyewe vitakuwa aidha, vibrazamen au tuzee. Kama ni wazee, I reserve my comments na kama ni vijana basi huwa ni SSK (Suti Safi Kibaruani). Mashati saaafi ya dukani kama waimba kwaya, kikamba kimeshuka shingoni na kutokomea mfuko wa shati na kabeji saaaafi IT. Kazi kuvaa suruali za model na viatu vya kuchongoka mbele, website ya kampuni kichefuchefu. Wanapitapita tu makoridoni wakivuta muda ifike lunch time wakale juice na sambusa 2 kama mademu...pambaf!
Duh, kaka! Umeniongezea pia msamiati mpya, SSK!
 
Back
Top Bottom