Askofu Pengo asema Muhimbili inatosha

Askofu Pengo asema Muhimbili inatosha

singidadodoma

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2013
Posts
4,394
Reaction score
1,538
12400783_1020620508002407_2428723273658187783_n.jpg
 
Wananiudhi sana watu wanaopost heading bbila maelezo. Jf ni uwanja wa great thinker sni vizuri ukajipanga kabla ya kupost
 
kwa hiyo anataka kusemaje kuhusu upasuaji wa tezi dume kufanyika nje ya nchi?
 
Inawezekana kabisa kuwa inatosha. Askofu Pengo akumbuke kuwa hata Hositali ya Temeke, Mwananyala, Ilala zinatosha. Hata vituo vya afya vya vingunguti, mbagala n.k. vinatosha pia. Suala ni uwezo wa kufedha wa kwenda huko. Kama huna kitu mfukoni au huduma za afya ziko mbali hata miti shamba inatosha. Gharama alizotumia Askofu wetu ni wangapi wanazimudu hapohapo Mhimbili?
 
Wewe mtoa hoja, sio wote tuna smart phone, tunaomba ufafanue habari yako tafadhali.
 
Inawezekana kabisa kuwa inatosha. Askofu Pengo akumbuke kuwa hata Hositali ya Temeke, Mwananyala, Ilala zinatosha. Hata vituo vya afya vya vingunguti, mbagala n.k. vinatosha pia. Suala ni uwezo wa kufedha wa kwenda huko. Kama huna kitu mfukoni au huduma za afya ziko mbali hata miti shamba inatosha. Gharama alizotumia Askofu wetu ni wangapi wanazimudu hapohapo Mhimbili?
Nafikiri au niseme naamini Serikali inajaribu kuwapa reassurance wananchi na viongozi mbalimbali kuwa hospitali ya moyo ya JK inaweza, kwa hiyo watakapokuwa wananyimwa vibali vya kwenda nje ya nchi kuwe na reference ya mtu maarufu.
 
Huu wala si uzalendo, ni maigizo. Angekuwa mzalendo angevunja MoU na Serikali, iliyokaa kiwiziwizi na kiupigaji. Anachofanya hapo ni PR, kucheza na umma...
Aione; Mohamed Said
 
Napata mashaka na mtumishi wa Mungu Pengo kujua kigezo alichotumia kutoa kauli hiyo.
Hivi anajua kuwa huduma aliyokuwa anapewa yeye pale haina tofauti na ya Rais kulingana na nafasi yake?
Jee anadhani hata babu toka Kimanzichana au kinda wa daladala naye atapata picha ya Muhimbili kama yeye?
 
pengo alienda muhimbili kama mgonjwa au mtafiti? jibu ni alienda kama mgonjwa, sasa asione huduma aliyoipata ya ki V.I.P kutokana na umaarufu wake na ushawishi wake akadhani kila mtanzania anafanyiwa hivyo akasema inatosha, anajiharibia heshima yake sana
 
You better research out kwa nn alisema hata hapo panatosha..........yawezekana kbs kuna pressure iliyompress mpaka akatoa kauli hyo. Kwa ufupi yapo magonjwa likuki yanayoweza kutibika hapa nyumbani lkn wapo viongozi wetu wachache wanaougua ugonjwa huo yet wanakimbilia nje.....hiyo tabia haitoi changamoto kwa wataalam wetu wa ndani kujitafiti na kujipa moyo kwamba wanaweza na hivyo kupressurize serikali kutoa huduma zinazohitajika.......Pengo ni wa kipogiwa mfano cyo uchovu tu kidogo......you take flight.....
 
Pengo aache kuhadaa uma, aombe akalazwe mwaisela au sewahaji ndio atuambie kama muhimbili panatosha au la
 
Mtu kalazwa wodi Private anawasemea wale wa Kajamba nani?
Ndugai ndo tumemtoa nje juzi tu.
 
ok, mi nimemwelewa anamaanisha inatosha kwa hiyo anawashangaa wanaoenda india, maana yeye pia alikua na uwezo wa kwenda nje ila akatibiwa hapahapa na akapona
 
Ndo maana huwa nasema ,siku hizi hakuna viongozi wa dini,kuna watoza ushulu tu,atuambie ghalama aliyotumia toka amelazwa ni sh.ngapi.na je mtanzania fukala anaweza akamudu,Pengo aacha kutufanya watoto,au kwa sababu anahudumiwa kwa sadaka zetu ,ndo maana hana uchungu?
 
Ila nilishangaa sana,kuandaliwa press conference hospitalin,yawezekana Pengo ni mtumishi wa Serikali.
 
Wabongo bwana hawana shukrani tupo kama kama masokwe akienda nje hoo wenzetu wanatibiwa ulaya sisi kajamba nani muhimbili akitibiwa nchini utasikia ana ekti mara katumia ela nyingi,shida tupu iv manaelewa kwamba kardinali ni nani ndio maana hata serikali ilitaka kuhagharimia.tuache unafiki
 
Askofu Pengo Tafadhali usiwakebehi walala hoi we we ulilazwa VIP ward mpaka Rais akakutembelea Mara 2 sisi tunalazwa kajamba nani usitucheke kiongozi
 
Back
Top Bottom