Askofu Kakobe amesimamia neno

Askofu Kakobe amesimamia neno

Sipendi matusi kabisa,
Lkn nachukia zaidi MTU mnafiki zaidi hata ya mtukanaji,
 
Go to hell
Huna lolote katafute huruma kwenu....hapa hatina huruma wala hatuuzi huruma.
Huko hell utakwenda wewe mwenyewe kwani miye sina haja nako! Tatizo lako ni umaliziaji hafifu. Ulikuwa na hoja nzuri inayoamsha fikra za wenye ufahamu na wasahaulifu. Ila umeingiza uchafu ambao umechafua kile kisafi ulichokileta mezani. Tubu!
 
Huko hell utakwenda wewe mwenyewe kwani miye sina haja nako! Tatizo lako ni umaliziaji hafifu. Ulikuwa na hoja nzuri inayoamsha fikra za wenye ufahamu na wasahaulifu. Ila umeingiza uchafu ambao umechafua kile kisafi ulichokileta mezani. Tubu!
Atubu nani sasa wewe au mimi.
 
Calm down peoples,naona emotions ziko very high hapa,
watu tujifuNze kuvumiliana.

Hata nchi za watu mfano marekani kuna vyama vya siasa na vina wafuasi mbalimbali,
mfano chama cha Republican kinaungwa mkono na mapastor wa kilokole a wafuasi wao,na wako free ku critisize serikali ama mtu yeyote na hata kama democratic ndo wako madarakani,haina maana kuwa mapastor wa kilokole wakimcriticize obama basi watakuwa sio wazalendo,
wote sisi ni watanzania bila kujali huyu anaunga mkono cuf,cdm,ccm ama Act.
 
Hayo ni mawazo yake hauna haja ya kutukanana. Mimi pia sipendi kumfananisha mtu yoyote ktk biblia na amabye hajamaliza mwendo. Pia ktk biblia kila mtume nabii au mtumishi alikuwa na madhaifu na ubora ukiondoa Yesu pekee. Kuna manabii walikimbia wanawake kwa hofu tuu ya kifo. Je akitokea mtu Leo haogopi kufa atalinganishwa kumzidi yule nabii ? Hasha haitawezekana huo upinganifu utakuwa batili. Kila mtu na karama na kibali chake. Utakuta anaweza tokea mwingine akongea kama Kakobe lakini mwitikio ukawa tifauti kwa jamii na kwa serkali.
Yesu naye aliua nguruwe wa watu kwa kuwatumbukiza baharini. Hatuambiwi kama aliwalipa fidia wenye nguruwe!
Si sahihi kumuita hivyo binadamu mwenzako
 
Mimi kwA leo sisemi lolote maana kuna watu humu wanapenda kusifiwa tu kama yule bwana ukikosoa tu umekuwa adui shame on you....#mkatubu#
 
Mkuu, usually hawa ni watoto wa kizazi kipya. Hawana hoja wala adabu ya kuweza kusemeshana kwa staha. Wao hudhani kuwa kutukana hovyo ndiyo ujanja kumbe ni ujinga tu na utoto wa kifikra hata kimalezi na kimakuzi.

Ingekuwa zamani tungetukanana hapa mpaka ningekula ban lakini siku hizi nilishajifunza kupotezea tu. Dunia itawafunda !!!
Alaa kumbe "zamani" wewe ulikuwa kama yeye !!! Sasa unalalamika nini ! Hivi umejiuliza kipindi chako cha ujana ni wangapi waliathirika na kauli za ujana wako? Nikwambie huyo anayetukana leo kajifunza kutoka kwako. Yote hayo ni nyie mnaojifanya wakubwa, kufumbia macho na masikio; ukiukwaji KATIBA ambayo wameapa kuilinda. Hakuna Uhuru wa kuongea na Uhuru wa kukutana. Nyie wakubwa wa leo mnafumba macho, hamuoni kuwa Sheria naomba 5 ya Vyama vya Siasa, 1995 inavunjwa mchana kweupe. Nchi inaendeshwa kwa "matamko" yanayopingana na katiba na sheria za nchi, lakini bado leo kuna watu wanajiita "wakubwa" wenye busara !! Eti leo kasisi akimsifia Mkuu ni sawa; kasisi akisoma dua kumwomvea Mkuu ni sawa; lakini kasisi huyo akisema Mkuu upo "uchi" aaaha huyo ni mpotoshaji/mchochezi. Kasisi leo akisoma dua kuomba Mungu amponye LISSU, aaah huyo mchochezi. Mtu hata ukivaa tu nguo yenye picha ya Lissu ni mchochezi. Bado unajiita wewe una hekima na busara !!! Mungu Aliye Hai Anakuona.
 
Siku ya mkesha wa Mwaka Mpya Nakuja kuimba Haleluya Hapo Kanisani Full Gospel. Tusheherekee tuimbe,tuupokee mwaka mpya mbele za Madhabahu Takatifu ya Mungu. Tupokee baraka za mwaka 2018 kutoka Kwake Yeye Aliye Juu....Sifa na Utukufu apewe Bwana aliyetandaza nyota angani na mchanga ardhini. Yeye awezaye kuzihesabu nywele kichwani kwa mwanadamu, yeye atupaye mvua na jua.....Jina lake lihimidiwe. Eee Mola walinde watumishi wako dhidi ya mbwa mwitu wakali ambao wamevaa ngozi ya kondoo....Amen
 
Back
Top Bottom