PostGE2025 Askofu Msoganzila: Hatuna sababu ya kujibu mijadala ya kijinga

PostGE2025 Askofu Msoganzila: Hatuna sababu ya kujibu mijadala ya kijinga

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Askofu wa Jimbo Katoliki la Musoma, Michael George Mabuga Msonganzila, amewataka waumini na viongozi wa dini nchini kutokubeba jazba wala kujiingiza katika mijadala ya matusi, lawama na kejeli inayoibuka mitandaoni na kwenye mikutano ya kijamii, akisema kuwa njia ya Kristo ni ya upole, uvumilivu, huruma na kutanguliza haki.

Akizungumza kufuatia mfululizo wa matamko kutoka taasisi kadhaa za Kikristo na Kiislamu kuhusu matukio ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu, huku baadhi ya kauli zikiishambulia Kanisa Katoliki kwa kile kilichoelezwa kuwa ni uchochezi dhidi ya amani ya nchi, Askofu Msonganzila amesema kuwa migogoro na kejeli haviwezi kuizima nguvu ya ukweli.

“Hamna sababu ya kuijibu, ni kuinyamazia tu wakati mwingine watu wakisema sisi tumeenda shule sio zamani, kwani kwenda shule ni shida? Shida ni kusoma, shida ni kuelimika, sasa kuzozanazozana katika misingi hiyo haina haja- ni kunyamaza kama Kristo aliyedhihakiwa: Wewe si ni mwana wa Mungu Jiokoe basi nafsi yako, Nyamaza kimya endelea kusali”, amesema.

Askofu Msonganzila amesisitiza kuwa nguvu ya maneno ya kupotosha haiwezi kuzidi uzito wa maadili, utu, na dhamira njema ya Kanisa, akionya kuwa matusi na vitisho ambavyo vimekuwa vikitolewa haviwezi kubadilisha msingi wa imani wala wajibu wa viongozi wa dini kusimama katika kweli.

“Mahangaiko yakitokea ndugu zangu tusiogope kwa sababu ndio Kristo amepitia njia hiyo, Kanisa Katoliki linaweza likateseka kwa njia za namna hiyohiyo na matishio mbalimbali: umemwaga ugali tutamwaga mchuzi, tutawakatakata- tusiogope Mungu yupo”, ameeleza.

Kauli ya Askofu Msonganzila imekuja wakati ambapo mjadala kuhusu nafasi ya viongozi wa dini katika kueleza ukweli wa kijamii na kisiasa umeendelea kushika kasi, huku baadhi ya taasisi za kiimani zikitoa matamko yanayopingana kuhusu misimamo ya Kanisa Katoliki na makundi mengine ya kijamii kuhusu mwenendo wa uchaguzi na matukio yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Tanzania.

 
Maaskofu nyinyi tulieni tu. Sisi waumini wa Kanisa Katoliki na wapenda haki wengine tuna uwezo wa kuwajibu kwa hoja hawa wahuni na wapenda ubwabwa wao.
 
Askofu Michael George Mabuga Msonganzila amesisitiza kuwa waumini na viongozi wa dini hawapaswi kujishughulisha na matusi, kejeli au lawama zinazotokea mitandaoni au mikutanoni. Njia ya Kristo ni ya upole, uvumilivu, huruma na kutanguliza haki, hivyo mara nyingine ni vyema kunyamaza badala ya kujibu chuki.

Amesema kwamba nguvu ya maneno ya kupotosha haiwezi kuzidi maadili, utu, na dhamira njema ya Kanisa Katoliki. Migogoro na vitisho hivi havina uwezo wa kubadilisha msingi wa imani, na viongozi wa dini wanapaswa kuendelea kusimama katika ukweli.

Askofu Msonganzila amebainisha kuwa hali ngumu ni sehemu ya njia ya Kristo. Waumini hawapaswi kuogopa, kwani Kanisa linaweza kuteseka kupitia changamoto na matishio mbalimbali, lakini Mungu yupo na anasaidia kuendeleza ukweli na amani.


 
Hebu mlinganishe huyu askofu na hili punga la kukata waandamanaji vichwa 😞

IMG-20251123-WA0008.jpg
 
Back
Top Bottom