ATCL kuanza safari za kwenda Afrika Kusini

ATCL kuanza safari za kwenda Afrika Kusini

Hii route ya dar-joburg imekua pasua kichwa sana. Kila anayejaribu kushindana na SAA kwenye hii route anachemka. Kuna wakati precision nadhani walijaribu wakashindwa..fastjet walijaribu wakashindwa..kulula/british airways walijaribu wakashindwa. Ngoja tuone kama air tanzania wataweza. Kukiwa na ushindani angalau bei itashuka maana saa hizi SAA anajichagulia tu nauli ya kutoza maana yupo peke yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu siku nyingine tumia malawian airline maana ni cheap kidogo
 
Mkuu siku nyingine tumia malawian airline maana ni cheap kidogo
Yes nafahamu. Nilikua nazumgumzia direct non stop route. Najua za indirect karibu zote ni cheaper than SAA. Wapo hao malawian..kuna rwandair..ethiopian..KQ...wote ni cheaper than SAA. Ila SAA ni the fastest kwa sasa maana haina connection. Air tanzania sasa watachuana nae kwenye direct route

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ile safari ya India na China mpaka leo imekuwa story na sasa Afrika kusini
 
View attachment 1075093
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) karibuni linatarajia kuzindua safari mpya za kwenda Afrika Kusini, ambapo ndege ya kwanza kuruka kwenda jijini Johannesburg itaruka Julai mwaka huu.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi amesema kuwa watatangaza nauli na kuanza kutangaza safari hizo watakapoanza kuuza tiketi.

Hatua hii kubwa ya kuendelea kupanuka kwa shirika hilo inakuja ikiwa ni miezi miwili tangu lilipozindua safari mpya za kwenda Harare nchini Zimbabwe na Lusaka nchini Zambia.

Safari ya kwenda Afrika Kusini itakuwa ni safari ya tano ya kimataifa kuzinduliwa na ATCL baada ya Harare, Lusaka, Bujumbura na Entebbe.

Baada ya kuzindua safari hiyo, Matindi amesema kuwa shirika hilo litajiandaa na safari za kwenda Mumbai (India) na Guangzhou (China) ambapo maandalizi yake yamefikia katika hatua nzuri.

Ameongeza kuwa safari hizo zitazinduliwa mara tu mazungumzo na mamlaka kwenye nchi hizo yatakapokamilika.

Kwa sasa shirika hilo linalofufuka baada ya kutofanya vizuri sokoni kwa miaka mingine lina ndege nane ambazo ni, Bombardiers Q-400s tatu, Airbus (A200-300) mbili, Fokker50, Fokker28 na Boeing 787-8 Dreamliner.
Hiyo route ni pasua kichwa muulize KQ au Fast jet. Mmbabe ni SAA
 
Laiti ungejua SAA ndio wanamatatizo makubwa ya kifedha. Serikali kila mara inabidi iwape ruzuku maana shirika linapata hasara kila mwaka.
Sent using Jamii Forums mobile app

..Nini kimewasibu SAA wakapata hasara.

..South Africa wanakadiriwa kupokea abiri milioni 17 kwa mwaka.

..ni kati ya nchi zinazoongoza kwa wasafiri wa anga Afrika.

..Tanzania inakadiriwa kupokea abiria milioni 1.7.


 
Vipi jamani angali namna ya kupeleka ndege Kongo Lubumbashi
 
Wacha niwe muwazi atcl watafaulu domestic routes tuu! Huko nje ni kugumu acha watapigwa za uso kila siku! Wakamate soko la ndani thats all wanachoweza, wakitoka nje wanachinjwa kibiashara watarudi kama mbwa koko mkia kaufyata!
 
Yes nafahamu. Nilikua nazumgumzia direct non stop route. Najua za indirect karibu zote ni cheaper than SAA. Wapo hao malawian..kuna rwandair..ethiopian..KQ...wote ni cheaper than SAA. Ila SAA ni the fastest kwa sasa maana haina connection. Air tanzania sasa watachuana nae kwenye direct route

Sent using Jamii Forums mobile app
Noted
 
Back
Top Bottom