yamindinda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2011
- 1,581
- 1,318
KAKOSEA NJIA.Mbunge wa wa Tarime John Heche amewaonya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuwa kama wanataka kumjibu Askofu Zacharia Kakobe kwa niaba ya serikali iliyopo madarakani basi wajibu kwa hoja na siyo kuropoka.
Heche amesema hayo ikiwa ni siku moja baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa huo, Frank Kamugisha kumtaka Askofu Kakobe aende kufanya toba na kisha kuwaomba radhi wana CCM wa Dar es salaam kwa kuacha miiko ya kidini na kushindwa kutumia busara na kisha kusema hovyo.
Akizungumza jana na Wanahabari Kamugisha alivitaka vyombo vinavyohusika na sheria vihakikishe hakuna mtu anayepata fursa ya kumtukana au kumbeza Rais wa nchi na kufafanua kwamba Rais amejipambanua katika kuwasaidia wananchi na anafanya mambo hayo kwa udhati wa moyo wake hivyo mtu anyebeza moja kwa moja atakuwa msaliti.
Heche amandika kwenye ukurasa wake wa Twitter na kusema kwamba "CCM kama mnataka kujibu hoja za Askofu Kakobe kwa niaba ya Rais Magufuli na Serikali jibuni kwa hoja, sio kuropoka! kazi za wachungaji ni kukemea maovu yote yaliyopo duniani, watu wanapotea, wanapigwa risasi, wanaokotwa baharini, sheria za nchi hazifuatwi, haya yatakemewa na kila mtanzania" Heche.
Source eatv news.
Na Thadei Ole Mushi.
[HASHTAG]#Mahubiri[/HASHTAG] ya jana ya sikukuu ya Christmass yalitanguliwa na Mkutano wa maaskofu ambao kwa pamoja walikubaliana kuweka agenda zinazofanana katika mahubiri yao. Huu ndio utaratibu wao na ndio maana kwa pamoja walizungumzia, amani ya nchi, Hali ya kisiasa, umoja na uchumi wa nchi.
[HASHTAG]#Hakuna[/HASHTAG] walipokubalia mtu akamshambulie mtu mwingine kwenye mimbari ya kanisa lake na sio utaratibu. Ubaya zaid unatumia story za vijiweni kutaja jina la mtu ambaye ndiye image ya nchi.
[HASHTAG]#Kufanya[/HASHTAG] hivyo ni kuaminisha jamii kuwa Rais wa nchi hafai na ni mdhambi na anapaswa kwenda kutubu. Ni ujasiri wa aina yake huu nimeuona. Hakuna kanisa linaloweza kufanya hivyo pale Urusi Kwa Valdimir na ndio maana Urusi inaendelea.
[HASHTAG]#Lazma[/HASHTAG] nchi iwe na one Chain of Comand si kila mtu anapaswa kutoa kauli. Hapa Askofu katugawa badala ya kutuunganisha kama wananchi.
[HASHTAG]#Taasisi[/HASHTAG] ya Urais ina hadhi yake haipaswi kutajwa tajwa kwa Tuhuma tu...... njia aliyotumia lazma aambiwe kuwa haifai. Hawezi kuachwa akashambulia tu mtu kwa tuhuma.
[HASHTAG]#Sijawahi[/HASHTAG] kusikia mahali katika mimbari ya Dini kasisi au Shekhe kumshambulia mtu wazi wazi kuwa ni Mdhambi hata Yesu hakufanya hivyo japokuwa alikuwa na uwezo wa kuona yaliyofichika. Hakuwahi kuhukumu moja kwa moja kuwa ni mdhambi wewe. Kwa hili mm binafai nakataa hakutumia njia iliyosahihi kufikisha ujumbe wake.
KILA ZAMA NA KITABU CHAKE.
Nani anaifahamu nadharia ya Hot Stove Rule ya McGregory.
Serikali ya JPM imeamua kutumia nadharia hii katika utekelezaji wa majukumu yake. Ni nadharia iliyopaswa na inayofaa sana kutumia na nchi kama Tanzania ambao watu wake wanataka kupiga Soga zaidi kuliko kazi.
INAFANYAJE KAZI.
Hii huhusika na kutoa mwongozo wa nini kitakupata kama utaweka mkono wako kwenye jiko la Stove linalowaka. Kama utavunja sheria zilizowekwa kwa kutumia nadharia hii adhabu utaipata katika mazingira yafuatayo.
1. Burns immediatelly:- Utachomwa haraka sana mara ushikapo jiko hilo. Na mhusika atatambua kuwa kachomwa kwa kuwa tu alilishika jiko hilo. Magufuli na serikali yake inavyokwenda hakuna subira hata kidogo. Nimeangalia kuanzia bungeni na nje ya bunge serikali hii haina muda wa majadiliano. Ukijichanganya wanakuchangamkia mara moja ni tofauti na ile ya mh Kikwete. Angalia hata wateule wake wanapokosea hakuna muda wa kusubiri kesi.......
2. Provides warning:- Ni kama ilivyo kwa jiko la stove kadri unavyosogeza mkono wako kuelekea kwenye jiko ndivyo hivyo joto huongezeka. Hii hutoa tahadhari kwa kitakachokukuta kama utaendelea kuusogeza mkono wako..........
3. Give Consistent punishment:- Hapa ni pale uhakika wa stove kurudia jambo lile lile kwa ufanisi ule ule. Kila ukishika utachomeka kwa kiwango kile kile bila kupunguza au kuongeza.Hii haitajalisha ni mara ngapi utakuwa umelishika jiko hilo. Ukishika mara moja utachomwa mara moja. Ukishika mara mbili utachomwa mara mbili na ukishika mara mia utachomwa mara mia.
4. Burn impersonally:- Kama jiko hili lilivyo litakuchoma bila kujua huyu ni nani. Moto wa jiko hauangalii huyu ni nani alimradi tu umejichanganya kuushika. Awe mtoto, mtu mzima, Askofu, Shekhe, Tajiri, Maskini au yeyote atachomwa tu kwa kadiri ya alivyoshika.
Ole Mushi.
0712702602